Mwasapile
JF-Expert Member
- Apr 20, 2020
- 206
- 441
Yaani imekuwa kila mara nikipata pesa mke wangu analeta kamzozo.. Mpaka imefika mahala nawaza au hapendi nipate pesa!
Nikipokea mshahara mara zote anasema nitoe pesa yote benki nilete mezani. Ofcourse anaweza akawa na hoja zake kuwa hata zikikaa benki huwa tunazitumia na zinaisha haibaki hata senti. Nikimwambia pesa hazitolewagi zote benki haelewi hata kidogo anakuwa mkali sana na anazira
Pia analalama sana kuwa mimi ni mbinafsi kwenye suala la pesa; kitu ambacho nikijitathimini naona kama ananionea tu, over 90% of my income inaishia kwenye matumizi ya familia, sinywi pombe wala sihongi. I am a family man with three sons
Nikimuuliza mke wangu mbona unakuwa mkali kuhusu suala la pesa anazira huku akiniambia kwa kejeli "Samahani nimekuingilia kwenye pesa zako".
Na mara nyingi sana huwa ananilalamikia kuwa nafanya maamuzi yanayohusu pesa mwenyewe kwasababu yeye hana mchango wowote wa kipesa anaounesha kwenye familia; mke wangu ni mama wa nyumbani by default analea watoto watatu.
Imefika mahala mpaka natamani tubadilishane majukumu. Nikae nyumbani yeye akatafute hizo pesa ambazo huwa natafuta ili aridhike na aone kuwa ana mchango kwenye hii familia.
NIFANYAJE WANA JF?
Nikipokea mshahara mara zote anasema nitoe pesa yote benki nilete mezani. Ofcourse anaweza akawa na hoja zake kuwa hata zikikaa benki huwa tunazitumia na zinaisha haibaki hata senti. Nikimwambia pesa hazitolewagi zote benki haelewi hata kidogo anakuwa mkali sana na anazira
Pia analalama sana kuwa mimi ni mbinafsi kwenye suala la pesa; kitu ambacho nikijitathimini naona kama ananionea tu, over 90% of my income inaishia kwenye matumizi ya familia, sinywi pombe wala sihongi. I am a family man with three sons
Nikimuuliza mke wangu mbona unakuwa mkali kuhusu suala la pesa anazira huku akiniambia kwa kejeli "Samahani nimekuingilia kwenye pesa zako".
Na mara nyingi sana huwa ananilalamikia kuwa nafanya maamuzi yanayohusu pesa mwenyewe kwasababu yeye hana mchango wowote wa kipesa anaounesha kwenye familia; mke wangu ni mama wa nyumbani by default analea watoto watatu.
Imefika mahala mpaka natamani tubadilishane majukumu. Nikae nyumbani yeye akatafute hizo pesa ambazo huwa natafuta ili aridhike na aone kuwa ana mchango kwenye hii familia.
NIFANYAJE WANA JF?