Ufunuo: Hatari kubwa CHADEMA

Ufunuo: Hatari kubwa CHADEMA

Majaribu2013

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
952
Reaction score
1,050
Wanajukwaa,

Kwanza nianze kwa kutanabaisha mi si mwanasiasa, sina chama na sipendi siasa lakini siku kadhaa nilipata mafunuo haya, nikaamua kunyamaza cha ajabu nafsi inaniuma sana na mengi yameanza kutokea wacha niseme ukweli.

1. Kuna hatari kubwa sana inakuja CHADEMA endapo uongozi wa chama hiki hautachukulia umuhimu unabii huu. Katika mafunuo haya nimethibitishiwa kwamba Mungu anampango wa kuliokoa taifa la Tanzania kupitia chama hiki, na amesema ni lazima ataonyesha uwezo wake viongozi wa CHADEMA muondoe wasiwasi.
2. Hatari kubwa inayoweza kuwapata mtakuwa na mapigo makali sana kwa sababu ya kwenda kinyume na taratibu au njia Mungu aliyowapangia. Hamfuati lile wingu lilikuwa linaongoza wana wa Israel, mnataka kufanya kama Yona ole wenu kwani hata vifo vitawapata. Kwanini mnaogopa wakati Mungu yu nanyi? Hatari kubwa sana.

Hatua za kuchukua.
1. Zipuuzieni tuhuma zote zinazotolewa na CCM mwangalieni nyoka wa shaba, achaneni na hawa nyoka wadogo wadogo.
2. Mnatakiwa kufanya maamuzi magumu bila kupenda, njia ya wazi imewekwa machoni kwenu. Kuna kiongozi mmoja mkubwa ndani yenu si wa KWENU ni Yuda ndani ya wanafunzi wa Yesu msiogope huyu hatafanya kitu juu yenu ila mnatakiwa mumuondoe mapema
iwezekanavyo, hana madhara kwa wanachama kama mnavyodhani. Huyu anajulikana na anajadiliwa sana saivi kwa usaliti.
3. 2015 mtashinda ila kutakuwa na vita vikali sana msipofuata haya hamtaingia IKULU na kutatokea vita Tanzania. CCM wataiba sana kura, na watajitangaza washindi.
Katika hili fanyeni hivi,
Mungu anasema hamtashinda kwa kupambana nao vita au kusimamia kura, ila mnatakiwa kuwa na kikundi cha sifa na maombi, na kianze kazi sasa. Nyinyi mtamwimbia Mungu na atawapigania nyinyi mtakuwa mnamwimbia nayeye anawapigania kama taifa la mfalme
Yehoshafati.

Niko tayari kuwasaidia katika hili la timu ya maombi.

Zaidi tuwasiliane.
 
Tumeanza na Mungu na tutamaliza na Mungu, people'sssss powerrrr!? Haya tuchangeni sasa pesa za kukiendesha chama. Lema chukua kapu na uzunguke kuchukua michango ya makamanda. People'sssss powerrrr!? Mwisho wa siku pesa zinazochangwa na wafuasi walalahoi zinatumika katika utalii wa slaa na demu wake, zinajengewa mahekalu ya viongozi wa chadema bongo na ughaibuni n.k na mwisho ni people's power.
 
Wanajukwaa,
Kwanza nianze kwa kutanabaisha mi si mwanasiasa, sina chama na sipendi siasa lakini siku kadhaa nilipata mafunuo haya, nikaamua kunyamaza cha ajabu nafsi inaniuma sana na mengi yameanza kutokea wacha niseme ukweli.

1. Kuna hatari kubwa sana inakuja CHADEMA endapo uongozi wa chama hiki hautachukulia umuhimu unabii huu.
Katika mafunuo haya nimethibitishiwa kwamba Mungu anampango wa kuliokoa taifa la Tanzania kupitia chama hiki, na amesema ni lazima ataonyesha uwezo wake viongozi wa CHADEMA muondoe wasiwasi.

2. Hatari kubwa inayoweza kuwapata mtakuwa na mapigo makali sana kwa

Wewe ni Nabii au Mtume? au ni Nabii na Mtume kama Mwingira?
 
Unajua mafunuo wewe? Stress za ndoa zinakuchanganya.

Mkuu, hata mie nimemshangaa sana huyu mburula. naona viroba vya pale kinondoni vimemlewesha asubuhi hii na ndo maana katoa uharo huu. eti ufunuo!
 
Nafahamu ufunio wa mtume na nabii Mwingira kuhusu kijana wa Upinzani aliyekuwa machachari na kupewa mil. 200. Na ni Zitto tu
 
Hapo mwisho umesema upo tayari kuwasaidia ktk timu ya maombi kivipi yani bure au? Na unadhani CDM wakifanya hivyo wa Islam wataichukuliaje?[naamini kabisa wewe ni mlokole] sasa kama ni maono umeoneshwa huwa hayazuiliki ni lazma yatokee kama ilivyopangwa amigo
 
Hiki ndio kibwagizo cha makamanda "TUMEANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU "halafu mwisho utawasikia wakiimbishana peole's power. Mimi naichukulia kauli hii kama dhihaka kwa Mwenyezi Mungu alietasika na utukufu.

Kumbe mmeanza na MUNGU katika kufanya haya maovu yenu yafuatayo?


  • Mmeanza na Mungu kula ruzuku ya chama mnayopokea kutoka serikalini katika kujenga mahekalu kwa kisingizio @ katibu mkuu hawezi kuendelea kuishi katika nyumba ya kupanga ni hatari kwa usalama wake. Hivi kujimilikisha kienyeji pesa ambayo inatokana na kodi ya walalahoi ambao hata mlo mmoja wa siku kwao imekuwa ni kitendawili MUNGU anapenda?
  • Mmeanza na Mungu kuratibu mipango miovu ya kuwadhuru watanzania ili kijitengenezea mazingira ya kuonewa huruma na wananchi na mwisho kufanikiwa kwa lengo lenu la kuingia ikulu? Hivi kweli MUNGU anapenda vitendo hivyo? Kumbukeni mlichofanya pale Arusha kulipua mabomu katika mkutano wenu na kufuatiwa na mkusanyiko batili ambao ulipelekea kupotea maisha ya watu akiwamo kijana mdogo Mussa Mtoi aliekuwa anatoka kwenye mambo yake. Kumbukeni igunga, Mauaji ya daudi Mwangosi, kifo cha marehemu chacha Wange ambacho inasemekana kimeratibiwa na Mbowe, kumbukeni habari za sumu, kulegeza tairi za gari la zitto ili kumuua, n.k.
  • Mmeanza na Mungu kuwasingizia binadamu wenzenu kuwa ni mafisadi kisa tu wanataka kugombania nafasi mbalimbali za juu katika chama chenu?.
  • Mmeanza na Mungu sikuhizi kudai posho ziongezwe kwa wabunge huku mkijinadi kama watetezi wa wanyonge?.
  • Mmeanza na Mungu kwenda kujenga majumba ya kifahari ughaibuni huku mkiwashakiza walalahoi waaandamane ili kikinuka nyinyi mkimbilie nje ya nchi mkale zenu kuku kwa mirija mkiwaacha walalahoi wakiteseka?

  • Mmeanza na Mungu kueneza chuki miongoni mwenu ya kuwachukia na kuwabagua wanachama wenzenu kwa madai ya kinafiki yasio na ushahidi wa kueleweka?.
​ To mention a few.

Nakuombeni mumheshimu MUNGU na msililitaje bure jina la Mungu hata maandiko yatuonya ya kwamba "usilitaje bure jina Mungu wako".
Akhsanteni kwa kunisoma.
 
we vipi.....kwani chadema ni kanisa??? CHADEMA is not a one man army....!!!!! toa utabiri wako hapo.

huko juu ulianza vizuri but mambo ya kuwepo kikund cha mapambio na kusali umechemka..
 
Anatafuta sokn jpili hii,sadaka haitoshi !eti tuwasiliane, tuwasiliane na wewe ili iweje?? ....manina
 
Hakuna mambo ya kitaifa ya kujadili zaidi ya kushinda hapa mtandaoni kumtaja Mbowe na Slaa? Tembo wanaisha. Kinana anamaliza tembo wetu. Hamlioni hilo isipokuwa Slaa na mbowe tu?

Katika mapambano yoyote, Amiri jeshi anatakiwa kujenga umoja kwa jeshi na watu wake ili kupata ushindi. hatari ya umoja kupotea lazima atolee msimamo ili asivunje moyo wengine. Mgogoro huu unabadili mwelekeo wa mapambano ndiyo maana unajadiliwa. Viongozi itisheni vikao halali lijadiliwe upepo upite. Kosa kubwa ni kufanya kila kiongozi hadi mfagiaji kuwa Msemaji wa Chama mtandaoni.
 
Viongozi wa CHADEMA muwe mnawapa na chakula hawa vijana sio mnawapa viroba tu!
 
Back
Top Bottom