Ufugaji wa Bata Mzinga, Bata Bukini na Kanga: Maoni, Ushauri, Utaalamu na Masoko

G-son

Member
Sep 5, 2008
68
17
Wana JF Habari za mapumziko ya sikukuu ya X-mas.

Leo nina jambo nataka uliza. Nimepata fununu kuwa katika kipindi cha hivi karibuni biashara ya mayai ya Kanga imekuwa nzuri sana kwani yai linafika hadi Tsh 1000 hasa kwa Jijiji Dsm.

Mimi huwa najishughulisha sana na ufugaji wa kuku wa kienyeji na niliposikia hii biashara mpya inayolandana na nifanyayo nikavuitwa, ila sina taarifa za kutosha kuanza kulifanyia kazi. Hivyo nimeona nililete hapa jukwaani ambapo kuna utaalam wa kila aina ili kunifungua macho.

Kwa kuanzia tu,
(1) Je ufungaji wa Kanga unakuwaje ukiliganisha na wa Kuku?
(2) Kuna sehemu maalum ambapo naweza pata hawa Kanga (vifaranga) wa kuanzia?
(3) Hivi Kanga sio maliasili ya Taifa? nikimaanisha sitasumbuliwa na Afisa wanyama pori pindi wakigundua nafuga Kanga?

Ni hayo tu kwa leo na asanteni

 
Mkuu bluetooth hakika umenisoma, Kumradhi ni Kware wanaJF

Asante bluetooth

Kawaone JB farms pale kwa Mathias Kibaha, au nenda pale Ubungo mataa karibu na YENU BAR wana ofisi pale. Kingine ni kwamba, wewe fuga kware, hao maliasili mpaka waje utakuwa umeshapata ujuzi tosha wa kufuga, naamini wakikufikia, mtaelewana. Vibali utapata mwaka 2019, upoooo
 
Kuna kanga wa kufugwa na kanga pori mkuu, so usiogope ni vitu viwili tofauti
 
Nimekua mpenzi wa ufugaji, hasa jamii ya ndege, nimeanza mwaka jana kufuga kanga nilinunua mayai na kutotolesha kupitia kuku, kiukweli nilifanikiwa na kutotolesha vizuri.

Msaada naomba kwamwenye uelewa kuhusu mayai ya kanga huchukua muda gani kutotolewa/kuanguliwa kupitia kuku? na ili kutotolesha mayai ya kanga na kuku kwa pamoja unafanyeje? Msaada tafadhari.
 

Ndg yang KUHUSU kanga Mayai yake yanatotolewa baada ya siku 28, iwe kwenye mashine au kwa kuku. Mayai ya kuku huchukua siku 21. Hii Ina maana unaweka mayai ya kanga kwa siku saba Kisha siku ya nane unaweka ya kuku ili yaje yatotolewe pamoja.
swaw?
 
Ndg yang KUHUSU kanga Mayai yake yanatotolewa baada ya siku 28, iwe kwenye mashine au kwa kuku. Mayai ya kuku huchukua siku 21. Hii Ina maana unaweka mayai ya kanga kwa siku saba Kisha siku ya nane unaweka ya kuku ili yaje yatotolewe pamoja.swaw?
hapa ndo huwa napenda yaani kama hujuikitu we uliza kisha utapata majibu yanayo stahili bila taabu na kuwaelewesha wengine maana hatamimi nilikuwa naitaji sana nshu hii
 
Ndg yang KUHUSU kanga Mayai yake yanatotolewa baada ya siku 28, iwe kwenye mashine au kwa kuku. Mayai ya kuku huchukua siku 21. Hii Ina maana unaweka mayai ya kanga kwa siku saba Kisha siku ya nane unaweka ya kuku ili yaje yatotolewe pamoja.
swaw?

Nimekusoma ndugu nashukuru sana heri na amani juuyako
 
hapa ndo huwa napenda yaani kama hujuikitu we uliza kisha utapata majibu yanayo stahili bila taabu na kuwaelewesha wengine maana hatamimi nilikuwa naitaji sana nshu hii

Umeona unatatizo ingia hm toa/uliza irimladi usitukane wala kumlenga mtu vibaya karibu nawe
 
Usisahau kuwapa chanjo ya Newcastle siku ya 7 na gumboro siku ya 14 na hakikisha siku ya 19 hadi 23 unawapa dawa ya mafua, wawe na mafua au hawana mafua (kipindi hiki kanga hushambuliwa sana na mafua), wakifika siku ya 25 salama basi umekula bingo.

Nashukur kwa taarifayako samahani, hebu nipena elim nzuri upande wa kuku dawaipi nzuri ? pia nikuulize kaswari kimasihara, hivi kanga unawatofautishaje huyu dume au jike?
 
Kwa mjini hasa dar kang mkubwa ananzia ela ngap coz huk kwet kanga mkubwa kabisa ni tsh 6,000-7,000
mtena kanga dar ni elfu 35 mpaka 40. Hii ni bei ya sehemu moja makumbusho karibu na millenium tower. Ilikua inapigwa bendi zamani. Mimi nilinunua kanga mdogo wa wiki 4 elfu 15 kwa kubembeleza sana. Kwenu wewe wapi?
 
mtena kanga dar ni elfu 35 mpaka 40. Hii ni bei ya sehemu moja makumbusho karibu na millenium tower. Ilikua inapigwa bendi zamani. Mimi nilinunua kanga mdogo wa wiki 4 elfu 15 kwa kubembeleza sana. Kwenu wewe wapi?
Ee wewe kumbe ndoivyo da jamani kumbe tujitume vijana fulsa tunazo
 
Usisahau kuwapa chanjo ya Newcastle siku ya 7 na gumboro siku ya 14 na hakikisha siku ya 19 hadi 23 unawapa dawa ya mafua, wawe na mafua au hawana mafua (kipindi hiki kanga hushambuliwa sana na mafua), wakifika siku ya 25 salama basi umekula bingo.
Naanza kufuga kwa kupitia wafugaji wa jf naona humu naweza pata japo fikra ya kunirejesha nam ktk ulimwengu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…