(UFOS) na Aliens wa Zimbabwe! nini hasa Kilitokea?

(UFOS) na Aliens wa Zimbabwe! nini hasa Kilitokea?

mareeTZ

Senior Member
Joined
Jun 4, 2015
Posts
171
Reaction score
181
Kumekuwa na hadithi nyingi sana katika ulimwengu huu tunaoishi kuwa hatupo tu binadamu na wanyama pekee yetu bali pia kuna viumbe wengine wanaishi walio kama sisi maumbo mithili ya kwetu, akili kama sisi pengine kutuzidi sisi. Wengi hudai viumbe hawa wanaishi katika sayari nyingine tofauti na dunia yetu na mara kwa mara wamedaiwa kutembelea maeneo kadhaa duniani. Viumbe hawa wanatambulika kama aliens na yako mamia ya shuhuda ziliripoti na watu mbalimbali waliodai kuwaona viumbe wakiwa na chombo cha duara kinachoruka kama ndege na hukitumia katika safari zao za kutembelea duniani vyombo hivi pamoja na aliens hawa hujulikana kama (UFOS) kirefu chake ni (Unidentified flying object) maana yake ni viumbe wasioeleweka warukao pande mbalimbali za dunia yetu. Je ni kweli viumbe hawa wapo? Je Ni kweli wameonekana hapa duniani? Kuna wanaopinga na kudai ni ndege za kijeshi zinazofanya mipango ya siri na hivyo watu hudhani ni UFOs.

Moja kati ya shahidi zinazoonyesha kwamba UFOs siyo ndege au vyombo vya kawaida vitumiwavyo na wanadamu wa kawaida ni uwepo wa matukio haya ya UFOS yaliyoanza kuripotiwa zamani sana kipindi ambacho hata binadamu hajagundua ndege au chombo chochote cha moto. Tukio la kwanza kabisa kuwahi kuripotiwa ni la gavan wa koloni la Massachusetts bwana john winthrope mnamo mwaka 1639 aliyeandika kwenye kitabu chake cha kumbukumbu kuhusu tukio la msaidizi wake james evereel aliyeona chombo kikubwa chenye kutoa mwanga mkali kikipaa na kutua pembezoni mwa mto muddy kwa muda wa masaa matatu. Pia julai 1884 iliripotiwa kuonekana kwa chombo cha umbo la duara kilichozungukwa na pete kama sayari ya Saturn huko mjini norwood new York.

Katika matukio ya kushangaza kabisa ya karne hii yaliyoacha maswali mengi ulimwenguni kote ni pamoja na tukio la wanafunzi waliodai kuwaona viumbe hawa nchini Zimbabwe.

Mnamo asubuhi moja ya septemba 16 mwaka 1994 walimu na wafanyakazi wa shule ya ariel walishikwa na mshangao baada ya baadhi ya wanafunzi kuanzia miaka 7 na 12 kudai kuna ndege ya ajabu ilitua katika viwanja vya shule hiyo. Muda huo walimu walikuwa kwenye kikao hivyo wanafunzi walikuwa nje bila uangalizi wowote wakati tukio hilo linatokea, siku mbili kabla ya tukio hilo huko mjini Harare kilomita 20 kutoka mji wa ruwa kuliripotiwa kuonekana vitu vinavyopaa angani visivyoelewka.

Watoto hao walidai kwamba mwanzo waliona vitu tofauti vitatu vinazunguka angani baada na ya muda vinapotea na kutokezea tena eneo lingine halafu vyombo hivyo vikaanza kusogea kuelekea chini mwishowe vikatua katika vichaka pembezoni mwa viwanja vya shule hiyo,

Wanafunzi hao wakadai waliona kiumbe mfupi mithili ya mwanadamu mwenye urefu kama mita moja kasimama juu ya chombo hicho. Ghafla yule kiumbe alianza kuwasogelea wale wanafunzi taratibu. Kimwonekano alikuwa ana shingo kama ya mtu mzee sana, macho makubwa meusi na nywele ndefu nyeusi. Ghafla wanafunzi wale walianza kupiga mayowe wakikimbia huku na kuo kuomba msaada wakijua labda ni mashetani waliyokuwa wakihadithiwa na mababu zao katika baadhi ya hadithi. Kelele zile zilimshtua kiumbe yule alipowaona wanafunzi wale na ghafla alipotea na kutokeza tena pembeni ya kile chombo ambacho kiliondoka ghafla na kupotelea angani.

Cynthia hind mchunguzi wa matukio ya UFO barani africa aliwasili shuleni hapo kesho yake asubuhi ambapo ali kutana na mkuu wa shule hiyo, wanafunzi Zaidi ya 65 waliapa na kuripoti vitu vinavyofanana kuhusu tukio hilo. waliambiwa wachore picha za kile walichokiona jana yake. Zilichorwa picha tofauti 35 zilizokuwa na mwonekanao wa aina moja. Mmoja wa watoto hao alisema viumbe hao walikuwa wakitoa ishara kuonesha kwamba binadamu tunaharibu dunia yetu kwa uchafuzi wa mazingira hivyo tuache kabla hakujawa na madhara makubwa
Michoro ile ililingana na mamia ya matukio ya watu waliokiri kuona viumbe wa ajabu duniani
upload_2016-11-14_16-15-23.png
upload_2016-11-14_16-15-33.png
upload_2016-11-14_16-15-46.png


Kitabu kimoja kinachoitwa the report on identified flying object cha mwaka 1955 kilichoandikwa na Ruppelts kimeelezea mamia ya matukio ya kuonekana kwa UFOS duniani kikiandika shahidi mbalimbali za kweli kutoka kwa marubani wa jeshi pamoja na wanasayansi mbalimbali ambao walitoa ushahidi kuhusu kuwaona viumbe hao wakiwa huko angani. Shahidi nyingi zimethibitishwa lakini mpaka sasa kisa cha zimbambwe kimeacha maswali kadhaa , je ni kweli tukio hilo lilitokea? Na lipi fundisho hasa kwetu sisi wanadamu?

 

Attachments

  • upload_2016-11-14_16-14-52.png
    upload_2016-11-14_16-14-52.png
    25 KB · Views: 336
  • upload_2016-11-14_16-16-34.png
    upload_2016-11-14_16-16-34.png
    15.4 KB · Views: 398
NI sawa lakini lazima uzimie, ukizimia unapoteza kumbukumbu zote mwanga mkali wa chombo chao unafuta memory card yako kwa muda huo tu kwa tukio lao tu lakini we ukiwaona uwahi kunywa maziwa fasta
uzushi mtupu kama kweli mbona wao waliwaona sasa memory ikaendelea kuwepo...!!uzushi wakidunia tu huu nakubaliana namambo mengi ya mzungu na tafiti zake ila hapa alikwama kunikamata
 
Kuna ukweli wowote kuhusu hawa viumbe ufozi kwamba wanaogopa sana camera na ndio maana dunia hii ya teknologia hawaja tokea tena.

Na washawasha?
 
Habari za uwepo wa Hao viumbe zimekuwepo kwa siku nyingi sana. Ila huwa ninakuwa na maswali mengi kuwahusu ambayo hayana majibu ya kuridhisha.

Kama ni viumbe toka sayari nyingine kweli, na wana uwezo huo wa kuja mpaka huku, ni nini haswa dhumuni la safari kama hizo? Haiwezekanai waje tu na kuondoka. Mf. katika hilo tukio la Zimbabwe wangeweza kuondoka na mtoto mmoja (labda) au kitu kingine chochote kwa ajili ya uchunguzi, hapo ingeonyesha wapo na wana malengo fulani kwa kuja kwao.

Kwa huo uwezo wao wa kuja mpaka huku na kurudi inaonyesha wana utaalam mkubwa kuliko sisi. Kama walianza kuonekena huku tangu enzi za giza 1639 ina maana wangekuwa wameendelea zaidi na wakija wangekuja kwa namna ya kimaendeleo na muonekano tofauti wa vyombo vyao na malengo tofauti pia. Mfano, wangeweza hata kutua kwenye Jangwa la Sahara na kufanya yao kwa siku wanazotaka kisha kuondoka. Sio kuja kwa kujificha na kukimbia kwa vyombo vile vile vya miaka ile.

Hao wa Zimbabwe Eti, watoto walipiga kelele wakakimbia..hao walikuwa vibwengo.
 
Kwani hawa ndo jamii ya 'JADU' na POPO BAWA au nimechanganya mafile?
 
Habari za uwepo wa Hao viumbe zimekuwepo kwa siku nyingi sana. Ila huwa ninakuwa na maswali mengi kuwahusu ambayo hayana majibu ya kuridhisha.

Kama ni viumbe toka sayari nyingine kweli, na wana uwezo huo wa kuja mpaka huku, ni nini haswa dhumuni la safari kama hizo? Haiwezekanai waje tu na kuondoka. Mf. katika hilo tukio la Zimbabwe wangeweza kuondoka na mtoto mmoja (labda) au kitu kingine chochote kwa ajili ya uchunguzi, hapo ingeonyesha wapo na wana malengo fulani kwa kuja kwao.

Kwa huo uwezo wao wa kuja mpaka huku na kurudi inaonyesha wana utaalam mkubwa kuliko sisi. Kama walianza kuonekena huku tangu enzi za giza 1639 ina maana wangekuwa wameendelea zaidi na wakija wangekuja kwa namna ya kimaendeleo na muonekano tofauti wa vyombo vyao na malengo tofauti pia. Mfano, wangeweza hata kutua kwenye Jangwa la Sahara na kufanya yao kwa siku wanazotaka kisha kuondoka. Sio kuja kwa kujificha na kukimbia kwa vyombo vile vile vya miaka ile.

Hao wa Zimbabwe Eti, watoto walipiga kelele wakakimbia..hao walikuwa vibwengo.
Mkuu kama inavyo semekana walikuwa na uwezo wa kupotea itajuaje kama walichukua sample ya baadhi ya vitu bila kuonekana..
Na huenda wamesha kuwa na teknolojia kubwa zaidi kiasi kwamba vyombo vyetu haviwezi kuwaona tena
Hata kwa macho ya kawaida hatuweze kuwaona
 
Kumekuwa na hadithi nyingi sana katika ulimwengu huu tunaoishi kuwa hatupo tu binadamu na wanyama pekee yetu bali pia kuna viumbe wengine wanaishi walio kama sisi maumbo mithili ya kwetu, akili kama sisi pengine kutuzidi sisi. Wengi hudai viumbe hawa wanaishi katika sayari nyingine tofauti na dunia yetu na mara kwa mara wamedaiwa kutembelea maeneo kadhaa duniani. Viumbe hawa wanatambulika kama aliens na yako mamia ya shuhuda ziliripoti na watu mbalimbali waliodai kuwaona viumbe wakiwa na chombo cha duara kinachoruka kama ndege na hukitumia katika safari zao za kutembelea duniani vyombo hivi pamoja na aliens hawa hujulikana kama (UFOS) kirefu chake ni (Unidentified flying object) maana yake ni viumbe wasioeleweka warukao pande mbalimbali za dunia yetu. Je ni kweli viumbe hawa wapo? Je Ni kweli wameonekana hapa duniani? Kuna wanaopinga na kudai ni ndege za kijeshi zinazofanya mipango ya siri na hivyo watu hudhani ni UFOs.

Moja kati ya shahidi zinazoonyesha kwamba UFOs siyo ndege au vyombo vya kawaida vitumiwavyo na wanadamu wa kawaida ni uwepo wa matukio haya ya UFOS yaliyoanza kuripotiwa zamani sana kipindi ambacho hata binadamu hajagundua ndege au chombo chochote cha moto. Tukio la kwanza kabisa kuwahi kuripotiwa ni la gavan wa koloni la Massachusetts bwana john winthrope mnamo mwaka 1639 aliyeandika kwenye kitabu chake cha kumbukumbu kuhusu tukio la msaidizi wake james evereel aliyeona chombo kikubwa chenye kutoa mwanga mkali kikipaa na kutua pembezoni mwa mto muddy kwa muda wa masaa matatu. Pia julai 1884 iliripotiwa kuonekana kwa chombo cha umbo la duara kilichozungukwa na pete kama sayari ya Saturn huko mjini norwood new York.

Katika matukio ya kushangaza kabisa ya karne hii yaliyoacha maswali mengi ulimwenguni kote ni pamoja na tukio la wanafunzi waliodai kuwaona viumbe hawa nchini Zimbabwe.

Mnamo asubuhi moja ya septemba 16 mwaka 1994 walimu na wafanyakazi wa shule ya ariel walishikwa na mshangao baada ya baadhi ya wanafunzi kuanzia miaka 7 na 12 kudai kuna ndege ya ajabu ilitua katika viwanja vya shule hiyo. Muda huo walimu walikuwa kwenye kikao hivyo wanafunzi walikuwa nje bila uangalizi wowote wakati tukio hilo linatokea, siku mbili kabla ya tukio hilo huko mjini Harare kilomita 20 kutoka mji wa ruwa kuliripotiwa kuonekana vitu vinavyopaa angani visivyoelewka.

Watoto hao walidai kwamba mwanzo waliona vitu tofauti vitatu vinazunguka angani baada na ya muda vinapotea na kutokezea tena eneo lingine halafu vyombo hivyo vikaanza kusogea kuelekea chini mwishowe vikatua katika vichaka pembezoni mwa viwanja vya shule hiyo,

Wanafunzi hao wakadai waliona kiumbe mfupi mithili ya mwanadamu mwenye urefu kama mita moja kasimama juu ya chombo hicho. Ghafla yule kiumbe alianza kuwasogelea wale wanafunzi taratibu. Kimwonekano alikuwa ana shingo kama ya mtu mzee sana, macho makubwa meusi na nywele ndefu nyeusi. Ghafla wanafunzi wale walianza kupiga mayowe wakikimbia huku na kuo kuomba msaada wakijua labda ni mashetani waliyokuwa wakihadithiwa na mababu zao katika baadhi ya hadithi. Kelele zile zilimshtua kiumbe yule alipowaona wanafunzi wale na ghafla alipotea na kutokeza tena pembeni ya kile chombo ambacho kiliondoka ghafla na kupotelea angani.

Cynthia hind mchunguzi wa matukio ya UFO barani africa aliwasili shuleni hapo kesho yake asubuhi ambapo ali kutana na mkuu wa shule hiyo, wanafunzi Zaidi ya 65 waliapa na kuripoti vitu vinavyofanana kuhusu tukio hilo. waliambiwa wachore picha za kile walichokiona jana yake. Zilichorwa picha tofauti 35 zilizokuwa na mwonekanao wa aina moja. Mmoja wa watoto hao alisema viumbe hao walikuwa wakitoa ishara kuonesha kwamba binadamu tunaharibu dunia yetu kwa uchafuzi wa mazingira hivyo tuache kabla hakujawa na madhara makubwa
Michoro ile ililingana na mamia ya matukio ya watu waliokiri kuona viumbe wa ajabu duniani
View attachment 434108View attachment 434109View attachment 434110

Kitabu kimoja kinachoitwa the report on identified flying object cha mwaka 1955 kilichoandikwa na Ruppelts kimeelezea mamia ya matukio ya kuonekana kwa UFOS duniani kikiandika shahidi mbalimbali za kweli kutoka kwa marubani wa jeshi pamoja na wanasayansi mbalimbali ambao walitoa ushahidi kuhusu kuwaona viumbe hao wakiwa huko angani. Shahidi nyingi zimethibitishwa lakini mpaka sasa kisa cha zimbambwe kimeacha maswali kadhaa , je ni kweli tukio hilo lilitokea? Na lipi fundisho hasa kwetu sisi wanadamu?


Aliens real exist...and there is the reason why we are in the dark about them, kwasababu ukweli ukijulikana sasa kila msingi ya imani na dini zitaharibika...Muumba wa vyote yupo lakini sio kwa jinsi inavyofundishwa, we have been mislead by secrecy....mfano wa aliens

RAK alitembelea middle east ndo walitengeneza imani ya jinn (genies) in islamic methology na ndo aliens race ambayo imetembelea dunia mara chache "and they stopped visit earth because their immune system could not cope with earth's fauna and flora and now they exist in dimension beyond the existing dimension of our universe they last record visit 712AD.

Alien wengine wanaitwa The pleyadiyans wanausika sana katika ukuaji wa kiroho...(spiritual growth) they regularly visiting earth and they have remain most silence since 10,000BC their ship are known has beamship...they are the oldest race

Alpha draconians:- hawa wanataka kutawala dunia kwa madai kwamba wao wanaumri sana kuliko sisi kwahiyo dunia ni mali yao "They are apparently a major part of a planned 'invasion' which is eventually turning from covert infiltration mode to overt invasion mode as the "window of opportunity" (the time span before International human society becomes an interplanetary and interstellar power) slowly begins to close.

They are attempting to keep the "window" open by suppressing advanced technology from the masses, which would lead to eventual Terran colonization of other planets by Earth and an eventual solution to the population, pollution, food and other environmental problems.

Being that Terrans have an inbred "warrior" instinct the Draconians DO NOT want them/us to attain interstellar capabilities and therefore become a threat to their imperialistic agendas"

Negumak (aka. Gnomopo) hawa alien ndo wameinspire filamu ya Hollywood independent day wametembelea dunia kwa mara ya kwanza 1989 na wanateka binadamu na kufanya majaribio ya mind control na ni moja ya kati alien race ambayo serikali kubwa inaziogopa considering the future human

Hii ni baadhi tu but ukitafuta KGB alien race leakage note book unajua zaidi...and you be the judge if it real or not
 
Back
Top Bottom