Watu wengi wataishangaa kauli yangu, watakaa midomo wazi na kujiuliza maswali kibao moja ya maswali watakayojiuliza ni kama yafuatayo.
Anasema EL ni msafi wakati alithubutu kumuita Fisadi?
Usafi wake uko wapi au kwa kuwa kahamia Chadema?
Huyu anayesema haya ni mamluki au Chadema kweli?
Hayo ni baadhi tu ya maswali japo najua kuna maswali mengine mengi zaidi juu ya mh EL.
Wanapoendelea kujiuliza ni vyema na mm niwaulize maswali kadhaa kama ifuatavyo?
Kama EL ni mwizi au fisadi ni kwanini hadi leo hajakamatwa na kupelekwa Mahakamani?
Je hajakamatwa kwakuwa serikali ni dhaifu au haijui sheria inazosimamia yenyewe au iliogopa kuumbuliwa zaidi?
Toka 2008 hadi leo nini kimefanyika baada ya EL kwa kulinda heshima yake na kuamua kujiweka pembeni?
Tunadhani ni kwanini jina lake liliishia njiani? papo hapo jiulize kwanini Rizone alitweete akionesha hayupo tayari kuona Rais akitokea kaskazini kipindi cha Uhai wake?
Je ni kwanini Rais JK hajawahi kuthubutu kumsema EL hadharani?
Je ni kwanini Upinzani walimpiga sana mitandaoni na hata majukwaani lakini leo wapo meza moja?
Ni kwanini CCM walimuamini tena 2010 akapeperusha Bendera yao jimbo la Monduli? utamuaminije Mwizi?
Je ni nchi gani upinzani ilishawahi kuing'oa serikali bila kutumia watu waliokuwepo au waliopo Madarakani?
Je tunapenda kuendelea kuwa masikin kwa mfumo uliopo?
Bado nina maswali ambayo sitayamaliza sasa hivi ila endelea na ww kujihoji na kujipa majibu huku ukiangazia mfumo mzima wa chama cha mapinduzi na serikali yake ndipo utapata majibu.
Narudia kusema "EL si Mchafu hata kidogo" lakini katika yote Mfumo wa CCM ndio mchafu na ndio unaowafanya wachafuke hata wasio wachafu, yawezekana kabisa msielewe dhana yangu lakini pia mkanielewa dhana yangu.
Mimi kama mwanachama wa chadema sipo tayari kuendelea kuitwa mpinzani lakini nipo tayari kuona nchi hii ikiwa upinzani kwa masilahi mapana ya watz wote.
Nitaeleza kwa kina nikitulia sehemu yenye upepo mwanana
Kwa mara ya kwanza naomba nipishane na wewekidogo.
Maswali yako yako valid yote. Kutokuchukuliwa hatua kwa fisadi Lowasa na mafisadi wa EPA, Escrow na wengine, ni kwa sababu ya ushetani wa ccm na mifumo yake ambayo kwa mantiki hiyo, imeua taifa.
Lowasa kama wanaccm wengine si msafi hata kidogo. Ni sawa na mafirauni wengine waliotuibia na kisha kula yamini ya kuficha ukweli na kuendelea kulindana na kutuhadaa Watanzania. Hii ndiyo inayoonekana kwa JK kumnadi tena 2010 huku wakiendeleza uaharamia hadi kwenye bunge la katiba, escrow n.k.
Kinachoweza kueleweka kwa watu wenye akili siyo propaganda za kusema EL ni mtu safi sana wakati ananuka Rushwa, Wizi na Ufisadi. Na hadi sasa hajawahi kuzungumzia kwa uwazi na ukweli suala la wizi wa Richmond, na wala hajawahi kujibainisha kinyume na mitazamo ya ufisadi dhuruma na maonevu yanayofanywa na ccm dhidi ya wananchi. Anachosema yeye ni kuwakomboa watanzania, kuondoa umaskini ambao ameshindwa kuuondoa Monduli bila kugusa rushwa, ufisadi, udanganyifu, uvnjaji wa haki za binadamu na udharimu wanaofanyiwa Watanzanai ndani ya nchi yao na ccm ambavyo ndivyo visima na chemichemi za machozi na vilio vya watanzania.
Usafi wa Lowasa hauji kwa sababu ya ccm kutokumchuklia hatua. Hii inamaanisha mafirauni wote wa ccm ambao hawajachukuliana hatua ni wasafi na kupoteza maana ya vita yetu dhidi ya ccm.
Ilo lowasa awe msafi, kama vile tunategemea Watanzania mafirauni wote kubadilika na kuwa wasafi katika uongozi wa lowasa, wanahitajika kuwa wakweli na Tanzania na si ulaghai lazimishi.
Tunahitaji warudishe mali zetu walizohujumu, waweke wazi mitandao yao ya uchafu na wizi kama richmond kwa Lowasa ili tuichambue na kuifumua kama vile kuchoma uchawi wanasemaga, na kukata kata mirija yake yote ili tuwe na mfumo safi mpya usiofungamana na ufirauni huu.
Mimi ninaimani katika ujenzi wa taifa wa pamoja lakini upamoja usiwe kudanganyana na kuficha maovu. Maovu yawekwe wazi na yatafutiwe tiba sahihi ya pamoja na kwa pamoja tujenge kinga ya kulilinda taifa dhidi ya umumiani ule, huku tukishirikisha taifa zima katika ujenzi wa taifa jipya.
Kwa ufupi, ninaunga mkono ukaribisho wa Lowasa Chadema, ikiwa ni pamoja na watanzania wote wachafu na wasafi ili tuwe pamoja katika ujenzi wa taifa. Lakini ninaktaa propaganda za kusema Lowasa ni msafi bila kutuonyesha wala kutuambia amejisafishaje dhidi ya mali alizotuibia za richmond, rushwa, na mtizamo wake dhidi ya udanganyifu, ughushaji, na uvunjaji wa haki za watanzania ambako ameshiriki kwa 100 akiwa kiongozi ndani ya ccm na serikali yake.
HUKO KUTAKUWA KUENDELEA KUTUHADAAA WATANZANIA KITU AMBACHO KITADHOOFISHA IMANI YA WATANZANIA KWA CHADEMA UKIZINGATIA KUNA WATU MASHUJAA KAMA MWANGOSI, WAHANGA WA SOWETO, DR. MVUNGI N.K N.K , WAMEMWAGA DAMU ZAO WAKIPIGANIA UKOMBOZI WA TAIFA, DHIDI YA UFIRAUNI WA CCM AMBAYO SASA KWA MTAZAMO WAKO HUU NI KAMA UNAANZA KUUBARIKI.