WanaJF,
Ufisadi mkubwa umebainika kufanywa na viongozi wa CHADEMA na kupelekea upotevu wa mamilioni ya pesa za chama ambazo kimsingi ni kodi za wananchi.
Ufisadi huo unahusisha website/tovuti ya chama ambayo inalipiwa kila mwezi kiasi cha Tshs. 4 millioni kwa ajili ya uendeshaji na takribani Tshs. 15 millioni kwa ajili ya ukarabati wa tovuti hiyo hali ya kuwa HAKUNA kitu kinachoitwa tovuti ya CHADEMA.
Ukweli wa mambo ni kwamba vigogo wa CHADEMA walifunga tovuti hiyo miaka karibu 7 iliyopita na kulaghai wanachama wake kuwa tovuti hiyo inahitaji matengenezo makubwa hivyo haitakuwa hewani.
Jambo la kushangaza ni pale ambapo pesa za kutosha zinatumika kulipa uendeshaji wa tovuti pamoja na matengenezo yasiyoisha na kufanya chama kipoteze kiasi takribani cha Tshs. 20 millioni.
Aidha, pamoja na kwamba juhudi kubwa zilitumika kumtafuta Dr Slaa kama mtendaji mkuu wa chama ili atolee suala hili ufafanuzi, simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa na hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi (SMS) hakujisumbua kujibu.
Kimya hicho cha Dr Slaa kimezidi kuaminisha kuwa yeye ndiye muhusika mkubwa wa ufisadi huo. Dr Slaa, uzalendo wako upo wapi!?
Ufisadi mkubwa umebainika kufanywa na viongozi wa CHADEMA na kupelekea upotevu wa mamilioni ya pesa za chama ambazo kimsingi ni kodi za wananchi.
Ufisadi huo unahusisha website/tovuti ya chama ambayo inalipiwa kila mwezi kiasi cha Tshs. 4 millioni kwa ajili ya uendeshaji na takribani Tshs. 15 millioni kwa ajili ya ukarabati wa tovuti hiyo hali ya kuwa HAKUNA kitu kinachoitwa tovuti ya CHADEMA.
Ukweli wa mambo ni kwamba vigogo wa CHADEMA walifunga tovuti hiyo miaka karibu 7 iliyopita na kulaghai wanachama wake kuwa tovuti hiyo inahitaji matengenezo makubwa hivyo haitakuwa hewani.
Jambo la kushangaza ni pale ambapo pesa za kutosha zinatumika kulipa uendeshaji wa tovuti pamoja na matengenezo yasiyoisha na kufanya chama kipoteze kiasi takribani cha Tshs. 20 millioni.
Aidha, pamoja na kwamba juhudi kubwa zilitumika kumtafuta Dr Slaa kama mtendaji mkuu wa chama ili atolee suala hili ufafanuzi, simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa na hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi (SMS) hakujisumbua kujibu.
Kimya hicho cha Dr Slaa kimezidi kuaminisha kuwa yeye ndiye muhusika mkubwa wa ufisadi huo. Dr Slaa, uzalendo wako upo wapi!?