Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Mchungaji Gwajima amesimama na anaanza ufafanuzi
Update:
Anasema yeye anafafanua kwa habari ya washirika wake ambao wamesikia taarifa husika. Kwanza amen za na kuwauliza washirika wake ni nani amesikia taarifa hizo na kwa ujumla umati wa maelfu ya waumini wameitikia
UPDATE
Kwamba kwenye siku ya ibaada majira ya tarehe Tajwa huu mwananchi mmoja alizuka kanisani, na akakutana na walinzi wa kanisa. Na wakamhoji shida yake nini, na kwa kuwa alikuwa na Shari kubwa aliwaambia lengo lake ni kumwona mchungaji kiongozi
UPDATE
mtu huyo aling'ang'ania kwa Shari kumwona mchungaji kiongozi na kwa utaratibu si rahisi kumwona yeye pasipo kujua sababu.. Kwa hasira akaanza kuropoka kwamba yeye ni mafia na kwamba yeye ndiye aliyemteka Ulimboka
UPDATE
BAADA YA hapo walinzi si hao wakajua si mtu mwema, Wakampeleka polisi..
UPDATE
Baada ya hapo walinzi hao wakapigiwa cm polisi kwa ushahidi zaidi, na walipofika huko wakamtambua huyo kijana, na kweli huyo kijana mbele Yao akakiri kwamba alifika hapo kanisani.. Na pia kwamba aliropoka maneno yote mbele Yao . Na akakiri mbele Yao kwamba yeye huwa Ana roho inamuingia na kuwa Kama mwendawazimu na kuanza kuropoka maneno ambayo hata yeye hajui yanapotokea.. Hivyo walinzi pamoja na Polisi walikubaliana kwamba mtu huyo ni Kama mwendawazimu na ni Velma mambo hayo wakayapuuza na Kila mtu aende lee na shughuli zake.. Walinzi hao wakarudi kanisani na kuripoti taarifa za mtu huyo kwamba kuna mtu walimkamata na kumfikisha kituoni na baada ya hayo walipigiwa simu wakatoe ushahidi.. Na matoke yake yote..
Siku ya tatu ndipo
UPDATE
NIMEPATA AUDIO CLIP YAKE NADHANI NIFANYA KUIUPLOAD HUMU
Mbona hueleweki unachotaka kutuambia? au na wewe ni mwendawazimu?