Ufafanuzi wa Balaza la Elimu kuhusu Ufaulu wa E na F

gashambala uwezo

JF-Expert Member
Jan 17, 2014
485
67
wana Jf mimi binafsi nilijua mwenye ufaulu E na kanafuu kidogo kuliko aliyepata F

na kama ni hivyo ni kwanini watumie madaraja mawili.


UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI U YA WADAU WA ELIMU KUHUSMATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013
Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013 tarehe 21/02/2014. Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Baraza limekuwa likipokea maswali mbalimbali yanayoashiria kuwa baadhi ya wadau wa elimu hawakuelewa vizuri kuhusu Viwango vya Ufaulu (grade ranges), alama ya chini ya ufaulu (pass mark) na Ufaulu wa jumla wa mtahiniwa (overall performance). Baraza la Mitihani linapenda kutoa ufafanuzi katika mambo hayo kama ifuatavyo

:
1. Viwango vya ufaulu (grade ranges) ni makundi ya alama yanayopangwa ili kuwaweka pamoja watahiniwa wenye uwezo unaofanana katika somo husika na kuwatofautisha na watahiniwa waliopo katika kundi jingine. Makundi haya hupangwa ili kuwawezesha wadau kutambua namna watahiniwa walivyotawanyika katika viwango mbalimbali vya umahiri wa somo husika. Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likitumia makundi Matano (5) kwa kipindi kirefu hadi mwaka 2012. Aidha, Kuanzia Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013, Baraza limeanza kutumia utaratibu wa Makundi Saba (7) ambayo ni A, B+, B, C, D, E na F. Utaratibu huu umelenga kupunguza mlundikano mkubwa wa alama katika kundi moja. Mgawanyo wa makundi hayo ni kama inavyoonekana kwenye Jedwali la 1. Jedwali Na 1: Viwango vya ufaulu vilivyotumika katika Matokeo ya CSEE 2013.
Kundi
Gredi
Alama
Idadi ya Pointi
1
A
75 - 100
1
2
B+
60 - 74
2
3
B
50 - 59
3
4
C
40 - 49
4
5
D
30 - 39
5
6
E
20 - 29
6
7
F
0 - 19
7
. 2. Kwa kuzingatia viwango vya ufaulu vilivyoainishwa katika makundi saba yaliyopo kwenye Jedwali na 1, kiwango cha chini cha ufaulu ni gredi D na kiwango cha juu cha ufaulu ni Gredi A. Mtahiniwa atakuwa amefaulu somo husika iwapo atapata gredi D na kuendelea. Aidha, mtahiniwa aliyepata gredi E na F atakuwa hajafaulu somo husika.

baraza la mtihani la Tanzania linapenda kutoa taarifa kwamba, ufafanuzi wa sifa za kujiunga na mafunzo katika ngazi mbalimbali kwa kutumia mfumo huu mpaya wa madaraja,

utatolewa na mamlaka husika, ambaye ni KAMISHINA WA ELIMU.
 
  • Thanks
Reactions: ERO
Sasa tuseme ukitaka kuboresha elimu ni kupanua wigo wa alama za ufaulu ama kubana viwango vya ufaulu na kuboresha sera zenye tija kwa mlengwa yaani mwanafunzi na taifa, ninapata mashaka kuona uamuzi wa baraza la mitihani kama lina nia ya dhati juu ya uboreshaji wa sekta ya elimu, lakini ningewaomba wadau wa jf kama hili wazo ama dhana ya kupanua wigo wa madaraja una tija kwa wadau husika.
 
Hapa walikuwa na lengo la kufikisha 60% waliyoji-commit kwenye BRN. Ufafanuzi wao hauna mantiki hata kidogo kwa sababu utawekaje alama mbili E na F zenye maana moja? kwa nini isiwe alama moja tu kama zote ni kufeli? Sasa hapo una makundi saba ya ufaulu au ni sita tu? Inanichanganya naomba wenye ujuzi zaidi na masuala haya wasaidie
Sasa tuseme ukitaka kuboresha elimu ni kupanua wigo wa alama za ufaulu ama kubana viwango vya ufaulu na kuboresha sera zenye tija kwa mlengwa yaani mwanafunzi na taifa, ninapata mashaka kuona uamuzi wa baraza la mitihani kama lina nia ya dhati juu ya uboreshaji wa sekta ya elimu, lakini ningewaomba wadau wa jf kama hili wazo ama dhana ya kupanua wigo wa madaraja una tija kwa wadau husika.
 
Sijui ni vigezo gani vinavyotumika kuwapata viongozi wa elimu. Japo amesoma sana lakini wako kwenye mlengo wa kuingamiza elimu yetu zaidi badala ya kuweka mazingira ya wanafunzi kufanya vizuri




mimi nausubir huo ufafanuzi wa hao wadogo zetu kuhusu kujiunga kwenye ngaz mbalimbali za kielim maana sijui watu gan wanaenda kuzalishwa
 
Xio xili necta wana akili za panz yaan m2 mwenye 29 n xawa na M2 mwenye 0???hawana haya kwel NECTA.
 
NCHI hiii tumesha hiharibu kitambo kila kitu kinaamuliwa na wanasiasa
 
NCHI hiii tumesha hiharibu kitambo kila kitu kinaamuliwa na wanasiasa

na hiyo unayocema n dhahiri kuwa n ukwel coz viongoz wanataka kusafisha majina yao kwa kutuwekea grade zao za ajabuajabu ili wachaguliwe 2015!
 
ndugu yangu matokeo haya ni mabaya sana,ukizingatia shule nyingi za umma zinazidi kupolomoka uwezi amini shule kama mzumbe inakuwa ya 40 kati ya shule 3256,hapo zinazo ongoza ni shule za watu binafsi na waziri anachekelea kuwa viwango vya ufaulu vimeongezeka,
mzee wa matamko NAPE kimya maana na yeye ni zao la daraja la nne
hawa ndio CCM
 
Hali ya elimu ni tete sana sijui watanzania tumerogwa na nani kila kukicha tunafanya maamuzi ya ajabu ajabu
ndugu yangu matokeo haya ni mabaya sana,ukizingatia shule nyingi za umma zinazidi kupolomoka uwezi amini shule kama mzumbe inakuwa ya 40 kati ya shule 3256,hapo zinazo ongoza ni shule za watu binafsi na waziri anachekelea kuwa viwango vya ufaulu vimeongezeka,
mzee wa matamko NAPE kimya maana na yeye ni zao la daraja la nne
hawa ndio CCM
 
nmewaza sana kaka, b'se E inaanzia 20-29 na F inaanzia 0-19.Xaxa itakuaje m2 mwenye 25 alinganishwe na m2 alyepata 6???.
 
Back
Top Bottom