Ufafanuzi Kuhusu Upepo Wa Kisulisuli

Ufafanuzi Kuhusu Upepo Wa Kisulisuli

Nashukuru ,,ila bado sijaelewa huo upepo ndo wa namna gani!!!!
... upepo wa kisulisuli ni upepo uvumao kwa ghafla, nguvu na kasi ukitimua vumbi na kutengeneza mfano wa silinda (cylinder) refu kwenda juu (hadi mita 50 au zaidi). Mara nyingi huvuma majira ya kiangazi kuelekea majira ya mvua. Kwa kawaida, huvuma sehemu za wazi zenye miti michache na vumbi hususan mashambani.

Makabila mengi Tanzania wana mitazamo tofauti tofauti upepo huu unapoonekana. Kwanza, ni ishara kwamba majira ya mvua yamekaribia. Pili, kiimani utasikia "shetani" kapita, n.k. Kiingenreza hujulikana kama "whirlwind". Rejea picha; unaweza kuona uhusiano kati ya huo upepo na andiko hili: "Ikawa, hapo BWANA alipopenda kumpandisha Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya alitoka Gilgali pamoja na Elisha."; 2 FAL 2:1

Whirlwind_2250.jpg
 
Lwakatare 13:10 upepo ukawafanya binti za Mlima wa Moto kupata wenza.
 
Kwa hyo wadada😑 wanaenda kupokea upako wa kisulisuli
 
... upepo wa kisulisuli ni upepo uvumao kwa ghafla, nguvu na kasi ukitimua vumbi na kutengeneza mfano wa silinda (cylinder) refu kwenda juu (hadi mita 50 au zaidi). Mara nyingi huvuma majira ya kiangazi kuelekea majira ya mvua. Kwa kawaida, huvuma sehemu za wazi zenye miti michache na vumbi hususan mashambani.

Makabila mengi Tanzania wana mitazamo tofauti tofauti upepo huu unapoonekana. Kwanza, ni ishara kwamba majira ya mvua yamekaribia. Pili, kiimani utasikia "shetani" kapita, n.k. Kiingenreza hujulikana kama "whirlwind". Rejea picha; unaweza kuona uhusiano kati ya huo upepo na andiko hili: "Ikawa, hapo BWANA alipopenda kumpandisha Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya alitoka Gilgali pamoja na Elisha."; 2 FAL 2:1

View attachment 1234890
Hicho ni kimbunga
 
Hicho ni kimbunga
... kimbunga a.k.a hurricane kwa kawaida huanzia baharini na husababisha/huambatana na mvua kali kuliko viwango vya kawaida. Upepo wa kisulisuli haunaga mvua; hutokea majira ya ukame ni wa ghafla na wa muda mfupi kama nilivyoelezea awali. Ni kweli, wengi wetu huutambulisha upepo wa kisulisuli kama kimbunga ila tofauti ipo.
 
Umeeleza saafi. Shida yangu ni hii, kwanini uanze Sentesi na Herufi ndogo?
Mkuu unapokosoa uandishi wa mtu,angalia na wa kwako kabla hujapost.
Hapo kwenye ulichoandika,kwa "nini uanze Sentensi"neno sentensi hukutakiwa kuanza na herufi kubwa,na pia neno herufi hukutakiwa kuanza na herufi kubwa.
 
Hivi na hili nalo linahitaji wamisionari toka ulaya na Asia waje kutufundisha kuwa hii siyo maana ya dini walotuletea,
Huu ni utumwa mpya
 
Mkuu unapokosoa uandishi wa mtu,angalia na wa kwako kabla hujapost.
Hapo kwenye ulichoandika,kwa "nini uanze Sentensi"neno sentensi hukutakiwa kuanza na herufi kubwa,na pia neno herufi hukutakiwa kuanza na herufi kubwa.
Aisee uandishi ni mziki.

Asante kwa mwongozo mkuu.
 
Back
Top Bottom