Ufafanuzi kuhusu RAZABA

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,527
Reaction score
830,087
Maaana halisi ya neno RAZABA ni Ranchi ya Zanzibar, Bagamoyo (Ranch of Zanzibar in Bagamoyo) Kwa simulizi kutoka kwa watangulizi wetu eneo la RAZABA ilikuwa ni zawadi ya Mwalimu Nyerere kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na lina ukubwa wa zaidi ya hekta elfu ishirini na nane.

Mto Wami, reli ya Tanga, Barabara ya Bagamoyo Msata, mto ruvu na bahari ya hindi ndio mipaka halisi ya RAZABA. Mmiliki wa RAZABA ni Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Kwa maana halisi, RAZABA ni eneo la Zanzibar ndani ya Tanganyika.

Hayati Mwalimu Nyerere alitoa eneo hilo ili kuwapa fursa Wazanzibari kumiliki mifugo yao wenyewe, na mifugo yote inayotoka maeneo ya Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma na kwingineko kwenda Zanzibar, ifikie RAZABA kabla ya kusafirishwa kwenda kutumiwa na wananchi wa Zanzibar.

Your browser is not able to display this video.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili mbona liko wazi Kuna shida kubwa sana ya Watanganyika kutokujua historia Na Kwani Smz KUWA na ardhi NDANINYA TANGANYIKA nikosa !!! mbona sisi Tz tuna majengo ya ubakozi tunamiliki mataifa mengi tu
Hatuwezi kuwa watumwa wa Historia za kipumbavu. Ni aidha tuwe na umiliki sawa kama Watanzania Serikali 1, au mbaki na Kisiwa chenu Muungano ufe.

Hakuna Muungano wa NusuNusu.
 
Unaitwa Muungano, lakini kwa jicho la 3 hapa mfano wake, ni kama Tanzania bara kamuoa Zanzibar. Na wakati wa uchumba ndiyo kuhongwa Ranchi hiyo na bado mengi tutayasikia.

Sasa kipindi kamili cha ndoa ndiyo, hii kuhudumia mke sasa mara kafutiwa deni lote la umeme.
Unajua ile mke, anadekezwa na kupewa kila anachotaka. Ndiyo nikionacho hapo.
 
🤣🤣
 
Na wakati wa uchumba ndiyo kuhongwa Ranchi hiyo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau na Mkaa ulitoka hapo kupakiwa katika majahazi
 
Umenifurahisha na huu mfano hasa ukitoka kwa kisura kama wewe
 
Pengine serikali yetu inastahili lawama kwenye hili kwa kukaa kimya sana na kuwaachia matapeli kufanya yao.. Hilo eneo watu wamepigwa mno na sio watu wadogo ni watu wazito na taasisi pia... Wapo
Wabunge
Mawaziri
Majaji
Mahakimu
Wanasheria
Makatibu wakuu nknk
Mojawapo ya taasisi zilizoathirika sana kwenye hili ni KKKT

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…