King junior
Member
- Apr 8, 2011
- 63
- 12
Wanafunzi wa UDOM-college of education, wapo mbioni kugoma ili kushinikiza utawala ukamilishe matakwa yao hususani ya fedha za kujikimu. Mwaka huu wa masomo wa 2011/2012 umekuwa tofauti kidogo hasa kwa mwaka wa pili na watatu katika kupata pesa zao za kujikimu. Mwaka wa masomo wa 2011/2012 umeanza tarehe 23 oktoba, na mpaka sasa pesa za kujikimu hazijatolewa kwa wanafunzi wote wa mwaka wa pili na watatu kutokana na masharti yafuatayo: 1-uongozi wa chuo unataka wanafunzi wote wafanye usajili ndipo wapate pesa hizo (wamesahau kama pesa ya accomodation is a part and parcel of boom) 2- wanafunzi wote wanatakiwa wasaini kiwango cha pesa Tshs 646,250, badala ya 670,000/-. Hata hivyo robo tatu ya wanafunzi wote wa mwaka wa pili na watatu wameshamaliza mchakato wa kusaini na kufanya usajili,cha ajabu hadi leo pesa zao hazijaingia badala yake wamepewa wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Tamko limetolewa na baadhi ya wanafunzi kuwa wasipoweka pesa kesho hadi saa sita mchana,wataandaa mgomo.