Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.

Mkuu,

Mimi ninaomba kukuuliza,

Wewe una miaka mingapi?

Umezaliwa wapi?

Je, unaijua asili yako? (hapa tunajua kuwa watu waliopo zanzibar walitoka Congo, Malawi, Msumbiji, Burundi, Tanganyika, nk)

Mwisho, je wewe ni muislam? (kama ni muislam kwa nini unajitambulisha hivyo?)
 
Bado sijashawishika eti kiongozi kuwa na dini fulani ndio chanzo cha umasikini wetu, hata wote wakiwa waislam au wakristo au wapagani kama wanafanya wanayotuahidi hapo shida iko wapi? kama sio wezi na walafi hapo shida iko wapi kama sio wabaguzi hapo shida iko wapi. Swala la kurukia kwamba hawa ni wale na wale ni hawa halijawahi kutatua matatizo yetu kama nchi. Tuwabane kwenye uwajibikaji na utawala wa sheria hapo hatutajali dini zao.

Tukumbuke kama sio wa kuteuliwa washiriki wa kupiga kura ni sie wote waislam, wapagani na wakristo. tutengeneze hoja za uwajibikaji. Mimi binafsi sijawahi kuona matatizo ya dini Tanzania, watu wengi wanabebana kwa kujuana na wala sio kwa dini zao.Haijalishi mnajuana na mna dini gani, hata ukiangalia wewe mwenyewe hapo ulipo utaona marafiki zako sio wa dini yako pekee yake na wakipanda watakubeba bila kujali dini zenu.Wakati wanaiba hawaangalii kwamba wana dini gani wanaangalia deal lipite.wakati wanapanga kuiba kura hawaangalii wanamsaidia nani wanaangalia ccm ipite hivyo tuwe makini na hii dhambi ya dini wao wanaitumia kutugawa wao wanaungana.
 

wampinge nani sasa? maana wote wanashinda msikitini na lao moja!

Ukweli kuwa kuna influence ya mwenyekiti wa chama kwenye baadhi ya position, kama watu wake ni waislamu basi ndio hivyo tena

Pia si siri kuwa JK amejaza 'watu wake' katika nafasi nyingi muhimu, sipati piacha kama ingekuwa kinyume chake. Lakini world wide inajulikana kuwa wakristo they do not mind wala ku-care, wao na mambo yao!

thats how we are, so kama mtu anataka JK ahukumiwe kwa hilo, kwa kifupi wakristo hawana muda huo, na hakuna atakayekusikiliza
 
This is too simplistic jamani. Yani tukiangalia ajira serikalini na kwenye mashiraka ya umma kwa mtazamo huu wa juu juu ni rahisi kufikia conclusion kuwa serikali ina udini-inapendelea Christians; lakini it is a false conclusion.....hamna udini hapa kwetu Tanzania.
 
mki taka kila kitu kiwe 50-50 basi itakuwa kazi. Wakristo na Waislamu wata taka nafasi nusu kwa nusu, wanaume na wanawake wata taka nafasi nusu kwa nusu, wabara na wazenji wata taka nafasi nusu kwa nusu na makabila yote wata taka 50-50. Can we fit in all these demands if they arise?
 
Last edited:
we Philemon Mikael na mtoa hoja inaonekana mawazo yenu ni finyu sana, na mawazo yenu hayapo katika ulimwengu wa sasa, hivi na idea yako pamoja na mtoa hoja unaweza ukajiita ni great thinker? embu kuwa kaka...umenitia aibu...
 

Ikifikia kugawana, basi kwenye dini kutakuwa na kazi kwelikweli,
Kwani kuna akina sie tusiokuwa wakristo wala waislam tutadai na sisi tugaiwe nafasi.
Hata hivyo ukienda zaidi kwenye hizo dini mbili yaani ukristo na uislam,
yataibuka makundi mengine, Sisi ni Shia na wao ni Sunni kwahiyo tugawane...
Upande mwingine utasema , sisi ni wakatoliki na wao ni waprotestanti, tugawane...

Kana kwamba haitoshi
Wale Shia watasema sisi ni shia msimamo mkali na wale ni msimamo wa kati, tugawane...
Huku waprotestanti watesama sisi ni walutheri na wao ni waangalikana, tugawane...

Tutaendelea kugawana, tutagawana weee... sijui tutaishia wapi?
 
Last edited:


- Heshima mbele sana mkuu, marekebisho kidogo mkuu, Waziri Sophia Simba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa UWT sio Mu-Islam ni mkatoliki.

Respect.

FMEs!
 

Swala la udini lisiwe hoja bali tuangalie uwezo wa kuliongoza jahazi wanao?
 

Give me a break!

Kwa mtu mwenye nafasi yako sikutegemea kuwa una mentality hizi

mbona hakuna anayelalamika kuhusus udini CHADEMA?

au mbona hakuna anayesema kitu kuhusu CHADEMA as chama cha watu wa chagga?

Game Theory = Pundamilia = Rostam Azizi
 

It is completely true Waberoya.
We Christians hatuna matatizo na kupigizana kelele na mambo ya udini katika siasa. Jamaa zetu wanamaindi hamna mfano. Kuna watu wakiwemo hata Maprofesa wanadai eti hata admissions za vyuo vikuu vinapendelea wakristo kitu ambacho hata hakiingii akilini.
 

CUF inapungua nguvu kwasababu wako mfukoni mwa RA. Hamkuwasikia Lipumba na Hamadi walivyomcharukia Mengi kwenye issue ya mafisadi papa? Mnafikiri ilikuwa bure tu?Pia inasemekana kuwa Lipumba na Seif wako karibu sana na mfanyabiashara mmoja maarufu huko Uarabuni ambaye ni swahiba wa RA. Pia msisahau kuwa Seif alishawahi kuwa waziri kiongozi wa Zanzibar kwahiyo anakula posho zinazoizinishwa na CCM so lazima awe mpole. So washirika wa CUF kwa ujumla hamna viongozi tafuteni chama kingine kama mna nia ya kuikomboa Tanzania kutoka mikononi mwa matapeli na wezi CCM.
 
Mbona umesahau katibu mkuu wa UMOJA WA WANAWAKE aliyeteuliwa hivi karibun HASNAT MWILIMA mwislam

MEYA WA JIJI- ADAM KIMBISA NI MWISLAM

MSAIDIZI MEYA-AHMED MWILIMA NI MWISLAM

Pundamilia amesahau kukwambia kuwa Waziri mkuu kipindi cha Mkapa alikuwa mkrsitu-Sumaye.

Hivyo MKAPA alikuwa na wasaidizi wote wakristu mfano makamu wa Mwenyekiti alikuwa John Malecela,waziri mkuu sumaye,katibu mkuu wa chama Philiph Mangula. katibu mkuu ofisi ya Rais Martin ,hawa ndio wasaidizi wakubwa wa rais au mwenyekiti wa chama kama udini basi Mkapa ni mdini.
wakati JK ana mizengo Pinda,makamba yusuf, PIUS MSEKWA na Luhanjo kama wasaidizi wake kiserikali na kichama.
 

NCCR MAGEUZI ilipoteza umaarufu wake na kupungua nguvu kabisa uchaguzi wa mwaka 2000,jee kwa vile MKAPA alikuwa mkristu mwenzao?

CUF ngome yake iko Zanzibar toka 1995 na kila chaguzi inazoa viti vya ubunge na ikishindika wanatembea dunia nzima kueleza kuwa uchaguzi wa Zanzibar haukuwa huru na Zanzibar inyimwe misaada na kutengwa na jumuiya za kimataifa kwanini wafanye hivyo huku wakazi wa zanzibar ni waislam na pia wagombea urais kupitia CCM huwa ni waislam.

toka 1995,2000 na 2005 CUF imeshiriki chaguzi hizo Zanzibar ikipambana na DR.Salmin Amour na Aman Karume ambao wote ni waislam udini wa CUF unatoka wapi?

Hoja ya udini iko huko kwanu Chadema kwani alipogombea MKAPA mwaka 1995 na mwaka 2000 Chadema haikuweka mgombea wa urais.alipokuja KIKWETE 2005 ndio CHADEMA ikasimamisha mgombea kwa mara ya Kwanza ambaye ni Mkristu bwana Mbowe na kutumia gharama kubwa za helkopta ambazo hazikutumika huko nyuma kipindi cha rais Mkristu MKAPA.Jee mlikuwa wapi chadema kusimamisha wagombea urais vipindi viwili vya rais mkristu bwana Mkapa akiwa JOHN MALECELA,FREDRICK SUMAYE,PHILIPH MANGULA NA MARTING LUMBANGA?

Ukitizama wabunge wa viti maalum wa CUF wamechukua wakristu toka Tanzania Bara ingawa wao hawana kiti cha mbunge Tanzania Bara, lakini cha chadema wamechukua wabunge wa viti maalum wanne toka Mkoa mmoja tu wa Tanzania yaani Kilimanjaro na hakuna mbunge hata mmoja toka Zanzibar jee mmewatenga ZANZIBAR kwa uislam wao? kama CUF wadini kina elizabeth Sakaya wangepata vipi ubunge wa viti maalum nao wametoka bara?
 
Mimi naomba waandishi wa Tanzania wabadilike.Kunahaja yakuwa tunapewa wasifu wa wagombea-kazi walizowahi kufanya na elimu zao.Hii itasaidia kuwaondoa watu wanaotaka kutetea maslahi ya mafisadi.Elimu ya Bulembo hafai hata kuwa diwani kazi yake ni usanii tu.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…