Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,928
Mwanakijiji! mzee wetu Mohamed Said ameianza nakala yake kwa kuturudisha nyuma kidogo na habari ya yule Sheikh aliyerudishwa "kwao" Zanzibar halafu akaendelea kutupeleka mwaka 1964 wakati masheikh wengi waliwekwa kizuizini, hakutuacha hapo bali alitukumbusha mwaka 1993 ambapo kulizuka tafrani kati ya askari na Waislamu akamalizia tukio la Sheikh Kishki juzijuzi na Mufti wa Yemen halafu akaunganisha na lilomkuta yeye.
Huu ni mlolongo wa matukio baada ya matukio haiwezekani ulifananishe na tukio moja la Ulimboka au na jingine kama la Ulimboka pale na hapa......mwisho kauli yako imenishangaza sana kwani inaonekana kuihukumu Serikali kuwa na hatia ya utekwaji wa Ulimboka!
Mohamed said ametuletea udhalilishwaji wa Waislamu unaofanywa na vyombo vya dola, wakati ya Ulimboka ndio kwanza uchunguzi unaendelea!
Vyombo vya dola mwaka 2006 kama ilivyo leo vinaongozwa na Waislamu. Kwanini wasiseme ni waislamu serikalini wanawadhalilisha Waislamu wenzao? Mwaka 1964 waliowekwa kizuizini hawakuwa waislamu peke yao.