Tanzania itajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno!.
Kadri siku zinavyokwenda ndivyo ninavyozidi kumkumbuka Mwalimu Nyerere. Sera yake ya Ujamaa na Kujitegemea ililenga njia zote kuu za uchumi ziwe mikononi mwa umma ili kitakachopatikana, tukigawane kwa wote, Hali sasa ni tofauti, gap kati ya wenye nacho na wasionacho linazidi kukua. Sasa tuna makundi matatu ya nchi, Wenyenchi, Walanchi na Wananchi!.