Fanfa
JF-Expert Member
- Sep 25, 2009
- 2,388
- 3,710
Hivi karibuni ndugu Polepole baada ya kujiuzuru ubalozi ame-trend sana na kujipatia maujiko (umaarufu) kuwa ni mpigania haki, demokrasia na utawala Bora.
Swali la kujiuliza ni kweli Polepole ana uchungu na mpigania haki, demokrasia na utawala Bora???.
Hebu tujiulize maswali mengine haya tena.
1. Tundu Lissu alipopigwa risasi akipigania haki, Demokrasia na utawala Bora, ndugu Polepole aliwahi kumpa pole Lissu au hata kwenda kumsalimia akiwa hospitali kama ishara ya kumuunga mkono ??
2. Polepole akiwa kama mwenezi wa CCM mwaka 2017 wakati Tundu Lissu alipopigwa risasi, aliwahi kulaani kitendo hicho cha kinyama??? kuonyesha kuwa anakerwa na uvunjifu wa wazi wa haki, demokrasia na utawala Bora.
3. Wakati wa utawala wa kikatiri wa mwendazake, ambao haukuzingatia haki, demokrasia na utawala Bora, huku yeye Polepole akiwa mwenezi wa CCM, mbona hakuwahi kupinga au kulaani utawala ule wa kidikteta na mabavu uliokuwa unavunja haki, demokrasia na utawala Bora ????
4. Wakati wa utawala wa mwendazake mambo ya utekaji, kutesa na kuwaua watu ulishamiri, huku Polepole akiwa Mwenezi, mbona hatujasikia anayakemea kwa nguvu matendo hayo maovu ya kikatiri na kishenzi????. Na hata yalipoendelezwa na utawala wa sasa hadi yakazidi vipimo mbona alikuwa kimya siku zote hatukusikia kuyakemea???
5. Baadhi ya Mbuga za wanyama wamepewa waarabu, bandari kubwa wakapewa waarabu, mapori wakapewa waarabu, viwanja vya ndege wakapewa waarabu. Mbona hatujasikia polepole anapinga mambo haya ya hovyo na ya kuiangamiza taifa.???
6. N.k
Tuendelee kujiuliza maswali ni kweli Polepole ni mzalendo na mwenye uchungu wa nchi yake kama anavyojaribu kujinasibu????
Wakati tunaendelea kujiuliza maswali mengi haya haina maana kwamba mtawala wa sasa anafuata misingi ya haki, demokrasia na utawala Bora, bali yeye kamzidi hata mtangulizi wake kwa mambo ya hovyo tunayoyahoji. Pengine ni kwa sababu alikuwa ni sehemu ya uasisi wa matendo hayo maovu labda ndo sasa anaya-practice vizuri zaidi.
Swali la kujiuliza ni kweli Polepole ana uchungu na mpigania haki, demokrasia na utawala Bora???.
Hebu tujiulize maswali mengine haya tena.
1. Tundu Lissu alipopigwa risasi akipigania haki, Demokrasia na utawala Bora, ndugu Polepole aliwahi kumpa pole Lissu au hata kwenda kumsalimia akiwa hospitali kama ishara ya kumuunga mkono ??
2. Polepole akiwa kama mwenezi wa CCM mwaka 2017 wakati Tundu Lissu alipopigwa risasi, aliwahi kulaani kitendo hicho cha kinyama??? kuonyesha kuwa anakerwa na uvunjifu wa wazi wa haki, demokrasia na utawala Bora.
3. Wakati wa utawala wa kikatiri wa mwendazake, ambao haukuzingatia haki, demokrasia na utawala Bora, huku yeye Polepole akiwa mwenezi wa CCM, mbona hakuwahi kupinga au kulaani utawala ule wa kidikteta na mabavu uliokuwa unavunja haki, demokrasia na utawala Bora ????
4. Wakati wa utawala wa mwendazake mambo ya utekaji, kutesa na kuwaua watu ulishamiri, huku Polepole akiwa Mwenezi, mbona hatujasikia anayakemea kwa nguvu matendo hayo maovu ya kikatiri na kishenzi????. Na hata yalipoendelezwa na utawala wa sasa hadi yakazidi vipimo mbona alikuwa kimya siku zote hatukusikia kuyakemea???
5. Baadhi ya Mbuga za wanyama wamepewa waarabu, bandari kubwa wakapewa waarabu, mapori wakapewa waarabu, viwanja vya ndege wakapewa waarabu. Mbona hatujasikia polepole anapinga mambo haya ya hovyo na ya kuiangamiza taifa.???
6. N.k
Tuendelee kujiuliza maswali ni kweli Polepole ni mzalendo na mwenye uchungu wa nchi yake kama anavyojaribu kujinasibu????
Wakati tunaendelea kujiuliza maswali mengi haya haina maana kwamba mtawala wa sasa anafuata misingi ya haki, demokrasia na utawala Bora, bali yeye kamzidi hata mtangulizi wake kwa mambo ya hovyo tunayoyahoji. Pengine ni kwa sababu alikuwa ni sehemu ya uasisi wa matendo hayo maovu labda ndo sasa anaya-practice vizuri zaidi.