Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Kumbe ni hatari tena hatari sana kujaribu kuzuia ufisadi. Hatari hii wanaharakati na wapiganaji maarufu kama Mwanakijiji wameifumbia macho au hawajui kuwa ipo. Hii ni hatari ya kujaribu kuvuruga mfumo ambao kumbe ndio unaoendesha nchi. Huu ndio mfumo utupao nishati ya umeme, huduma za maji, elimu, afya na kadhalika. Kila kunapokuwa na jitihada za kuutibua mfumo huu basi nchi huingia gizani, kipindupindu huzuka na magonjwa lukuki hutuvamia. Heri tuuache mfumo wa zimwi likujualo uendeshe nchi yetu hivyo hivyo tu!
Kwa ufupi huu ndio mfumo ambapo Mtanzania aliyeliona jua kuanzia 1985 na hasa 1995 huzaliwa, hulelewa, hukua na hata hufa. Kama anavyonena Mwana wa Ulimwengu katika Rai ya Jenerali, mtoto aliyezaliwa katika ufisadi (na naongezea, aliyezaliwa kifisadi), na kulelewa kifisadi basi huishia kuwa fisadi tu. Naam na kama unavyothibitisha Utafiti wa gazeti la The Citizen, Mtanzania kwa kawaida hupitia hatua elfu za ufisadi toka anapozaliwa hadi anapoingia kaburini. Kwa kawaida cheti chake cha kuzaliwa hupatikana kifisadi, hupata nafasi ya kujiandikisha darasa la kwanza kifisadi, hutumia desa au mafeki kufaulu mitihani ya taifa na ikibidi hufanya ufisadi ili afaulishwe. Safari hiyo ya kifisadi haishii hapo. Kama akiwa dereva basi kwa kawaida hupata leseni ya udereva kifisadi, akipata ajali basi husamehewa na matrafiki kifisadi. Siku akiamua kumiliki ardhi au nyumba basi hupata hatimiliki kifisadi. Na hata akitaka kuwa kiongozi basi hupata kura kifisadi na pia huweza hata kutumia cheti cha uprofesa wa kifisadi ili atinge mjengoni. Hata harakati na upiganaji hufanyika kifisadi pia, kama huamini waulize mashujaa wa vita dhidi ya ufisadi ni jinsi gani wanapata taarifa za ufisadi na huwa wanazipata kwa nani na wakati gani!
Kwa ujumla hayo ni maisha ambayo yanaendeshwa kwa uchumi wa kifisadi. Huu ndio uchumi unaomfanya dereva wa taxi amuulize mteja wake aandike shilingi ngapi kwenye risiti kana kwamba hajui bei halali anayopaswa kuandika ni shilingi ngapi! Ni mfumo ambao umeufanya ufisadi ujikite katika nyoyo na fikra za wananchi na jamii kwa ujumla. Hakika kikulacho ki nguoni mwako, naam ufisadi u nguoni mwetu. Kumbe yule mtafiti tuliyetaka kumpiga mawe alikuwa sahihi aliposema kuwa uchumi wetu ni wa kujaliana, naam, kifisadi!
Kwa ufupi huu ndio mfumo ambapo Mtanzania aliyeliona jua kuanzia 1985 na hasa 1995 huzaliwa, hulelewa, hukua na hata hufa. Kama anavyonena Mwana wa Ulimwengu katika Rai ya Jenerali, mtoto aliyezaliwa katika ufisadi (na naongezea, aliyezaliwa kifisadi), na kulelewa kifisadi basi huishia kuwa fisadi tu. Naam na kama unavyothibitisha Utafiti wa gazeti la The Citizen, Mtanzania kwa kawaida hupitia hatua elfu za ufisadi toka anapozaliwa hadi anapoingia kaburini. Kwa kawaida cheti chake cha kuzaliwa hupatikana kifisadi, hupata nafasi ya kujiandikisha darasa la kwanza kifisadi, hutumia desa au mafeki kufaulu mitihani ya taifa na ikibidi hufanya ufisadi ili afaulishwe. Safari hiyo ya kifisadi haishii hapo. Kama akiwa dereva basi kwa kawaida hupata leseni ya udereva kifisadi, akipata ajali basi husamehewa na matrafiki kifisadi. Siku akiamua kumiliki ardhi au nyumba basi hupata hatimiliki kifisadi. Na hata akitaka kuwa kiongozi basi hupata kura kifisadi na pia huweza hata kutumia cheti cha uprofesa wa kifisadi ili atinge mjengoni. Hata harakati na upiganaji hufanyika kifisadi pia, kama huamini waulize mashujaa wa vita dhidi ya ufisadi ni jinsi gani wanapata taarifa za ufisadi na huwa wanazipata kwa nani na wakati gani!
Kwa ujumla hayo ni maisha ambayo yanaendeshwa kwa uchumi wa kifisadi. Huu ndio uchumi unaomfanya dereva wa taxi amuulize mteja wake aandike shilingi ngapi kwenye risiti kana kwamba hajui bei halali anayopaswa kuandika ni shilingi ngapi! Ni mfumo ambao umeufanya ufisadi ujikite katika nyoyo na fikra za wananchi na jamii kwa ujumla. Hakika kikulacho ki nguoni mwako, naam ufisadi u nguoni mwetu. Kumbe yule mtafiti tuliyetaka kumpiga mawe alikuwa sahihi aliposema kuwa uchumi wetu ni wa kujaliana, naam, kifisadi!