Uchumi wa Canada una nini cha ziada?

Uchumi wa Canada una nini cha ziada?

Mkuu Boss, Canada kulikuwa na tukio moja la kihistoria lililoitwa Klondike Gold Rush ambalo lilitokea katika kipindi cha miaka mitatu tu! 1866 hadi 1899.

Hiyo Dhahabu ilikuwa ni bomba kuliko hata ile ya Kimberly Afrika Kusini.

Hiyo Dhahabu ndiyo khasa iliyowatoa waCanada pamoja na maliasili zingine.

Soma link hii ukipata muda na utaelewa. Klondike Gold Rush - Wikipedia, the free encyclopedia

Thanks muu ngoja niitazame hii
 
Hawa wanategemea sana
1. Logging - sijui niite mbao au magogo
2. Mafuta
3. Viwanda vya magari
4.Viwanda vya kutengeneza ndege - hata hizi mpya za ATC zimenunuliwa huko
5. Uvuvi
6. Kutengeneza na kuuza vyakula vitokanavyo na samaki - seafood industry nadhani wanashika namba nane hapo
9. Kwenye software pia wapo vizuri hasa entertainment softwares

Lakini pia Canada ndiyo nchi yenye kiwango cha juu kabisa katika ''economic freedom''.

Export ya nchi ya Canada ni kubwa mno kutokana na mauzo ya bidhaa asili, zile za viwandani kwenda nchi za nje.
 
Hata Sweden wana utawala bora
but huioni top ten
Canada wana produce nini zaidi?
Mkuu mafuta, gas, madini, mbao ( mteja mkubwa USA na China) Kilimo, kodi (serikali ipo serious sana na ulipaji kodi) kikubwa zaidi utawala bora. Canada spends very little kwenye mambo kujihusisha na ugomvi wa mataifa yanayopigana. Wao kubwa kwao ni wahamiaji kuinua uchumi na Elimu bora.
 
Ili inchi ipae kiuchumi inahitaji watu walioelimika na uongozi bora (good governance). Canada inavyo hivi vyote. Mbali na hapo wana rasilimali, mafuta, viwanda, kifupi uchumi wao uko diversified so wana earn kwingi.

Huku Afika tunakosa watu walioelimika na uongozi bora ndio maana hata rasikimali ziwe nyingi vipi bado ni vituko na viroja.

Mtaji pekee taifa linapaswa kuwa nao ni watu. Watu walioelimika. Elimu elimu elimu.
 
Ili inchi ipae kiuchumi inahitaji watu walioelimika na uongozi bora (good governance). Canada inavyo hivi vyote. Mbali na hapo wana rasilimali, mafuta, viwanda, kifupi uchumi wao uko diversified so wana earn kwingi.

Huku Afika tunakosa watu walioelimika na uongozi bora ndio maana hata rasikimali ziwe nyingi vipi bado ni vituko na viroja.

Mtaji pekee taifa linapaswa kuwa nao ni watu. Watu walioelimika. Elimu elimu elimu.

Hata Israel inatuacha sisi TZ wakati ni kinchi kidoogo mno
 
ni nchi kubwa sana hivyo inarasili mali nyingi sana. pia raia wake ni wasomi hilo linawafanya kuweza kuextract hizo mali kiweledi. kingine wanautawala bora na sheria zinazojali property rights. siyo africa ukivuna serikali inatake control ya mali yako.
 
Canada wamejikita zaidi kwenye elimu bora na kufanya wananchi wake kuwa na maisha bora kwa elimu yao, wengi wao wanamiliki nyumba.
Sio kama nchi zingine ambazo fedha nyingi wanawasaidia wananchi wasiojiweza poor peple who just wait to be fed by government
 
Hata Israel inatuacha sisi TZ wakati ni kinchi kidoogo mno
Mkuu hapa ndio unapata jibu tunakosa vitu viwili vya msingi. Watu walioelimika na siasa safi (good governance). Israel hawana rasilimali lakini wanawatu walioelimika na serikali imara. Nikisema serikali imara namaana strong institution si kiongozi mmoja anayejiamulia lolote aonalo linafaa.

Mkuu ukiangalia hata nchi za Asia kama Singapore zinapaa kiuchumi kwasababu wamewekeza tutengeneza generation ya watu walioelimika na upande mwingine serikali inajitahidi kuwa ya kidemokrasia zaidi kuvutia wawekezaji/wafanyabiasha ili kuchochea ushindani na ukuuaji wa uchumi.

Watu walioelimika na siasa safi ndio njia pekee kuvunja minyororo ya umasikini kwa watu wetu.
 
Enzi hizo nadhani Std. V or VI somo la jiografia - kilimo cha ngano Canada huko katika mbuga za Saskatchewan. Nadhani ngano iliwainua sana hawa jamaa.

Kubwa kuliko yote, kilichowainua zaidi ni kuwekeza sana katika brains za watu wao na kutumia brains hizo kubadili mazingira na maliasili zao kwenda katika tafsiri halisi na sahihi ya UCHUMI.
umenikumbusha saskatchewan manitoba na alberta ilikuwa mahrufu sana kwa ngano pale
 
Ili inchi ipae kiuchumi inahitaji watu walioelimika na uongozi bora (good governance). Canada inavyo hivi vyote. Mbali na hapo wana rasilimali, mafuta, viwanda, kifupi uchumi wao uko diversified so wana earn kwingi.

Huku Afika tunakosa watu walioelimika na uongozi bora ndio maana hata rasikimali ziwe nyingi vipi bado ni vituko na viroja.

Mtaji pekee taifa linapaswa kuwa nao ni watu. Watu walioelimika. Elimu elimu elimu.

Unaleta uchochezi
 
Mkuu kwa usahihi wako kwenye G8 na members kamili ni kama ifuatavyo

USA
UK
JAPAN
GERMANY
CANADA
ITALY
FRANCE
RUSSIA

Hawa ndio wababe kiviwanda duniani. Ila sijui kwa nini CHINA haimo.

Kwenye hii list naona China itakuwa ya pili kwenye kumi bora ya uchumi imara kufikia 2030:



Kufikia 2050 ripoti ya EIU inatabiri China itaongoza kuwa na sarafu yenye biashara, ikiipiku Marekani. Japo katika matumizi ya mtu mmoja mmoja, wanatabiri China haitakuwepo hata kwenye kumi bora

http://pages.eiu.com/rs/783-XMC-194/images/Long-termMacroeconomicForecasts_KeyTrends.pdf

Ujuzi wangu wa uchumi ni mdogo, wataalam tuelewesheni tafadhali. Inamaana tabaka la wasionacho litaongezeka ndio maana? Au hii inawezekana vipi?
 
Hata Israel inatuacha sisi TZ wakati ni kinchi kidoogo mno
alafu kipo jangwani maji yao yote wanafanyia recycle sisi tunamaji mpaka yakuchezea lakini ukimaliza km tano kunawatu wanashida kubwa isiyoelezeka ya maji
 
Hapo nimepata picha kwamba nchi hata kama ina uchumi mkubwa lakini population yake ni kubwa mfano nigeria ina wakazi wapatao mil400 jiji la lagos pekee lina idadi ya watu wa tanzania nzima!
Hapa ndipo pananichanganya maana logically nchi ikiwa na wakazi wengi uchumi unakuwa mkubwa sababu mzunguko wa pesa pia unakuwa wa kutosha ila ajabu kwa nchi kama nigeria ambae ni ya kwanza africa kwa utajiri wa mafuta lakini maisha yao ni duni.ipo tofauti hapo na nchi ya libya hapo awali ilikuwa na wakazi wasiozidi mil20 na waliishi kama peponi.
Hapa ndio pa kujipima kwa population yetu hii na hali yetu ya uchumi wa ubabaishaji maendeleo tutaona katika tv tu
 
Hapo nimepata picha kwamba nchi hata kama ina uchumi mkubwa lakini population yake ni kubwa mfano nigeria ina wakazi wapatao mil400 jiji la lagos pekee lina idadi ya watu wa tanzania nzima!
Hapa ndipo pananichanganya maana logically nchi ikiwa na wakazi wengi uchumi unakuwa mkubwa sababu mzunguko wa pesa pia unakuwa wa kutosha ila ajabu kwa nchi kama nigeria ambae ni ya kwanza africa kwa utajiri wa mafuta lakini maisha yao ni duni.ipo tofauti hapo na nchi ya libya hapo awali ilikuwa na wakazi wasiozidi mil20 na waliishi kama peponi.
Hapa ndio pa kujipima kwa population yetu hii na hali yetu ya uchumi wa ubabaishaji maendeleo tutaona katika tv tu


Nigeria hata milioni 200 hawajafika..ndo wanakaribia
 
Back
Top Bottom