Inaonekana wazazi wako wawili wanavutana juu ya hili jambo, mzazi wako mmoja hataki uolewe huko (kisingizio kinakuwa dini) na mwingine anakutakia kila la kheri na mabaya yakuepuke huko kwa mumeo (yuko tayari kwa vyovyote uolewe)
Anayekubali uolewe inaonekana ana turufu. (i guess ni MAMA) sasa baba anataka kutumia ubabe wa hoja yake kuungwa ili amfelishe mkewe (mama yako)
Kaitisha hicho kikao kawaita nduguze wa kiumeni (sio ujombani kwake) na ndugu wa mama yako kawachagua wenye msimamo mkali (unaofanana na wake) ambao nao ni wa kiumeni.
Kikao kimefanywa na watu wenye silika moja wakaikandamiza turufu ya mama yako isisikike wala kuwa na mashiko kutokanana na wingi wao.
Neno "kikao cha ukoo" ndio kimemtahayarisha mtetezi wako, kwa kuwa yeye hawezi kurudi kwao kuiacha ndoa yake kwa ajili ya kutetea wewe uwe na mji wako nao wapate wajukuu, anaamua kufa na tai shingoni.
Ninao ushauri nitakupa lakini unithibitishie hutokani na wachaga, wapare, wanyakyusa, wasukuma (wanyatuzu) na angalau uislam.