Uchumba wangu upo mashakani

Uchumba wangu upo mashakani

Sumia kwani wewe msimamo wako ni upi ili tukushauri kutokea hapo?
Uelewa kuwa mwenye jukumu la maisha yako ni wewe ila wazazi wapo kukuongoza (kukushauri) il kufuata njia iliyo sahihi.
Wakati mnaanza uhusiano wenu je mliangalia suala la dini na kukubaliana jinsi ya kulikabidhi?
 
Kati ya hao waliokaa kikao cha kuamua kurudisha mahari kuna mmoja wapo ameonyesha nia ya kukuposa?
 
Inaonekana wazazi wako wawili wanavutana juu ya hili jambo, mzazi wako mmoja hataki uolewe huko (kisingizio kinakuwa dini) na mwingine anakutakia kila la kheri na mabaya yakuepuke huko kwa mumeo (yuko tayari kwa vyovyote uolewe)

Anayekubali uolewe inaonekana ana turufu. (i guess ni MAMA) sasa baba anataka kutumia ubabe wa hoja yake kuungwa ili amfelishe mkewe (mama yako)

Kaitisha hicho kikao kawaita nduguze wa kiumeni (sio ujombani kwake) na ndugu wa mama yako kawachagua wenye msimamo mkali (unaofanana na wake) ambao nao ni wa kiumeni.

Kikao kimefanywa na watu wenye silika moja wakaikandamiza turufu ya mama yako isisikike wala kuwa na mashiko kutokanana na wingi wao.

Neno "kikao cha ukoo" ndio kimemtahayarisha mtetezi wako, kwa kuwa yeye hawezi kurudi kwao kuiacha ndoa yake kwa ajili ya kutetea wewe uwe na mji wako nao wapate wajukuu, anaamua kufa na tai shingoni.

Ninao ushauri nitakupa lakini unithibitishie hutokani na wachaga, wapare, wanyakyusa, wasukuma (wanyatuzu) na angalau uislam.
 
Poleni sana ila kama mnapendana hivyo na hauko tayari kumpoteza basi fuata moyo wako. Wewe ndiye utakayeishi na mume wako na si wazazi wako na wachumba wenyewe siku hizi wenye mapenzi ya kweli ni nadra sana kuwapata. Kila la heri.
sumia
 
Last edited by a moderator:
Hakika ushauri wenu wanajamvi unanifungua macho sana,naanza kuona vitu ambavyo Hapo
awali nilikuwa civioni naamini kupitia ushauri mbalimbali nilioupata na ninaoendelea kuupata nitatoa maamuz yaliyo sahihi
 
Kiafrika mahari ikishatolewa maanake ndoa tayari.
Hao wazazi wako wana roho ngumu.
Ila sishangai ndiyo baadhi ya wazazi wapo hivyo. Kikubwa ambacho hawajui ni kwa kiasi gani wanaingiza maumivu mioyoni msa watoto wao.
Its very painful to be rejected kwa staili hiyo.
Mimi nakupa ushauri fuata maamuzi ya wazazi wako kwani hiyo ndoa itakuwa ya mashaka mashaka sana , hata mkizinguana huko mbeleni mnaweza kuwekeana Majuto au pengine kuona hili ndiyo sababu, let it pass pole sana.
 
Wazazi hawamtishi ila lazima achunguze wazazi wameshtuka nini hadi kutaka kurudisha hiyo posa????
Kwa kweli awasikilize wazazi wake, mimi naamini ni mzazi pekee ndio mwenye huruma kwa mwanae ivo hawezi kumuongoza mwanae kwenye njia isiyo sahihi.
Inategemea kwani wao ni binadamu si kila wakati wako sahihi
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Duh! Unasema kweli au unatania Mamndenyi!? Kuchapwa na mikanda kwa kosa lipi!? Kufall in love with someone from another religion!? SMDH!!!
Mamndenyi
 
Last edited by a moderator:
Wazazi wametazama mbaali wakaona bora nusu shari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom