Tafadhali kwa yeyote anayejua au anao uzoefu wa gharama za uchimbaji wa visima naomba anielezee mchanganuo wake akijumuisha na gharama za uchunguzi (surveying) eneo nilipo ni Mbeya km 8 kabla ujafika Uyole barabara kuu ya kutokea Makambako. Vilevile anayejua makampuni ya uchimbaji visima yanayopatikana Mbeya na namba zake anisaidie.