Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,453
- 40,446
Mapenzi ni sanaa,
Na inapotokea mtu mmoja kumpenda mwingine, ina maana amekukabidhi hisia zake zote kwako.
Kwa hiyo mnatakiwa kwa pamoja, mjaliane, mchekeshane, muondoleane msongo wa mawazo, na mjadili ni kipi kitakuwa hatima yenu; Je, ni kuoana, kulana tu, au kupeana mawazo mbalimbali ya maisha.
Unaweza kununua mbuzi, kuku, n.k au ukaamua kununua nyama kilo tano; mkaiandaa vizuri kwa ajili ya kuichoma; na ulaji wake unatakiwa uwe unakatakata kidogo kidogo ikiwa jikoni, mnakuwa mnakula na mpenzi wako, huku kinywaji kikiwa kwa pembeni.
Katika mazingira hayo mnatakiwa muwe wawili tu; huku mkijadili nini hatima ya mahusiano yenu.
Baada ya muda mtajikuta mko katika mazingira fulani, na mwisho wa siku mtajiona mko sahihi na mahusiano yenu yatadumu.
Kama eneo lako ni dogo au mazingira hayaruhusu, unaweza kukodi eneo kwa muda, apartment, au ukaamua kutoka nje ya mji na ukahamisha familia wenyeji kwa muda.
Na inapotokea mtu mmoja kumpenda mwingine, ina maana amekukabidhi hisia zake zote kwako.
Kwa hiyo mnatakiwa kwa pamoja, mjaliane, mchekeshane, muondoleane msongo wa mawazo, na mjadili ni kipi kitakuwa hatima yenu; Je, ni kuoana, kulana tu, au kupeana mawazo mbalimbali ya maisha.
Unaweza kununua mbuzi, kuku, n.k au ukaamua kununua nyama kilo tano; mkaiandaa vizuri kwa ajili ya kuichoma; na ulaji wake unatakiwa uwe unakatakata kidogo kidogo ikiwa jikoni, mnakuwa mnakula na mpenzi wako, huku kinywaji kikiwa kwa pembeni.
Katika mazingira hayo mnatakiwa muwe wawili tu; huku mkijadili nini hatima ya mahusiano yenu.
Baada ya muda mtajikuta mko katika mazingira fulani, na mwisho wa siku mtajiona mko sahihi na mahusiano yenu yatadumu.
Kama eneo lako ni dogo au mazingira hayaruhusu, unaweza kukodi eneo kwa muda, apartment, au ukaamua kutoka nje ya mji na ukahamisha familia wenyeji kwa muda.