Uchambuzi na Marekebisho ya Rasimu ya Mtaala wa Elimu: Kuondoa Mambo ya Dini na Masuala Mengine ya Kukinzana na Katiba

ichumu lya

JF-Expert Member
Aug 11, 2016
2,605
2,729
Mimepitia na kufanya uchambuzi katika rasimu ya mtaala wa elimu iliyotangazwa na Waziri wa Elimu inahitaji marekebisho kabla ya kupitishwa rasmi na kuwa mtaala unaofaa. Ni muhimu kuondoa kabisa mambo ya dini yanayoweza kusababisha machafuko. Nakumbuka mwaka 2014 tulipopendekeza kuondolewa kwa mambo ya dini, lakini sasa wamerudisha kijanja. Nani yuko nyuma ya dini?

Kuna vitu vingi tulivyokataa, lakini wanavilazimisha:

1. Kuwekwa kwa swala la dini kwenye mtaala huu litasababisha malumbano au hata vurugu. Nchi hii haiongozwi kwa misingi ya dini, ingawa watu wake wana dini na wengine hawana. Ukisoma kwa makini rasimu hii, unaona kuwa nchi inaingia mkenge wa dini: Elimu ya biashara wameipa umuhimu wa kitaalamu, elimu ya dini ya Kiislamu, lakini wakristo na wasio na dini wameachwa wapi? Je, mtaala huu umechukuliwa kutoka Zanzibar na kuhamishiwa Tanganyika? Kuna maswali mengi sana bado tunajiuliza, je, lengo lao ni kuleta mfarakano na watafika wapi na ligi wanayotaka kuanzisha?

2. Mtaala huu unakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 🙄.

13.-(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.

(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake.

(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka.

Usawa wa binadamu Sheria ya 1984 na. 15 ib. 6 Usawa mbele ya Sheria Sheria Na. 15 ya 1984 ib. 6 Sheria Na. 4 ya 1992 ib. 8 Sheria ya 2000 na. 3 ib. 5 Sheria ya 1994 na. 7. Fungu la 8[1], [k].

Ukisoma vifungu hivi unaona Waziri anavyoingiza nchi kwenye mgogoro wa kikatiba na mimi kutokea hapo niko tayari kupinga vifungu hivi mahakamani kuzuia Mtaala huu wenye ubaguzi kupishwa. Tayari nimemwandikia Waziri e-mail nikimkumbusha kwenye maoni tulivyopinga mambo ya dini kuingizwa kwenye mtaala wa Elimu, na hii ndiyo sababu kuu iliyomfanya Rais Magufuli kuukataa. Najua kuna lengo ovu, ila tutashughulika nalo kisheria.

2. CHAKULA mashuleni tulisema jukumu la chakula ni jukumu la serikali, sio jukumu la wazazi. Kwakuwa Elimu bure ni pamoja na chakula, lakini wao wameliacha hewani bila kuonyesha mwenye wajibu. Hili tukiliacha hivi, litafungua mlango kwa serikali kuwalazimisha wazazi kupeleka chakula shuleni kama ilivyo leo. Tunataka swala la Elimu libaki mikononi mwa Serikali, maana wakati wanaomba kura walinadi elimu bure, na hawawezi kulikwepa. Na kwakuwa sera ya CCM ndiyo inayotekelezwa, ni vyema wakahakikisha watoto wetu wanapata chakula shuleni, ama watwambie kwamba wameshindwa. Tufanye maamuzi kama wenye nchi, apo nasimama na kifungu hiki 🙄.

(a) Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii.

(b) Lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi
(C) Serikali itawajibika kwa wananchi;

Niwakumbushe kwamba serikali inawajibika kwa wananchi sio wananchi kuwajibika kwa serikali kama ilivyo sasa.

3. Tulipendekeza elimu ya ufundi aina zote ifundishwe kuanzia darasa la tatu ili kupata utaalamu wakiwa na uwezo mzuri wa kufundishika na apo ndipo tunaweza kupata matokeo mazuri ya watoto wetu kujua nini wanataka kufanya mbeleni, tutapata mafundi wa vyombo mbalimbali tutapata wataalamu na wahandisi lakini pia tutaondoa utegemezi wa ajira unaoitesa dunia.
 
Sasa mbona hayo masomo ya dini yanafundishwa huko mashuleni kwa miaka nenda! Lengo unataka vipindi vya dini visitambulike! Au unataka visiwepo kabisa?

Au hayo mapendekezo mapya yanaongelea kitu gani hasa chenye mkanganyiko wa dini?
 
Sasa mbona hayo masomo ya dini yanafundishwa huko mashuleni kwa miaka nenda! Lengo unataka vipindi vya dini visitambulike! Au unataka visiwepo kabisa?

Au hayo mapendekezo mapya yanaongelea kitu gani hasa chenye mkanganyiko wa dini?
Vipindi vya dini vinapaswa kuondolewa katika shule za umma. Huwa kuna ufidhuli wa kulazimisha wanafunzi wote kuhudhuria vipindi vya kidini.
 
mkuu tuwekee hiyo rasimu
Mageuzi makubwa
Elimu nchini

. Prof Mkenda asema Rais Samia kuweka Historia

. Lugha Nne kufunzwa, Mkazo maadili, Chakula Shuleni

Na. Mwandishi Wetu

Ikiwa ndiyo injini ambayo nchi inawajengea uwezo wa kiakili na kitaaluma raia wake, mitalaa (mitaala) ya Elimu nchini imefanyiwa maboresho makubwa kuielekeza kwenda kumtoa mhitimu mahiri (competency based) ili nchi ipate wataalamu stahiki kwa maendeleo na ustawi.

Maboresho hayo yamelenga kwenye Elimu na ujuzi (knowledge), nyenzo za utendaji (skills), ubora na tabia njema anayotakiwa kuwa nayo mhitimu huyo kumtofautisha na wanajamii wengine ambako kutamjengea kuheshimika, kujiamini na kuwa tegemeo la jamii katika kujibu changamoto anuai.

Hayo anasema Profesa Adolf Mkenda Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi akiweka hadharani kukamlika kwa rasimu ya mtalaa(mtaala) wa elimu nchini katika kutekeleza maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan juu ya kufanyika kwa mageuzi makubwa ya mfumo wa Elimu nchini.

“Curriculum should therefore, meet the needs of the individual citizens and the Nation. With this principle in mind and in accordance with the Sustainable Development Goals”, anasema Profesa Mkenda akikazia kwamba mtalaa wa Elimu kwa ajili hiyo unapaswa kukidhi mahitajio ya jamii na nchi sawia, hili ndilo zingatio lakini pia katika kufika malengo ya Maendeleo endelevu.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaweka Historia ya kutukuka itakayokumbukwa na vizazi vijavyo na kwamba aliangalia mbali katika kuibua wazo la kuboreshwa mitalaa hivyo wao kama Watendaji na watekelezaji, wamekuja na rasimu yenye kujumuisha mambo kadhaa yendanayo ambayo ni umilisi (fluency) wa lugha nne kuu duniani sanjari Kiswahili kama lugha ya Taifa na ya kufundishia.

“The need for curriculum change is prompted by many factors (hitajio la mageuzi ya mtalaa huibuliwa na sababu nyingi), kwa sisi moja ya sababu hizo, tumelenga kumuwezesha mwanafunzi kuelewa lugha muhimu sanjari kuelewa dhana (concepts) za masomo bila ya kikwazo cha lugha ambacho kilisababisha wanafunzi kukariri badala ya kuelewa masomo hali iliyoleta athari hasi katika utendaji ambapo, kuchangia na upungufu wa kimtaala, alama alizopata Mwanafunzi darasani haziakisi kwenye utendaji wake katika maisha halisi”, amesema Prof Adolf Mkenda.

Aidha mambo mengine yaliyojumuishwa katika rasimu hiyo inayotarajiwa kujazilizwa na maoni ya wadau wengine, ni pamoja na somo la maadili kwa ujumla na mafunzo ya dini kwa namna ya pekee, kadhalika Rasimu imependekeza kuwepo kwa mlo mwepesi kwa wanafunzi shuleni ili kuwawezesha Wanafunzi wote kuwa katika hali changamfu wakiwa darasani.

“Lugha ya Kiswahili itaendelea kuwa ya kufundishia katika Elimu ya msingi, lakini rasimu imependekeza lugha ya Kiingereza ifunzwe kwa utaalamu mkubwa ili wanafunzi waijue vema kutokea darasa la kwanza wasipate ugumu katika masomo yao ya Sekondari na Elimu ya juu, lakini pia lugha za kiarabu, kifaransa na kichina kwa kuwa zina matumizi ya kimataifa, kiuhusiano na kimaendeleo duniani hivi sasa,” amesema.

Mapendekezo ya Mitaala kwa darasa la kwanza na la pili ni Kusoma, Kuandika, umahiri katika lugha ya kiingereza, hisabati, kuthamini utamaduni mzuri, Sanaa na michezo na kutunza afya na mazingira.

Masomo kwa darasa la tatu hadi la sita ni Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa, Kichina, Kiarabu, hisabati, historia yaTanzania na maadili, Elimu ya dini, sanaa na Michezo, Sayansi, jiografia na Mazingira.

Kwa Elimu ya Sekondari hatua ya chini, masomo ni Historia ya Tanzania na Maadili, Historia, jiografia, Kiingereza, Fasihi Andishi ya kiingereza, Kiswahili, Kiarabu, Kichina, Kifaransa, Michezo, bailojia, kemia, fizikia, kilimo, Hisabati, Sayansi ya computer na utunzaji wa taarifa za Fedha.

Aidha masomo ya Elimu ya biashara, Ushoni, Sanaa Sanifu, Sanaa za maonesho, Maarifa ya nyumbani, Chakula na Lishe, Elimu ya Dini ya kiislamu, Fasihi ya Kiswahili.

Kwa Elimu ya Sekondari rasimu inapendekeza hatua ya juu ni Historia, jiografia, Elimu ya dini ya Kikristo, Elimu ya dini ya Kiislamu, Kiingereza, Kiarabu, kifaransa, Kichina, fizikia, Kemia, baiolojia, Chakula na Lishe, Sayansi ya Computer, hisabati, hisabati tumizi (Applied mathematics).

Mengine ni Kilimo, historia ya Tanzania, Maadili, Michezo, Sanaa za maonesho, Ushoni, Mawasiliano ya kitaaluma, Elimu ya Biashara, Uhasibu, Uchumi, Fasihi ya Kiswahili na Fasihi ya Kiingereza.

Wanafunzi wa kidato cha kwanza watakaoingia mkondo wa Elimu ya amali na wa Elimu ya njumla, watasoma kwa pamoja masomo matatu ya Elimu ya michezo pamoja na masomo ya jumla yaliyopendekezwa.

Kidato cha pili wanafunzi katika mkondo wa elimu ya Amali watachagua michezo miwili na fani ambazo watazisoma na kubobea hadi kidato cha Nne.

Kuhusiana na lugha ya kufundishi, rasimu imependekeza Kiswahili kiendelee kutumika katika Elimu ya Awali na Msingi isipokuwa katika masomo ya lugha na katika shule zitakazoomba kutumia lugha ya kiingereza kufundishia.

Aidha Lugha ya Kiingereza itatumika kufundishia kuanzia Sekondari ya chini na Elimu ya juu isipokuwa katika somo la Kiswahili.
 
Vipindi vya dini wanafundishwa wahusika na wala hakuna anaelazimishwa....why ambae hahusiki alalamikie??

Kuna shule ilimualika Amber Rutty na wala hukuona mapovu haya...lakini ukisikia kuna vipindi vya dini since sio dini yako makasiriko yanakuwa makubwa why?
 
Mageuzi makubwa
Elimu nchini

. Prof Mkenda asema Rais Samia kuweka Historia

. Lugha Nne kufunzwa, Mkazo maadili, Chakula Shuleni

Na. Mwandishi Wetu

Ikiwa ndiyo injini ambayo nchi inawajengea uwezo wa kiakili na kitaaluma raia wake, mitalaa (mitaala) ya Elimu nchini imefanyiwa maboresho makubwa kuielekeza kwenda kumtoa mhitimu mahiri (competency based) ili nchi ipate wataalamu stahiki kwa maendeleo na ustawi.

Maboresho hayo yamelenga kwenye Elimu na ujuzi (knowledge), nyenzo za utendaji (skills), ubora na tabia njema anayotakiwa kuwa nayo mhitimu huyo kumtofautisha na wanajamii wengine ambako kutamjengea kuheshimika, kujiamini na kuwa tegemeo la jamii katika kujibu changamoto anuai.

Hayo anasema Profesa Adolf Mkenda Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi akiweka hadharani kukamlika kwa rasimu ya mtalaa(mtaala) wa elimu nchini katika kutekeleza maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan juu ya kufanyika kwa mageuzi makubwa ya mfumo wa Elimu nchini.

“Curriculum should therefore, meet the needs of the individual citizens and the Nation. With this principle in mind and in accordance with the Sustainable Development Goals”, anasema Profesa Mkenda akikazia kwamba mtalaa wa Elimu kwa ajili hiyo unapaswa kukidhi mahitajio ya jamii na nchi sawia, hili ndilo zingatio lakini pia katika kufika malengo ya Maendeleo endelevu.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaweka Historia ya kutukuka itakayokumbukwa na vizazi vijavyo na kwamba aliangalia mbali katika kuibua wazo la kuboreshwa mitalaa hivyo wao kama Watendaji na watekelezaji, wamekuja na rasimu yenye kujumuisha mambo kadhaa yendanayo ambayo ni umilisi (fluency) wa lugha nne kuu duniani sanjari Kiswahili kama lugha ya Taifa na ya kufundishia.

“The need for curriculum change is prompted by many factors (hitajio la mageuzi ya mtalaa huibuliwa na sababu nyingi), kwa sisi moja ya sababu hizo, tumelenga kumuwezesha mwanafunzi kuelewa lugha muhimu sanjari kuelewa dhana (concepts) za masomo bila ya kikwazo cha lugha ambacho kilisababisha wanafunzi kukariri badala ya kuelewa masomo hali iliyoleta athari hasi katika utendaji ambapo, kuchangia na upungufu wa kimtaala, alama alizopata Mwanafunzi darasani haziakisi kwenye utendaji wake katika maisha halisi”, amesema Prof Adolf Mkenda.

Aidha mambo mengine yaliyojumuishwa katika rasimu hiyo inayotarajiwa kujazilizwa na maoni ya wadau wengine, ni pamoja na somo la maadili kwa ujumla na mafunzo ya dini kwa namna ya pekee, kadhalika Rasimu imependekeza kuwepo kwa mlo mwepesi kwa wanafunzi shuleni ili kuwawezesha Wanafunzi wote kuwa katika hali changamfu wakiwa darasani.

“Lugha ya Kiswahili itaendelea kuwa ya kufundishia katika Elimu ya msingi, lakini rasimu imependekeza lugha ya Kiingereza ifunzwe kwa utaalamu mkubwa ili wanafunzi waijue vema kutokea darasa la kwanza wasipate ugumu katika masomo yao ya Sekondari na Elimu ya juu, lakini pia lugha za kiarabu, kifaransa na kichina kwa kuwa zina matumizi ya kimataifa, kiuhusiano na kimaendeleo duniani hivi sasa,” amesema.

Mapendekezo ya Mitaala kwa darasa la kwanza na la pili ni Kusoma, Kuandika, umahiri katika lugha ya kiingereza, hisabati, kuthamini utamaduni mzuri, Sanaa na michezo na kutunza afya na mazingira.

Masomo kwa darasa la tatu hadi la sita ni Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa, Kichina, Kiarabu, hisabati, historia yaTanzania na maadili, Elimu ya dini, sanaa na Michezo, Sayansi, jiografia na Mazingira.

Kwa Elimu ya Sekondari hatua ya chini, masomo ni Historia ya Tanzania na Maadili, Historia, jiografia, Kiingereza, Fasihi Andishi ya kiingereza, Kiswahili, Kiarabu, Kichina, Kifaransa, Michezo, bailojia, kemia, fizikia, kilimo, Hisabati, Sayansi ya computer na utunzaji wa taarifa za Fedha.

Aidha masomo ya Elimu ya biashara, Ushoni, Sanaa Sanifu, Sanaa za maonesho, Maarifa ya nyumbani, Chakula na Lishe, Elimu ya Dini ya kiislamu, Fasihi ya Kiswahili.

Kwa Elimu ya Sekondari rasimu inapendekeza hatua ya juu ni Historia, jiografia, Elimu ya dini ya Kikristo, Elimu ya dini ya Kiislamu, Kiingereza, Kiarabu, kifaransa, Kichina, fizikia, Kemia, baiolojia, Chakula na Lishe, Sayansi ya Computer, hisabati, hisabati tumizi (Applied mathematics).

Mengine ni Kilimo, historia ya Tanzania, Maadili, Michezo, Sanaa za maonesho, Ushoni, Mawasiliano ya kitaaluma, Elimu ya Biashara, Uhasibu, Uchumi, Fasihi ya Kiswahili na Fasihi ya Kiingereza.

Wanafunzi wa kidato cha kwanza watakaoingia mkondo wa Elimu ya amali na wa Elimu ya njumla, watasoma kwa pamoja masomo matatu ya Elimu ya michezo pamoja na masomo ya jumla yaliyopendekezwa.

Kidato cha pili wanafunzi katika mkondo wa elimu ya Amali watachagua michezo miwili na fani ambazo watazisoma na kubobea hadi kidato cha Nne.

Kuhusiana na lugha ya kufundishi, rasimu imependekeza Kiswahili kiendelee kutumika katika Elimu ya Awali na Msingi isipokuwa katika masomo ya lugha na katika shule zitakazoomba kutumia lugha ya kiingereza kufundishia.

Aidha Lugha ya Kiingereza itatumika kufundishia kuanzia Sekondari ya chini na Elimu ya juu isipokuwa katika somo la Kiswahili.
Wametumia utaalamu kuficha ujinga huu ila tuko macho hatuwezi kuruhusu ujinga huu
Screenshot_20230511-115523.jpg
 
Mimepitia na kufanya uchambuzi katika Rasimu ya mtaala wa Elimu iliyotangazwa na Waziri wa Elimu inahitaji marekebisho kabla ya kupitishwa rasmi na kuwa mtaala yafaa waondoe kabisa mambo ya dini yanayoweza kusababisha machafuko nakumbuka mwaka 2014 wakati wanakusanya maoni tulipendekeza mambo ya dini yaondolewe lakini sasa wameyarudisha kijanja. Nani yuko nyuma ya dini?

Kuna vitu vingi tulivikataa lakini wanavilazimisha
1. Swala la dini kuingizwa kwenye mtaala hili litaleta malumbano kama sio vurugu, nchi hii haiongozwi kwa misingi ya dini ila watu wake wana dini na wengine hawana ukifuatiria vizuri kwenye Rasimu unaona tayari nchi inaingia mkenge wa dini :Elimu ya biashara wamepachika kitaalamu Elimu ya dini ya Kiislamu sijui wakristo na wasio na dini wamebaki wapi? Sijui mtaala huu wamekopy Zanzibar na kupast Tanganyika? Apo kuna maswali mengi sana bado tunajiuliza hii ligi wanayotaka kuanzisha watafika nayo mwisho?

2.Mtaala huu unakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Thiki"
13.-(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria,
na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa
na kupata haki sawa mbele ya sheria.
(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa
na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano
kuweka sharti lolote ambalo ni la ubaguzi ama wa
dhahiri au kwa taathira yake.

(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na
mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka
Usawa wa
binadamu
Sheria ya
1984
na.15 ib.6
Usawa
mbele ya
Sheria
Sheria
Na.15 ya
1984 ib.6
Sheria
Na.4 ya
1992 ib.8
Sheria ya
2000 na.3
ib.5
Sheria ya
1994 na
7.Fungu la
8[1], [k].

Ukisoma vifungu hivi unaona Waziri anavyoingiza nchi kwenye mgogoro wa kikatiba namimi kutokea apo niko tayari kupinga vifungu hivi mahakamani kuzui Mtaala huu wenye ubaguzi kupishwa tayari nimemwandikia Waziri e-mail nikimkumbusha kwenye maoni tulivyopinga mambo ya dini kuingizwa kwenye mtaala wa Elimu na hii ndiyo sababu kuu iliyomfanya Rais Magufuli kuukataa najua kuna lengo ovu ila tutashughlika nalo kisheria.

2.CHAKULA mashuleni tulisema jukumu la chakula ni jukumu la serikali sio jukumu la wazazi kwakuwa Elimu bure ni pamoja na chakula lakini wao wameliacha hewani bila kuonyesha mwenye wajibu hili tukiliacha hivi litafungua mlango kwa serikali kuwalazimisha wazazi kupeleka chakula shuleni kama ilivyo leo tunataka swala la Elimu libaki mikononi mwa Serikali maana wakati wanaomba kura walinadi elimu bure na hawawezi kulikwepa na kwakuwa sera ya CCM ndiyo inayotekelezwa ni vyema wakahakikisha watoto wetu wanapata chakula shuleni ama watwambie kwamba wameshindwa tufanye maamuzi kama wenye nchi apo nasimama na kifungu hiki

(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na
Serikali itapata madaraka na mamlaka yake
yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa
Katiba hii;
(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi wa
wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;

Niwakumbushe kwamba serikali inawajibika kwa wananchi sio wananchi kuwajibika kwa serikali kama ilivyo sasa.

3.Tulipendekeza elimu ya Ufundi aina zote ifundishwe kuanzia darasa la tatu ili kupata utaalamu wakiwa na uwezo mzuri wa kufundishika na apo ndipo tunaweza kupata matokeo mazuri ya watoto wetu kujua nini wanataka kufanya mbeleni, tutapata mafundi wa vyombobalimbali tutapata wataalamu na mainjinia lakini pia tutaondoa utegemezi wa ajira unaoitesa dunia.
Hujui kuwa Islamic state wako madarakani?
 
Wametumia utaalamu kuficha ujinga huu ila tuko macho hatuwezi kuruhusu ujinga huuView attachment 2617797
Elimu ya dini ya kikiristo umeona!?..au hashua zilikucheza ulipoona elimu ya dini ya kiislam tu!!..taifa linalia watu hawana maadili,wewe hutaki watu wafundishwe dini,watafundishwa na nani!?..elimu ya dini ya kiislam nimeisoma o&a level,haimfundishi mtu kuua wengine,kujitoa muhanga au kusimamisha Dola ya kiislam tz tokana na mgawanyiko wa kijamii,unataka wasifundishwe wakafundishwe madrasa za vichochoroni ambako wanafundishwa kafiri hatakiwi hata kupishwa njia!?..Tanzania Haina dini lakini watu wake Wana dini,watanzania wameamua kutumia rasilimali zao kufundishana dini zao wewe hutaki!?..unaposema hatutaki mambo ya dini,unamsemea nani!?
 
Somo la dini linafundishwa na sio lazima maana hata wanaosoma dini wengine hawajisajili kufanya mitihani...Kwa kawaida uliyaongea yalikuwepo kama dini kitambo mi nilisma dini na nilifanya mtihani wengine walisoma na hawakufanya...

Somo dini sio lazima hakuna ulazima ni sehemu ya maadili maana hata bible knowledge lipo so lilikuwepo na litaendelea kuwepo ikiwa ni mbadala wa somo la maadili .

MAONI YANGU:
1. Serikali ipitie mtaala wa dini juu ya mada za ufundishaji ziwe ambazo wanaona zinafaa kwa sana ili kuwa kama mbadala wa maadili.

2. Somo la dini lile na utaratibu kama wa awali anayetaka kufanya mitahani afanye asiyetaka asifanye.
 
Back
Top Bottom