Uchambuzi: Kwanini Wanu Hafidh Ameir Hakupaswa kuwa Naibu Waziri wa Elimu

Uchambuzi: Kwanini Wanu Hafidh Ameir Hakupaswa kuwa Naibu Waziri wa Elimu

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Katika taifa ambalo linahitaji kufanya maamuzi magumu na sahihi kuhusu mustakabali wake, hakuna eneo nyeti kama elimu. Elimu ni injini, ni mapafu, ni moyo unaosukuma damu ya maendeleo. Taifa lisilo na mfumo madhubuti wa elimu ni sawa na kutembea gizani bila dira.
images (67).jpeg

Ndiyo maana uteuzi wa viongozi wa wizara hii unapaswa kuwa wa makini kupita maamuzi mengine yote ya kisiasa. Lakini uteuzi wa Wanu Hafidh Ameir kuwa Naibu Waziri wa Elimu umeibua maswali mazito—maswali ambayo hatuwezi kuyakwepa kama kweli tunataka kujenga Tanzania inayojitegemea.
1763534918978.jpg

Kwanza kabisa, mjadala huu si wa chuki binafsi, si wa kubeza mtu kama mtu. Ni mjadala wa uwezo, misuli ya kitaaluma, rekodi ya kazi, na uhalisia wa kile ambacho wizara ya elimu inahitaji katika karne hii ya sayansi na teknolojia. Wasifu wa Wanu ni mwepesi sana na hauoneshi uzito unaohitajika kuongoza sekta inayopaswa kubeba ndoto za vijana milioni kadhaa wanaoamini kuwa elimu ndiyo tiketi yao ya kutoka kwenye umasikini na kufika walipo Wachina, Wajapan au hata jirani zetu wanaosonga mbele kwa kasi.
1763534916933.jpg

Uteuzi wake unaonekana kama ishara nyingine kuwa Tanzania bado haijaamua kuwa serious kuhusu elimu. Ni kama tunacheza na maisha ya vizazi vijavyo. Ni kama tunasema: "haituhusu, muda utapita tu, nchi itaendelea tu kupumua kwa mazoea". Lakini ukweli ni kwamba nchi haiendelei kwa mazoea; inaendelea kwa maamuzi sahihi.
images (67).jpeg

Mwaka 1956, miaka zaidi ya 70 iliyopita, Uchina ilifanya uamuzi mkubwa wa kitaifa—kuiweka elimu ya sayansi na teknolojia kuwa kipaumbele cha taifa. Haikuwa nchi tajiri kivile, haikuwa na miundombinu mikubwa, haikuwa na viwanda vya kuvutia. Lakini viongozi wao walijua kuwa maendeleo hayaji kwa bahati, bali kwa kupanda mbegu sahihi—na mbegu hiyo ilikuwa elimu. Leo, tunawaona Wachina wakitamba duniani katika uhandisi, teknolojia, nishati, viwanda, na hata katika uchumi wa kimataifa. Siyo kwa sababu “wamejaliwa”, bali kwa sababu waliamua kuwa serious.
1763534918978.jpg

Tanzania, leo, mwaka 2025, bado tunapamba moto. Bado tunafanya utani na mizaha huku kina Lucas Mwashambwa wakipiga makofi. Na tunaonesha utani huo waziwazi pale tunapowakabidhi wasio na uzito mkubwa majukumu ya kujenga kizazi cha kesho.
1763534916933.jpg

Wizara hii leo inahitaji mtu mwenye dira ya kitaaluma, aliyelelewa katika mazingira ya kitaaluma, aliyeishi na kufikiri kama msomi, aliyeelewa mfumo wa elimu si kihisia, bali kiuchambuzi na kiutafiti. Elimu sio nafasi ya mazoea, sio sehemu ya kujaribia majina mapya, sio sehemu ya kuficha udhaifu wa kisiasa au kulipa fadhila. Kama kuna wizara inayopaswa kuongozwa na watu wenye CV zenye mizizi mikubwa, ni wizara ya elimu.
images (67).jpeg

Lakini CV ya Wanu—pamoja na kwamba inaonesha safari ya kisiasa—haioneshi uwezo, rekodi, au mchango wa kitaalam unaolingana na ukubwa wa jukumu la elimu ya taifa. Hili ndilo linaloumiza wengi. Ni kama tunafanya mzaha na mustakabali wa Taifa.
1763534918978.jpg

Tatizo si kwamba Wanu ni mtoto wa nani au kuwa ni mtoto wa Rais. Tatizo ni kwamba hatuoni uwezo unaolingana na nafasi. Hofu sio kwamba ametoka familia fulani. Hofu ni kwamba CV yake haiakisi mtu anayeweza kubadili mwelekeo wa elimu Tanzania; mtu anayeweza kusimama kwenye majukwaa ya kimataifa na kutetea mageuzi ya elimu; mtu anayeweza kuongoza mjadala wa kitaaluma bila kuyumba; mtu anayeweza kufikiria mbali.
1763534916933.jpg

Hii ndiyo sababu uteuzi wake unawasukuma Watanzania wengi kuamini: labda hatujui tunachotaka kama Taifa.

Je, tuna mpango wa kwenda sambamba na mapinduzi ya AI, Roboti, uchumi wa kidigitali, na ulimwengu wa sayansi?

Je, tunataka kuwa sehemu ya mataifa yanayounda teknolojia au tunataka kubaki mashabiki wa teknolojia ya wengine?

Haiwezekani tukafikia hayo ikiwa tunawapa watu wasio na rekodi za kitaaluma nafasi ya kusimamia sekta muhimu kama elimu.
images (67).jpeg

China ilipiga hatua kwa sababu walijua wanachotaka. Walisema: “Elimu kwanza.”
Tanzania leo inasema nini?
Kwa uteuzi kama huu, inaonekana tunaendelea kusema: “Tutakuja baadaye. Kwa sasa tusubiri bahati.”

Lakini dunia ya leo haina nafasi kwa nchi za kusubiri bahati. Bahati wanayo watu serious.

Na kama hatutaamua leo, basi tutaendelea tu kuwa watazamaji—wabeba uchungu—mashabiki wa mafanikio ya wengine.
1763534918978.jpg

Kwa kifupi, uteuzi wa Wanu Hafidh Ameir kama Naibu Waziri wa Elimu sio tu kosa la kimkakati, bali ni dalili ya ugonjwa mkubwa: kukosa dira, kukosa uamuzi mgumu, na kukosa seriousness katika eneo ambalo ndilo ufunguo wa maendeleo ya nchi.

Kama taifa, tunastahili zaidi. Na watoto wetu wanastahili zaidi. Mama ni Rais, Mtoto ni waziri na Mkwe ni waziri bado Baba naye atapewa uwaziri mwisho wa siku bunge lote linakuwa ni ukoo.
 
Katika taifa ambalo linahitaji kufanya maamuzi magumu na sahihi kuhusu mustakabali wake, hakuna eneo nyeti kama elimu. Elimu ni injini, ni mapafu, ni moyo unaosukuma damu ya maendeleo. Taifa lisilo na mfumo madhubuti wa elimu ni sawa na kutembea gizani bila dira.
View attachment 3504089
Ndiyo maana uteuzi wa viongozi wa wizara hii unapaswa kuwa wa makini kupita maamuzi mengine yote ya kisiasa. Lakini uteuzi wa Wanu Hafidh Ameir kuwa Naibu Waziri wa Elimu umeibua maswali mazito—maswali ambayo hatuwezi kuyakwepa kama kweli tunataka kujenga Tanzania inayojitegemea.
View attachment 3504090
Kwanza kabisa, mjadala huu si wa chuki binafsi, si wa kubeza mtu kama mtu. Ni mjadala wa uwezo, misuli ya kitaaluma, rekodi ya kazi, na uhalisia wa kile ambacho wizara ya elimu inahitaji katika karne hii ya sayansi na teknolojia. Wasifu wa Wanu ni mwepesi sana na hauoneshi uzito unaohitajika kuongoza sekta inayopaswa kubeba ndoto za vijana milioni kadhaa wanaoamini kuwa elimu ndiyo tiketi yao ya kutoka kwenye umasikini na kufika walipo Wachina, Wajapan au hata jirani zetu wanaosonga mbele kwa kasi.
View attachment 3504091
Uteuzi wake unaonekana kama ishara nyingine kuwa Tanzania bado haijaamua kuwa serious kuhusu elimu. Ni kama tunacheza na maisha ya vizazi vijavyo. Ni kama tunasema: "haituhusu, muda utapita tu, nchi itaendelea tu kupumua kwa mazoea". Lakini ukweli ni kwamba nchi haiendelei kwa mazoea; inaendelea kwa maamuzi sahihi.
View attachment 3504089
Mwaka 1956, miaka zaidi ya 70 iliyopita, Uchina ilifanya uamuzi mkubwa wa kitaifa—kuiweka elimu ya sayansi na teknolojia kuwa kipaumbele cha taifa. Haikuwa nchi tajiri kivile, haikuwa na miundombinu mikubwa, haikuwa na viwanda vya kuvutia. Lakini viongozi wao walijua kuwa maendeleo hayaji kwa bahati, bali kwa kupanda mbegu sahihi—na mbegu hiyo ilikuwa elimu. Leo, tunawaona Wachina wakitamba duniani katika uhandisi, teknolojia, nishati, viwanda, na hata katika uchumi wa kimataifa. Siyo kwa sababu “wamejaliwa”, bali kwa sababu waliamua kuwa serious.
View attachment 3504090
Tanzania, leo, mwaka 2025, bado tunapamba moto. Bado tunafanya utani na mizaha huku kina Lucas Mwashambwa wakipiga makofi. Na tunaonesha utani huo waziwazi pale tunapowakabidhi wasio na uzito mkubwa majukumu ya kujenga kizazi cha kesho.
View attachment 3504091
Wizara hii leo inahitaji mtu mwenye dira ya kitaaluma, aliyelelewa katika mazingira ya kitaaluma, aliyeishi na kufikiri kama msomi, aliyeelewa mfumo wa elimu si kihisia, bali kiuchambuzi na kiutafiti. Elimu sio nafasi ya mazoea, sio sehemu ya kujaribia majina mapya, sio sehemu ya kuficha udhaifu wa kisiasa au kulipa fadhila. Kama kuna wizara inayopaswa kuongozwa na watu wenye CV zenye mizizi mikubwa, ni wizara ya elimu.
View attachment 3504089
Lakini CV ya Wanu—pamoja na kwamba inaonesha safari ya kisiasa—haioneshi uwezo, rekodi, au mchango wa kitaalam unaolingana na ukubwa wa jukumu la elimu ya taifa. Hili ndilo linaloumiza wengi. Ni kama tunafanya mzaha na mustakabali wa Taifa.
View attachment 3504090
Tatizo si kwamba Wanu ni mtoto wa nani au kuwa ni mtoto wa Rais. Tatizo ni kwamba hatuoni uwezo unaolingana na nafasi. Hofu sio kwamba ametoka familia fulani. Hofu ni kwamba CV yake haiakisi mtu anayeweza kubadili mwelekeo wa elimu Tanzania; mtu anayeweza kusimama kwenye majukwaa ya kimataifa na kutetea mageuzi ya elimu; mtu anayeweza kuongoza mjadala wa kitaaluma bila kuyumba; mtu anayeweza kufikiria mbali.
View attachment 3504091
Hii ndiyo sababu uteuzi wake unawasukuma Watanzania wengi kuamini: labda hatujui tunachotaka kama Taifa.

Je, tuna mpango wa kwenda sambamba na mapinduzi ya AI, Roboti, uchumi wa kidigitali, na ulimwengu wa sayansi?

Je, tunataka kuwa sehemu ya mataifa yanayounda teknolojia au tunataka kubaki mashabiki wa teknolojia ya wengine?

Haiwezekani tukafikia hayo ikiwa tunawapa watu wasio na rekodi za kitaaluma nafasi ya kusimamia sekta muhimu kama elimu.
View attachment 3504089
China ilipiga hatua kwa sababu walijua wanachotaka. Walisema: “Elimu kwanza.”
Tanzania leo inasema nini?
Kwa uteuzi kama huu, inaonekana tunaendelea kusema: “Tutakuja baadaye. Kwa sasa tusubiri bahati.”

Lakini dunia ya leo haina nafasi kwa nchi za kusubiri bahati. Bahati wanayo watu serious.

Na kama hatutaamua leo, basi tutaendelea tu kuwa watazamaji—wabeba uchungu—mashabiki wa mafanikio ya wengine.
View attachment 3504090
Kwa kifupi, uteuzi wa Wanu Hafidh Ameir kama Naibu Waziri wa Elimu sio tu kosa la kimkakati, bali ni dalili ya ugonjwa mkubwa: kukosa dira, kukosa uamuzi mgumu, na kukosa seriousness katika eneo ambalo ndilo ufunguo wa maendeleo ya nchi.

Kama taifa, tunastahili zaidi. Na watoto wetu wanastahili zaidi. Mama ni Rais, Mtoto ni waziri na Mkwe ni waziri bado Baba naye atapewa uwaziri mwisho wa siku bunge lote linakuwa ni ukoo.
Nimesoma yote ila umeshindw a kuonyesha kwamba hana uwezo na kuonyesha udhaifu wake, kua mtoto wa Raisi sio kosa au kutokua na uwezo fanya analysis nzima ya kabinenti ya CCM uonyesha kama wako tofauti sana na huyu wanu, wote ni wale wale Makonda ana elumu gani? Ummy mualimu kupewa afya zamani alikua na uwezo gani wengi tu, tafuta hoja zingine ila sio za uwezo kabisa.
 
Tanzania haijawai kuwa serious kwenye swala la elimu.

Tumevipa kipaumbele vitu vya kipumbavu kuliko elimu.

Zamani watu waliofeli ndio waliokuwa wanaenda kusomea ualimu.

Sasa kiongozi mwenye akili yako timamu unakubali vipi mtu aliyefeli akasome ualimu?

Sio hivyo anagalia mishahara wanayolipwa walimu na wabunge.

Hapo utapata picha ni kwa jinsi gani hatuko serious na elimu yetu.

Tungekuwa serious na elimu yetu mtu kama mama samia hakupaswa hata kuwa diwani achilia mbali rais.


CCM wanaiharibu sana hii nchi kwa kuendekeza ubinafsi.
 
Nitajikita hapo mwishoni ulivomaliza...MAMA RAIS, MTOTO WAZIRI, MKWE WAZIRI! tumefika mbali sana kama nchi,.hawaoni hata soni daaa!
 
Kiukweli wamekosea sana kumpa wizara hiyo.Bora hata angempa wizara ya muungano au ya sanaa akadundike taarabu huko na siyo hiyo wizara waliyompa.wizara ya elimu inahitaji wenye elimu ambayo siyo ya kuungaunga kama kamba ya katani.Huyu bibi atengue uteuzi huo.
 
Back
Top Bottom