Marando anasema ataongoza kwa ufanisi na kutegemea taaluma, kwa kutumia sheria sababu yeye ni mwanasheria.
Anaahidi kulinda sheria na katiba na kuwapa wabunge uhuru wa kujieleza
nimeamini sasa hawa wabunge wa kuteuliwa wa CCM kweli wanakibeba.....wanashangilia swali aliloulizwa la kutafsiri sheria....naona Marando anajibu kiufasaha kabisa...kwamba spika alishawahi 'kutoa hukumu'
swali kwa Nyaucho: Marando anaulizwa atatafsirishe sheria wakati huo ni kazi ya Mahakama?
Marando anakumbushia msekwa alivyotafsiri sheria wakati huo, kwa hiyo yeye anachosema ni sahihi
Kuna swali linaulizwa na kijana mmoja sijuindo nani kwamba Marando ni mkali............naona limetokea zogo hapa ni kama vile hili swali lilipangwa.....kuna Swali aliulizawa Makinda Anna akalichakachua kwamba mambo yaliyopita yasiletwe hapa ....lakini naona hili ameliruhusu...yale yale...
Baada ya nusu saa hivi kuanzia sasa, kikao cha uteuzi wa spika mpya kitaanza hapo Dodoma yeyote mwenye la kuchangia hii thread ndiyo mahali pake..............nitajitahidi kuwaletea dondoo za matukio muhimu kutoka huko Dodoma.......................na kila mmoja ajaribu kufanya hivyo kuwapasha habari wale ambao hawataweza kuona tukio hili muhimu moja kwa moja..................
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.