Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,700
- 1,857
Nakumbuka, nilishabikia sana uchaguzi wa Marekani uliopita. Nilikuwa nalala usiku wa manane kufuatilia maendeleo ya kijana wetu, Barak Obama. Ila hivi sasa sitaki kusikia hata jina lake. Huyu jamaa- kama Mk...re- amewakatisha tamaa sana watu waliokuwa wakimsapoti. Sijui hakufahamu kuwa watu wengi walimwunga mkono kwa sababu ya kutarajia hataendeleza au kuanzisha vita duniani. Yote hayo yamekuwa matarajio hewa, hasa wakati huu mazungumzo ya kuishambulia Iran yakikoa moto.
Kwa upande wa pili, ameshindwa kabisa kugeuza dira ya Marekani, na kwa kweli haidhuru ameukuta uchumi wa Marekani katika hali mbaya, si makosa kusema yeye ameongezea kudidimia kwake.
Akichaguliwa tena, si tu kwamba twaweza kushuhudia vita ya III ya dunia, bali Marekani itakoma kuwa kiongozi wa kiuchumi duniani. Itabaki kuwa dola kubwa kwa miaka 10-15 ijayo kwa sababu tu ina silaha kali, kama vile ilivyokuwa Soviet Union, lakini si kwa kitu kingine.
Laiti kama Uchina ingekuwa na idadi ndogo ya watu, basi ingeipiku Marekani kwa pato la mtu na hata la taifa kwa muda mfupi sana.
Kwa vile nilikuwa nikimsapoti kwa kutarajia atatoa picha nzuri ya watu weusi, na angalau atawasaidia watu weusi wa nchini kwake ambao wanazidi kunyanyaswa na kuonewa (Zaidi ya Wamarekani milioni 2 wako jela, wengi wakiwa weusi), na kwa vile hakufanya lolote .......mimi naona RON PAUL ndiye kiongotzi mwenye dira nzuri ya kuikwamua Marekani kutokana na matatizo yake. Ni dhahiri kuwa bajeti ya Ulinzi, security nk na misaada isiyo mpaka kwa Israel (political, financial and military) ndiyo mambo mawili makubwa yanayoikausha (draining) Marekani. RON PAUL anaahidi kuondoa vituo vyote vya Majeshi ya Marekani nje ya nchi (takriban 180) na ku deal na Israel kama nchi nyinginezo duniani, ingawaje ataisapoti katika kuilinda. Aidha, hataanzisha vita nyingine isipokuwa kama nchi ya Marekani itashambuliwa.
Naona huyu ndiye anayetufaa kwa amani ya dunia, na pia kwa uchumi wa Marekani. Kwani kutetereka kwa uchumi wa Marekani kunatudhuru sote.
Kwa upande wa pili, ameshindwa kabisa kugeuza dira ya Marekani, na kwa kweli haidhuru ameukuta uchumi wa Marekani katika hali mbaya, si makosa kusema yeye ameongezea kudidimia kwake.
Akichaguliwa tena, si tu kwamba twaweza kushuhudia vita ya III ya dunia, bali Marekani itakoma kuwa kiongozi wa kiuchumi duniani. Itabaki kuwa dola kubwa kwa miaka 10-15 ijayo kwa sababu tu ina silaha kali, kama vile ilivyokuwa Soviet Union, lakini si kwa kitu kingine.
Laiti kama Uchina ingekuwa na idadi ndogo ya watu, basi ingeipiku Marekani kwa pato la mtu na hata la taifa kwa muda mfupi sana.
Kwa vile nilikuwa nikimsapoti kwa kutarajia atatoa picha nzuri ya watu weusi, na angalau atawasaidia watu weusi wa nchini kwake ambao wanazidi kunyanyaswa na kuonewa (Zaidi ya Wamarekani milioni 2 wako jela, wengi wakiwa weusi), na kwa vile hakufanya lolote .......mimi naona RON PAUL ndiye kiongotzi mwenye dira nzuri ya kuikwamua Marekani kutokana na matatizo yake. Ni dhahiri kuwa bajeti ya Ulinzi, security nk na misaada isiyo mpaka kwa Israel (political, financial and military) ndiyo mambo mawili makubwa yanayoikausha (draining) Marekani. RON PAUL anaahidi kuondoa vituo vyote vya Majeshi ya Marekani nje ya nchi (takriban 180) na ku deal na Israel kama nchi nyinginezo duniani, ingawaje ataisapoti katika kuilinda. Aidha, hataanzisha vita nyingine isipokuwa kama nchi ya Marekani itashambuliwa.
Naona huyu ndiye anayetufaa kwa amani ya dunia, na pia kwa uchumi wa Marekani. Kwani kutetereka kwa uchumi wa Marekani kunatudhuru sote.