Uchaguzi Mkuu kusimamishwa?

[FONT=ArialMT, sans-serif]Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amewaandikia barua maprofesa wawili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), akiwaomba wawe marafiki wa mahakama katika usikilizwaji wa rufaa ya mgombea binafsi itakayosikilizwa na Mahakama ya Rufaa Aprili 8, mwaka huu.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Maprofesa hao, ambao ni wanasheria kitaaluma na wahadhiri waandamizi, ni Jwan Mwaikusa na Palamagamba Kabudi, ambaye ni Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha UDSM.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika barua yake ya Machi 3, mwaka huu, Jaji Mkuu amewaomba maprofesa hao kuwa marafiki wa mahakama na wajielekeze katika hoja zao kama mahakama inaweza kutamka kifungu gani cha katiba kinakwenda kinyume cha Katiba.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha, Aprili 8, mwaka huu, Profesa Mwaikusa na Kabudi watachangia hoja kuhusu shauri hilo, litakaposikilizwa na Mahakama ya Rufani, mbele ya jopo la majaji saba linaloongozwa na Jaji Mkuu.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mahakama hiyo inatarajia kusikiliza rufaa ya serikali dhidi ya uamuzi uliotolewa na waliokuwa majaji wa Mahakama Kuu; aliyekuwa Jaji Kiongozi, Amir Manento, Salum Massati (sasa Jaji wa Mahakama ya Rufaa) na Thomas Mihayo (Mstaafu).[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Majaji hao katika hukumu yao, walikubaliana na hoja zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Democrat (DP), Mchungaji Christopher Mtikila za kuwapo mgombea binafsi katika uchaguzi wa siasa nchini.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Jopo la majaji saba wa Mahakama ya Rufaa, wakiongozwa na Jaji Mkuu, linawajumuisha Jaji Eusebia Munuo, Januari Msofe, Nathalia Kimaro, Mbarouk Salim, Dk. Stephen Bwana na Benard Ruanda, watasikiliza rufaa hiyo.[/FONT]
 
Rufaa ya mgombea binafsi ngoma nzito

Na Hellen Mwango
9th March 2010

headline_bullet.jpg
Jaji Mkuu awaalika maprofesa wawili

headline_bullet.jpg
Awaomba wawe marafiki wa mahakama


Jaji%20Mkuu(5).jpg

Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan.

[FONT=ArialMT, sans-serif]Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amewaandikia barua maprofesa wawili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), akiwaomba wawe marafiki wa mahakama katika usikilizwaji wa rufaa ya mgombea binafsi itakayosikilizwa na Mahakama ya Rufaa Aprili 8, mwaka huu.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Maprofesa hao, ambao ni wanasheria kitaaluma na wahadhiri waandamizi, ni Jwan Mwaikusa na Palamagamba Kabudi, ambaye ni Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha UDSM.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika barua yake ya Machi 3, mwaka huu, Jaji Mkuu amewaomba maprofesa hao kuwa marafiki wa mahakama na wajielekeze katika hoja zao kama mahakama inaweza kutamka kifungu gani cha katiba kinakwenda kinyume cha Katiba.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha, Aprili 8, mwaka huu, Profesa Mwaikusa na Kabudi watachangia hoja kuhusu shauri hilo, litakaposikilizwa na Mahakama ya Rufani, mbele ya jopo la majaji saba linaloongozwa na Jaji Mkuu.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mahakama hiyo inatarajia kusikiliza rufaa ya serikali dhidi ya uamuzi uliotolewa na waliokuwa majaji wa Mahakama Kuu; aliyekuwa Jaji Kiongozi, Amir Manento, Salum Massati (sasa Jaji wa Mahakama ya Rufaa) na Thomas Mihayo (Mstaafu).[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Majaji hao katika hukumu yao, walikubaliana na hoja zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Democrat (DP), Mchungaji Christopher Mtikila za kuwapo mgombea binafsi katika uchaguzi wa siasa nchini.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Jopo la majaji saba wa Mahakama ya Rufaa, wakiongozwa na Jaji Mkuu, linawajumuisha Jaji Eusebia Munuo, Januari Msofe, Nathalia Kimaro, Mbarouk Salim, Dk. Stephen Bwana na Benard Ruanda, watasikiliza rufaa hiyo.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika rufaa yake namba 45 ya mwaka jana, serikali imetoa sababu sita za kukata rufaa hiyo zikiwemo, Mahakama Kuu ilikosea kujipa mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo; ilikosea kutengua vifungu vya Katiba ya nchi; na ilikosea kisheria kwa kupunguza matakwa ya lazima ya Ibara 30 (5) na 13 (2) ya Katiba ya nchi.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Sababu nyingine ni kujipachika mamlaka ya kibunge ya kutunga sheria; kukosea kisheria kwa kuiweka Katiba ya nchi katika vyombo vya kimataifa; na pia ilikosea kuitolea maamuzi kesi hiyo bila kuweka suala hilo bayana.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mara ya kwanza serikali ilikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu, katika Mahakama ya Rufaa mwaka 2007, ambapo ilidai mahakama hiyo ya chini ilikosea kisheria kutafsiri Ibara ya 21(1) (c), 39 (1) (c) (b) na 69 (1) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Hata hivyo, rufaa hiyo ilitupiliwa mbali na Mahakama ya Rufaa baada ya kukubaliana na ombi la wakili wa Mtikila, Richard Rweyongeza, kwamba rufaa hiyo haina msingi na kwamba imejaa dosari za kisheria.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Awali, katika hukumu ya Mahakama Kuu iliyotolewa Mei 2006, iliruhusu kuwapo kwa mgombea binafsi katika uchaguzi, kwa sababu Katiba ya nchi inatoa haki hiyo. [/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mahakama Kuu ilibainisha kuwa katiba inatamka wazi kuwa, kila mwananchi ana haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi na haiweki masharti kuwa hilo lifanyike kwa mtu kujiunga na chama fulani. [/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Hii ilikuwa mara ya pili kwa Mtikila kupigania mgombe binafsi mahakamani, mwaka 1993 alishinda kesi kama hiyo katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, lakini licha ya uamuzi huo wa mahakama, Bunge lilishindwa kutunga sheria ya kuruhusu mgombea binafsi, hivyo alifungua kesi hiyo ya Kikatiba Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam ambako alishinda tena. [/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Rufaa hiyo ya serikali ilitajwa Februari 8 na iliahirishwa hadi Aprili 8, mwaka huu, kwa ajili ya kusikilizwa.[/FONT]

CHANZO: NIPASHE
 
Mahakama Kuu ilibainisha kuwa katiba inatamka wazi kuwa, kila mwananchi ana haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi na haiweki masharti kuwa hilo lifanyike kwa mtu kujiunga na chama fulani.

Ni kwa nini serikali ya CCM inawaogopa wagombea binafsi?
 
Kweli ngoma nzito. Sasa hawa marafiki wa mahakama ushauri/hoja zao zina uzito gani katika maamuzi ya mahakama?

Je marafiki hawa watakuwa independent (with a 'chinese wall' between them) au wanaweza kushirikiana ili kuwa na wazo moja? Kama watakuwa independent ndhani idadi yao ingekuwa odd number (mfano tatu, tano, etc) ili ilete maana zaidi.
 
Hii ilikuwa mara ya pili kwa Mtikila kupigania mgombe binafsi mahakamani, mwaka 1993 alishinda kesi kama hiyo katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, lakini licha ya uamuzi huo wa mahakama, Bunge lilishindwa kutunga sheria ya kuruhusu mgombea binafsi, hivyo alifungua kesi hiyo ya Kikatiba Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam ambako alishinda tena.


hakika ipo siku hawa CCM watatambua haki yangu ya kupiga kura na kupigiwa kura, ipo siku Mtikila atakumbukwa na kwa hili pia.
 
Kweli ngoma nzito. Sasa hawa marafiki wa mahakama ushauri/hoja zao zina uzito gani katika maamuzi ya mahakama?

Je marafiki hawa watakuwa independent (with a 'chinese wall' between them) au wanaweza kushirikiana ili kuwa na wazo moja? Kama watakuwa independent ndhani idadi yao ingekuwa odd number (mfano tatu, tano, etc) ili ilete maana zaidi.

Marafiki wa mahakama(amicus curiae)hawanana cha kupoteza katika hili,wao ni wasikilizaji tu na watoa maoni na wala hawapo upande wowote.Mawazo yao yaweza kuchukuliwa na kutiliwa maanani,lakini hayana nguvu yoyote kisheria.Kazi iko kwa wingi wa majaji, pale itakaotokea wakashindwa kuelewana(with dissenting opinions).
 
Mzee Marmo amekuwa jasiri sana kwa kuamua kupinga wagombea binafsi hadharani. Amenikumbusha hadithi ya mtu yule aliyekuwa anatengeneza kipupwe ndani ya kikombe.
 
Ni kwa nini serikali ya CCM inawaogopa wagombea binafsi?

Kwa sababu Itapoteza udhibiti wa bunge na haitakuwa na uwezo wa kunyamazisha wabunge wake kwa vitisho kuwa watanyanganywa kadi ya ccm na kupoteza ubunge.

Hata kama mbunge atafukuzwa katika chama ataendelea kuwa mbunge kwani haitalazimu mbunge kuwa mwanachama wa chama cha siasa
 
Kazi iko kwa wingi wa majaji, pale itakaotokea wakashindwa kuelewana(with dissenting opinions).

Ni mara chache sana nimeona hukumu za Mahakama za Juu (HC & CA) zenye dissenting opinions! Kwa maana hiyo huwa wanakubaliana zaidi kuliko kupingana!
 
Marafiki wa mahakama(amicus curiae)hawanana cha kupoteza katika hili,wao ni wasikilizaji tu na watoa maoni na wala hawapo upande wowote.Mawazo yao yaweza kuchukuliwa na kutiliwa maanani,lakini hayana nguvu yoyote kisheria.Kazi iko kwa wingi wa majaji, pale itakaotokea wakashindwa kuelewana(with dissenting opinions).

Asante Mayenga kwa ufafanuzi murua.
 
Huyu mwandishi wa NIPASHE amechemsha kutaja baadhi ya vifungu. Vifungu alivyovitaja kwa kuvikosea nimeviweka IN RED:
Mara ya kwanza serikali ilikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu, katika Mahakama ya Rufaa mwaka 2007, ambapo ilidai mahakama hiyo ya chini ilikosea kisheria kutafsiri Ibara ya 21(1) (c), 39 (1) (c) (b) na 69 (1) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Sehemu ya Hukumu ya Mahakama Kuu inasomeka kama nilivyoquote hapa chini (Vifungu sahihi nimeviweka tena in red):

We are of the settled view that the amendments to Articles 21(1) Article 39(1)c) and Article 67(1)(b) introduced by Act No. 34 of 1994 or popularly known as the 11th Amendment are unnecessary and unreasonable restrictions to the fundamental right of the citizens of Tanzania to run for the relevant elective posts either as party members or as private candidates.
 
Sijui hapa tuatazuia vipi mawazo ya kifisadi kwenye kuchangia hiyo hoja
Pia jaji mkuu amejitahidi sana,angalao amejaribu kutafuta nguvu ya maooni na kutanua wigo wake.

Lakini najua kuna uwezekano mkubwa serikali itabwagwaa hapa
 
Lakini najua kuna uwezekano mkubwa serikali itabwagwaa hapa

Mahakama zetu hazitabiriki ndugu yangu, unaweza kushangaa hukumu itakavyotoka iko tofauti na "public opinion!" Rejea hukumu ya kesi ya Zombe! Let's wait n c!
 
hivi kwa nini mgombea binafsi anaogopwa? kwa kupinga hili selikali haioni kama inavunja haki za raia wake? "one will remain one even if it will be broken it will smell one"
 
Back
Top Bottom