Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,989
Tume ya taifa ya uchaguzi (nec) imetangaza uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 14 tanzania bara utakazofanyika julai 13, mwaka huu.
Kuwepo kwa uchaguzi huo kumetangazwa leo juni 14, 2023 jijini dodoma na mkurugenzi wa nec, ramadhani kailima ambaye ameeleza kuwa unafanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa.
Kwa mujibu wa taratibu, tume kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 13 (3) cha sheria ya uchaguzi ya serikali za mitaa, sura ya 292, inatoa taarifa kwa umma kuhusu uwepo wa uchaguzi huo wa madiwani katika kata 14 za tanzania bara, amesema kailima.
Kuwepo kwa uchaguzi huo kumetangazwa leo juni 14, 2023 jijini dodoma na mkurugenzi wa nec, ramadhani kailima ambaye ameeleza kuwa unafanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa.
Kwa mujibu wa taratibu, tume kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 13 (3) cha sheria ya uchaguzi ya serikali za mitaa, sura ya 292, inatoa taarifa kwa umma kuhusu uwepo wa uchaguzi huo wa madiwani katika kata 14 za tanzania bara, amesema kailima.