Uchaguzi CUF: Prof. Lipumba ambwaga Prof. Safari

Safari na Lipumba wote ni wasomi wazuri ila sasa Lipumba sidhani kama ana jipya linaloweza kukisaidia chama chake; nilitegemea wakati wa uchaguzi wa Tarime angeonesha leadership qualities kwa kushauri chama chake kutosimamisha mgombea na kuunga mkona Chadema hakufanya hivyo!! Safari on the other hand anaweza kufanikiwa kupata wafuasi wengi wa dini ya kiislam kwasababu ya itikadi yake; he is a hardliner oppositionist kwahiyo anaweza kukaa na Chadema wakaweka mikakati imara!!
Bulesi tusaidie CUF walisimamisha Mgombea gani kule Tarime...?au waliside na Chama gani...?Vp Kiteto nako walishirikiana na nani?

kama Chadema mmekataa ushirikiano hapo Mbeya on baseless points...usilete hoja mfu....!!!

naona nchi hii tumeshajichagulia watu wa kutuongoza...Uwe Muongo!!! msanii na sifa zingine...ila ukiwa safi hufai
 
Mkuu Chuma,
Mwanachama wa CUF aligombea udiwani,lakini chama chake hakikumpigia campaign.Chama ngazi ya wilaya waliamua kusaidia CHADEMA na makao makuu wakaafiki msimamo wao.Yule mgombea aliambulia nafasi ya tatu kwa utashi wake binafsi.
 
mwenye profile ya huyu profesa tunaiomba please!!!! mimi ninachojua ni profesa wa sheria na wakili hapa mjini kingine sijui
 
Siku kama 2 zilizopita nilimsikia Profesa huyu akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.Katika mahojiano hayo Profesa SAFARI alitangaza nia yake ya kutaka kugombea Uenyekiti wa Taifa Chama cha Wananchi(CUF)..Katika maelezo yake alisema kwamba lengo hasa la kugombe ni kutaka kurudisha uhai wa CUF ambacho(kwa mujibu wa maelezo yake) ni kama kimepoteza umaarufu na kwamba kinahitaji mabadiliko ya uongozi ngazi ya Taifa kwani uongozi wa sasa umekaa muda mrefu na haujaleta mabadiliko yoyote(alizungumzia suala la CUF kutokuwa na mbunge hata mmoja wa kuchaguliwa kutoka Tanzania bara),pia alizungumzia suala la mikutano ya CUF kutokuwa na mahudhurio ya kuridhisha kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo alisema kwamba sasa hivi mpaka wanachama waambiwe kuwa kutakuwa na Pilau ndio mahudhurio kidogo yanakuwa ya kuridhisha...Binafsi namfahamu Profesa SAFARI kama Mwanasheria maarufu na mtaalamu mahiri wa Lugha yetu adhimu ya Kiswahili...Swali,,Je kwa wanaomfahamu Profesa huyu,ana uzoefu gani katika mambo ya kisiasa???,anaweza kuvaa viatu vya Profesa Lipumba???,hivi uchaguzi mkuu wa CUF unafanyika lini???....Mkuu Mzee Mwanakijiji ninaomba kama inawezekana ufanye mahojiano na Profesa huyu na kuyaweka hapa maana kwa jinsi nilivyomsikia ana uchungu sana na jinsi CUF ilivyopoteza umaarufu(kwa mtizamo wake)..Naomba kuwasilisha wakuu...Mbarikiwe sana

Hivi kilichomtimua kazi kule Chuo cha Diplomasia ni nini? Si kwa sababu alipeleka gari lenye namba za kidiplomasia kwenye mkutano wa wa CUF?
Mkuu Balantanda niwie radhi kwa kuongeza maswali badala ya majibu
 
Hivi kilichomtimua kazi kule Chuo cha Diplomasia ni nini? Si kwa sababu alipeleka gari lenye namba za kidiplomasia kwenye mkutano wa wa CUF?
Mkuu Balantanda niwie radhi kwa kuongeza maswali badala ya majibu

Nimekusoma Mwalimu,kimsingi hata mimi simjfahamu sana Profesa Safari(zaidi ya kufahamu kwamba ni mwanasheria na pia mchangiaji wa vipindi vya redio na luninga vinavyohusiana na Lugha yetu adhimu ya Kiswahili),ndo maana nikawaomba wanajamii humu ndani kama wanamfahamu watujuze Profesa huyu ni mtu wa aina gani hasa...Ubarikiwe sana Mwalimu Zawadi
 
It looks to me walau huko CUF kuna demokrasia ya kweli nafasi mpaka ya Mwenyekiti inapiganiwa kwa uwazi na watu wa hadhi.

I hope Chadema and CCM will take a leaf...
 
Mtarajiwa,
Yaani Lipumba ashindwe CUF, ajiunge na CHADEMA ndipo upinzani unoge? Akishindwa huko CUF, CHADEMA ndiko ataweza? Kama matarajio yetu ni kunogesha upinzani kwa njia hiyo tumepotea. Nadhani CUF kuna tatizo la kimfumo ambapo mwenyekiti anakuwa na cheo kama ceremonial wakati the real power ni katibu mkuu. If this is not changed watamaliza maprofesa wote with minimal gains hasa bara.

CUF huku bara ni very artificial, support base yake hasa ni ya waswahili, iliterates na baadhi ya vijana wenye jazba kutokana na kutambua kuwa uduni wao unatokana na sera mbaya za chama tawala. Bahati mbaya wameweza kupenetrate kwenye sehemu ndogo sana bara, lakini ZNZ ni hadithi nyingine. CUF ZNZ iko very organised, inaweza kuchukua na kutawala dola effectiveky hata in half hour notice. Kitu ambacho huku bara bado hakipo.
Profesa Lipumba nni mtu mwenye personality inayostahili kwa chama kikubwa kama CUF. Lakini sio profesa Safari, Profesa Safari anatakiwa aanzishe chama cha shari na atangaze itikadi zake zote for sure atapata wafuasi, lakini kama CUF wakitaka wabomoe mafanikio kidogo waliyoyapata bara basi wamchague Safari kuwa mwenyekiti.
 
CUF njia panda uchaguzi Tarime

2008-09-26 09:14:05
Na Muhibu Said
Hatua ya vyama vya Chadema na NCCR-Mageuzi kusimamisha wagombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, mkoani Mara, imekiweka Chama cha Wananchi (CUF) njiapanda, baada ya makao makuu ya chama hicho hadi sasa kushindwa kuamua mgombea wa chama kipi kati ya vyama hivyo `wampigie debe`.

Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na TLP, ni vyama vilivyoamua kuunda ushirikiano wa kisiasa katika kambi ya upinzani na miongoni mwa makubaliano waliyofikia katika ushirikiano huo, ni pamoja na kushirikiana katika chaguzi kwa lengo la kukishinda katika uchaguzi na kuking`oa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Wilfred Lwakatare aliliambia Nipashe ofisini kwake jijini Dar es Salaam juzi kuwa, hadi sasa makao makuu ya chama hicho, hawajafikia uamuzi wa mgombea wa chama kipi wamuunge mkono katika uchaguzi kwa madai kwamba suala hilo linahitaji busara kabla ya kuamua.

``Sisi baada ya kuona uwezo wetu ni mdogo wa kushinda jimboni humo, tuliamua kumwondoa mgombea wetu. Wenzetu NCCR na Chadema wamesimamisha wagombea. Mgombea wa chama kipi kati ya hivyo tuelekeze nguvu zetu, suala hilo linahitaji busara ya hali juu kuamua,`` alisema Lwakatare.

Hata hivyo, alisema watafikia uamuzi wa mgombea wa chama kipi wampigie debe, mara tu watakapopata taarifa kutoka kwa uongozi wa CUF Tarime kutokana na upepo wa kisiasa katika kinyang`anyiro cha uchaguzi huo utakavyokuwa ukienda.

``Tutakapopata taarifa kutoka uongozi wa CUF Wilaya ya Tarime, ndipo tutaamua namna ya kushiriki uchaguzi huo,`` alisema Lwakatare.

Hata hivyo, Lwakatare alisema kwa sasa wamempeleka Tarime, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya CUF, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la chama hicho, Mustapha Wandwi, kushiriki uchaguzi wa marudio wa udiwani.

Uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Tarime , ambao unafuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wake, Chacha Wangwe aliyefariki dunia kwa ajali ya gari katika eneo la Pandambili, Wilaya ya Kongwa, mkoani Dodoma, Julai 28, unatarajia kufanyika Oktoba 12, mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, Chadema imemsimamisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Charles Mwera wakati NCCR-Mageuzi, imemsimamisha Enock Haruni, maarufu kama `Machomanne`, ambao watapambana na mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemsimamisha Christopher Ryoba Kangoye kuwania kiti hicho.
• SOURCE: NIPASHE
Tarime ni soo!

2008-09-26 16:35:51
Na Mwandishi Wetu, Tarime
Wakati siku za kuelekea uchaguzi mdogo wa kumsaka mbunge wa Jimbo la Tarime zikizidi kukaribia, hali ya kisiasa mjini hapa imeanza kuwa tete baada ya wafuasi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kuendelea kufanyiana visa mfululizo, vikiwemo vile vya kumwagiana pilipili na kuwatwangana mawe mikutanoni.

Uchaguzi huo mdogo, unatarajiwa kufanyika Oktoba 12, ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Chacha Wangwe, aliyefariki mjini Dodoma Julai 28 mwaka huu baada ya kupata ajali ya gari.

Jana, muendelezo wa visa vya baadhi ya wafuasi wa vyama hivyo vya CCM, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na DP ulifikia pabaya baada ya Mwenyekiti wa UDP, mchungaji Christopher Mtikila kupigwa jiwe la kichwa wakati akiwa kwenye mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya Sabasaba.

Mtikila alijeruhiwa vibaya na kukukimbiziwa hospitali mjini hapa ambako inadaiwa alishonwa nyuzi saba.

Kutokana na vibweka vinavyoendelea katika kampeni za kuelekea siku ya uchaguzi huo, , viongozi mbalimbali wa vyama vilivyosimamisha wagombea wamekuwa wakitoa kauli tofauti kuhusiana na yanayojiri.

Dk. Sengondo Mvungi (NCCR-Mageuzi)
Yeye aliripotiwa kuwa kiongozi wa kwanza kufanyiwa vurugu wakati wa kampeni jimboni humo.

Mvungi alikumbana na kadhia ya kutimuliwa kwa mawe wakati akimnadi mgombea wa chama chake cha NCCR.

Baada ya hapo, Dk. Mvungi ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alilaani tukio hilo na kueleza kuwa ni la hatari, kwani hakuna chama chenye hakimiliki ya jimbo hilo.

Pius Msekwa (CCM)
Makamu huyu Mwenyekiti wa CCM, naye alionja ya joto ya jiwe ya kufanyiwa vituko vya kampeni hizo wakati alipokuwa akimnadi mgombea wa chama chake, Bw. Ryoba Kangoba.

Msekwa alifanyiwa fujo na kuzomewa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa vyama pinzani.

Aidha, wafuasi wawili wa chama chake wameripotiwa kuumizwa baada ya mmoja kupigwa jiwe na mwingine kumwagiwa pilipili.

Kutokana na hali hiyo, bosi huyo namba mbili wa CCM akailalamikia hali hiyo na kuripotiwa akitishia kulifikisha suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete ili hatimaye zifanyike taratibu za kudhibiti hali ya namna hiyo ambayo ni ya hatari.

Christopher Mtikila (DP)
Baada ya kasheshe la jana la kupigwa mawe kwenye uwanja wa Sabasaba, amekaririwa akilalamikia hali hiyo aliyodai kuwa imetokana na njama za wapinzani wake.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mtikila amekaririwa leo asubuhi akisema: ``Nilitoa taarifa mapema kwa Msimamizi wa Uchaguzi na OCD.. niliwaeleza juu ya agizo la mimi kupigwa mawe...``

Freeman Mbowe (CHADEMA):Mbowe na chama chake cha CHADEMA wamekuwa nao wakilalama kuonewa na askari polisi walio katika operesheni kali ya kulinda amani katika jimbo hili.

Aidha, kwa nyakati tofauti, yeye, Katibu Mkuu wake Dk. Wilbroad Slaa na Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho, Halima Mdee, wamekuwa wakitoa madai ya kuonewa kwa kunyimwa viwanja vya kufanyia kampeni za mgombea ubunge wa chama chao, Bw. Charles Mwera.
Prof. Ibrahim Lipumba (CUF)

Baada ya kutosimamisha mgombea jimboni humo ili kuwapa fursa wenzao wa upinzani jimboni humo, Prof. Lipumba na chama chake wamekuwa katika wakati mgumu wa kuamua wamuunge mkono mgombea yupi baada ya wenzao kuwasaliti kwa kusimamisha mgombea zaidi ya mmoja, kinyume cha makubaliano.

Mkanganyiko huo unadaiwa kutokea baada ya vyama vinavyoungana nacho katika umoja wao wa vyama vikiwemo vya CHADEMA, TLP na NCCR-Mageuzi kushindwa kumsimamaisha mgombea mmoja, hasa baada ya NCCR na CHADEMA kusimamisha wagombea wawili tofauti.

Hata hivyo, ingawa CUF Tarime wameamua kumuunga mkono Bw. Charles Mwera wa CHADEMA, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilfred Lwakatare, amekaririwa asubuhi ya leo akisema kuwa wamemtuma jimboni humo kiongozi wao Mustafa Wandwi ili kuangalia ni mgombea yupi anayeelekea kukubalika zaidi ili hatimaye wamuunge mkono.

Wakati huohuo, Jeshi la Polisi jimboni humo limesema liko makini katika kudhibiti vitendo vyote vinavyoashiria kuvunja amani.

Akizungumza na Alasiri juzi, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Liberatus Barlow, amesema FFU na polisi wengine kibao waliomwagwa jimboni humo wamejipanga vilivyo katika kuhakikisha kuwa uvunjifu wa amani unadhibitiwa ipasavyo.

Wakati huohuo, katika kuthibitisha kuwa Polisi wako makini, tayari wameshawanasa watu wanne wanaotuhumiwa kumvurumishia mawe Mchungahji Mtikila jana na kuwawezesha kuburuzwa kortini.

Walionaswa na polisi katika tukio hilo la jana na ambao leo wamepandishwa kizimbani ili kujibu mashtaka.

Kamanda Barlow amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mussa Peter, Mwita Chacha, Hafidh Stanslaus na Mwita Kilongo.

Amesema watuhumumiwa hao, mmoja alikamatwa wakati wa tukio la kupigwa kwa Bw. Mtikila na wengine watatu walikamatwa jana katika msako wa Polisi uliofuatia kujiri kwa tukio hilo la kupigwa kwa Mtikila.
• SOURCE: ALASIRI
`Ndoa` ya Chadema, TLP, CUF yavunjika

2008-09-13 09:40:54
Na Simon Mhina
Ushirikiano wa kisiasa kati ya vyama vinne vya upinzani, umesambaratika baada ya vyama vitatu kati ya hivyo kuamua kusimamisha mgombea mmoja katika uchaguzi mdogo wa Tarime.

Wenyeviti wa vyama hivyo, Augustine Mrema (TLP) Profesa Ibrahim Lipumba (CUF) na James Mbatia (NCCR- Mageuzi) juzi walifanya kikao cha kujadili uchaguzi huo, na kumtenga mwenzao wa Chadema, Freeman Mbowe.

Japokuwa Profesa Lipumba alisema kwamba taarifa za kumwalika Mbowe zilitumwa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilibrod Slaa, alisema hakuna mwaliko wowote uliotumwa kwa bosi wake na Chama chake hakina mawasiliano yoyote na viongozi wa vyama hivyo vitatu.

Hata hivyo, Profesa Lipumba hakuweza kueleza kwamba walitumia njia gani kumpelekea Mbowe taarifa.

``Unajua hapa katikati kumetokea sintofahamu zilizosababishwa na kifo cha Wangwe (Mbunge wa zamani wa Tarime, Chacha), kuna kamgogoro baridi kanafukuta ndio maana hawakuhudhuria,`` alisema.

Alisema vyama vitatu vimeamua kuweka mgombea mmoja ili kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa Tarime.

Lipumba alisema baada ya kikao cha viongozi wakuu, wamepeleka madaraka yao kwa viongozi wa vyama vyao Jimbo la Tarime.

``Vikao vya wenyeviti wa taifa havitoshi, tunataka wenzetu wa Tarime nao wakutane, wao wanajuana na wanaelewa mazingira yao zaidi. Tunataka nao watuletee mapendekezo yao,`` alisema.

Hata hivyo, kiongozi huyo alisema kwamba ushirikiano wa vyama hivyo, hauondoi haki ya kila chama kufanya shughuli zake kwa mujibu wa sera na katiba yake.

Awali akitoa taarifa za kikao hicho, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa NCCR, Faustine Sungura, alisema kwa kauli moja, viongozi hao wamependekeza mgombea wa Chama hicho apitishwe.

Alimtaja mgombea aliyependekezwa kuwa Enock Haruna Marwa maarufu kwa jina la Macho Manne.

Sungura alisema kikao hicho kilichofanyika siku nzima, viongozi wa Chadema waliingia mitini.

Alisema haelewi ni kwanini viongozi wa Chadema waliingia mitini bila kutoa taarifa yoyote.

Awali akizungumzia sakata hilo, Dk. Slaa alisema pamoja na kutengwa na wenzao, wataendelea na maandalizi yao ya kuingia vitani.

``Tutaingia vitani kivyetu vyetu, hatuwezi kurudi nyuma. Lazima jimbo la Tarime tutalirudisha mikononi mwetu,`` alisema.

Alisema kutokana Chadema kutengwa ghafla na wapinzani wenzake, kitachukua hatua kadhaa kuhakikisha Jimbo hilo haliendi CCM kama ilivyokusudiwa.

Alisema Tarime kuna rasilimali nyingi ambazo zinaporwa, hivyo waporaji wanaweza kuhakikisha wanasaidia mkakati wowote wenye lengo la kuifanya Tarime iwe ya CCM.

Mbunge huyo alisema Chadema kina mtaji mkubwa wa kisiasa Tarime, hivyo hakitishwi wala kubabaishwa na uamuzi wa kutengwa.

Vyama vya Chadema, TLP na CUF vilianza ushirikiano rasmi bungeni na kuunda kambi rasmi ya upinzani ambayo inatambulika rasmi bungeni.

Tangu kifo cha Wangwe kilichotokea kwa ajali ya gari Julai 28, 2008 iliyotokea kijiji cha Pandambili, Kongwa mkoani Dodoma akiwa safarini kwenda Dar es Salaam, kumekuwa na mvutano wa wazi baina ya viongozi wa kambi hiyo.

Tukio la kipekee lililotokea ni pale mazishi ya Wangwe yalipoahirishwa Julai 31, 2008 kutokana na familia kutaka uchunguzi wa kujitegemea juu ya chanzo cha kifo cha mbunge huyo, hali iliyowagawa viongozi hao kwenye makundi mawili.

Chadema wamekuwa wakilaumu wenzao kwamba walitaka kutumia msiba huo kupata faida ya kisiasa Tarime na kukiangamiza chama hao. Lawama ambazo pia zimeelekezwa kwa CCM.
• SOURCE: NIPASHE
 
CUF njia panda uchaguzi Tarime

2008-09-26 09:14:05
Na Muhibu Said
Hatua ya vyama vya Chadema na NCCR-Mageuzi kusimamisha wagombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, mkoani Mara, imekiweka Chama cha Wananchi (CUF) njiapanda, baada ya makao makuu ya chama hicho hadi sasa kushindwa kuamua mgombea wa chama kipi kati ya vyama hivyo `wampigie debe`.

Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na TLP, ni vyama vilivyoamua kuunda ushirikiano wa kisiasa katika kambi ya upinzani na miongoni mwa makubaliano waliyofikia katika ushirikiano huo, ni pamoja na kushirikiana katika chaguzi kwa lengo la kukishinda katika uchaguzi na kuking`oa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Wilfred Lwakatare aliliambia Nipashe ofisini kwake jijini Dar es Salaam juzi kuwa, hadi sasa makao makuu ya chama hicho, hawajafikia uamuzi wa mgombea wa chama kipi wamuunge mkono katika uchaguzi kwa madai kwamba suala hilo linahitaji busara kabla ya kuamua.

``Sisi baada ya kuona uwezo wetu ni mdogo wa kushinda jimboni humo, tuliamua kumwondoa mgombea wetu. Wenzetu NCCR na Chadema wamesimamisha wagombea. Mgombea wa chama kipi kati ya hivyo tuelekeze nguvu zetu, suala hilo linahitaji busara ya hali juu kuamua,`` alisema Lwakatare.

Hata hivyo, alisema watafikia uamuzi wa mgombea wa chama kipi wampigie debe, mara tu watakapopata taarifa kutoka kwa uongozi wa CUF Tarime kutokana na upepo wa kisiasa katika kinyang`anyiro cha uchaguzi huo utakavyokuwa ukienda.

``Tutakapopata taarifa kutoka uongozi wa CUF Wilaya ya Tarime, ndipo tutaamua namna ya kushiriki uchaguzi huo,`` alisema Lwakatare.

Hata hivyo, Lwakatare alisema kwa sasa wamempeleka Tarime, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya CUF, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la chama hicho, Mustapha Wandwi, kushiriki uchaguzi wa marudio wa udiwani.

Uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Tarime , ambao unafuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wake, Chacha Wangwe aliyefariki dunia kwa ajali ya gari katika eneo la Pandambili, Wilaya ya Kongwa, mkoani Dodoma, Julai 28, unatarajia kufanyika Oktoba 12, mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, Chadema imemsimamisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Charles Mwera wakati NCCR-Mageuzi, imemsimamisha Enock Haruni, maarufu kama `Machomanne`, ambao watapambana na mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemsimamisha Christopher Ryoba Kangoye kuwania kiti hicho.
• SOURCE: NIPASHE
Tarime ni soo!

2008-09-26 16:35:51
Na Mwandishi Wetu, Tarime
Wakati siku za kuelekea uchaguzi mdogo wa kumsaka mbunge wa Jimbo la Tarime zikizidi kukaribia, hali ya kisiasa mjini hapa imeanza kuwa tete baada ya wafuasi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kuendelea kufanyiana visa mfululizo, vikiwemo vile vya kumwagiana pilipili na kuwatwangana mawe mikutanoni.

Uchaguzi huo mdogo, unatarajiwa kufanyika Oktoba 12, ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Chacha Wangwe, aliyefariki mjini Dodoma Julai 28 mwaka huu baada ya kupata ajali ya gari.

Jana, muendelezo wa visa vya baadhi ya wafuasi wa vyama hivyo vya CCM, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na DP ulifikia pabaya baada ya Mwenyekiti wa UDP, mchungaji Christopher Mtikila kupigwa jiwe la kichwa wakati akiwa kwenye mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya Sabasaba.

Mtikila alijeruhiwa vibaya na kukukimbiziwa hospitali mjini hapa ambako inadaiwa alishonwa nyuzi saba.

Kutokana na vibweka vinavyoendelea katika kampeni za kuelekea siku ya uchaguzi huo, , viongozi mbalimbali wa vyama vilivyosimamisha wagombea wamekuwa wakitoa kauli tofauti kuhusiana na yanayojiri.

Dk. Sengondo Mvungi (NCCR-Mageuzi)
Yeye aliripotiwa kuwa kiongozi wa kwanza kufanyiwa vurugu wakati wa kampeni jimboni humo.

Mvungi alikumbana na kadhia ya kutimuliwa kwa mawe wakati akimnadi mgombea wa chama chake cha NCCR.

Baada ya hapo, Dk. Mvungi ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alilaani tukio hilo na kueleza kuwa ni la hatari, kwani hakuna chama chenye hakimiliki ya jimbo hilo.

Pius Msekwa (CCM)
Makamu huyu Mwenyekiti wa CCM, naye alionja ya joto ya jiwe ya kufanyiwa vituko vya kampeni hizo wakati alipokuwa akimnadi mgombea wa chama chake, Bw. Ryoba Kangoba.

Msekwa alifanyiwa fujo na kuzomewa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa vyama pinzani.

Aidha, wafuasi wawili wa chama chake wameripotiwa kuumizwa baada ya mmoja kupigwa jiwe na mwingine kumwagiwa pilipili.

Kutokana na hali hiyo, bosi huyo namba mbili wa CCM akailalamikia hali hiyo na kuripotiwa akitishia kulifikisha suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete ili hatimaye zifanyike taratibu za kudhibiti hali ya namna hiyo ambayo ni ya hatari.

Christopher Mtikila (DP)
Baada ya kasheshe la jana la kupigwa mawe kwenye uwanja wa Sabasaba, amekaririwa akilalamikia hali hiyo aliyodai kuwa imetokana na njama za wapinzani wake.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mtikila amekaririwa leo asubuhi akisema: ``Nilitoa taarifa mapema kwa Msimamizi wa Uchaguzi na OCD.. niliwaeleza juu ya agizo la mimi kupigwa mawe...``

Freeman Mbowe (CHADEMA):Mbowe na chama chake cha CHADEMA wamekuwa nao wakilalama kuonewa na askari polisi walio katika operesheni kali ya kulinda amani katika jimbo hili.

Aidha, kwa nyakati tofauti, yeye, Katibu Mkuu wake Dk. Wilbroad Slaa na Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho, Halima Mdee, wamekuwa wakitoa madai ya kuonewa kwa kunyimwa viwanja vya kufanyia kampeni za mgombea ubunge wa chama chao, Bw. Charles Mwera.
Prof. Ibrahim Lipumba (CUF)

Baada ya kutosimamisha mgombea jimboni humo ili kuwapa fursa wenzao wa upinzani jimboni humo, Prof. Lipumba na chama chake wamekuwa katika wakati mgumu wa kuamua wamuunge mkono mgombea yupi baada ya wenzao kuwasaliti kwa kusimamisha mgombea zaidi ya mmoja, kinyume cha makubaliano.

Mkanganyiko huo unadaiwa kutokea baada ya vyama vinavyoungana nacho katika umoja wao wa vyama vikiwemo vya CHADEMA, TLP na NCCR-Mageuzi kushindwa kumsimamaisha mgombea mmoja, hasa baada ya NCCR na CHADEMA kusimamisha wagombea wawili tofauti.

Hata hivyo, ingawa CUF Tarime wameamua kumuunga mkono Bw. Charles Mwera wa CHADEMA, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilfred Lwakatare, amekaririwa asubuhi ya leo akisema kuwa wamemtuma jimboni humo kiongozi wao Mustafa Wandwi ili kuangalia ni mgombea yupi anayeelekea kukubalika zaidi ili hatimaye wamuunge mkono.

Wakati huohuo, Jeshi la Polisi jimboni humo limesema liko makini katika kudhibiti vitendo vyote vinavyoashiria kuvunja amani.

Akizungumza na Alasiri juzi, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Liberatus Barlow, amesema FFU na polisi wengine kibao waliomwagwa jimboni humo wamejipanga vilivyo katika kuhakikisha kuwa uvunjifu wa amani unadhibitiwa ipasavyo.

Wakati huohuo, katika kuthibitisha kuwa Polisi wako makini, tayari wameshawanasa watu wanne wanaotuhumiwa kumvurumishia mawe Mchungahji Mtikila jana na kuwawezesha kuburuzwa kortini.

Walionaswa na polisi katika tukio hilo la jana na ambao leo wamepandishwa kizimbani ili kujibu mashtaka.

Kamanda Barlow amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mussa Peter, Mwita Chacha, Hafidh Stanslaus na Mwita Kilongo.

Amesema watuhumumiwa hao, mmoja alikamatwa wakati wa tukio la kupigwa kwa Bw. Mtikila na wengine watatu walikamatwa jana katika msako wa Polisi uliofuatia kujiri kwa tukio hilo la kupigwa kwa Mtikila.
• SOURCE: ALASIRI
`Ndoa` ya Chadema, TLP, CUF yavunjika

2008-09-13 09:40:54
Na Simon Mhina
Ushirikiano wa kisiasa kati ya vyama vinne vya upinzani, umesambaratika baada ya vyama vitatu kati ya hivyo kuamua kusimamisha mgombea mmoja katika uchaguzi mdogo wa Tarime.

Wenyeviti wa vyama hivyo, Augustine Mrema (TLP) Profesa Ibrahim Lipumba (CUF) na James Mbatia (NCCR- Mageuzi) juzi walifanya kikao cha kujadili uchaguzi huo, na kumtenga mwenzao wa Chadema, Freeman Mbowe.

Japokuwa Profesa Lipumba alisema kwamba taarifa za kumwalika Mbowe zilitumwa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilibrod Slaa, alisema hakuna mwaliko wowote uliotumwa kwa bosi wake na Chama chake hakina mawasiliano yoyote na viongozi wa vyama hivyo vitatu.

Hata hivyo, Profesa Lipumba hakuweza kueleza kwamba walitumia njia gani kumpelekea Mbowe taarifa.

``Unajua hapa katikati kumetokea sintofahamu zilizosababishwa na kifo cha Wangwe (Mbunge wa zamani wa Tarime, Chacha), kuna kamgogoro baridi kanafukuta ndio maana hawakuhudhuria,`` alisema.

Alisema vyama vitatu vimeamua kuweka mgombea mmoja ili kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa Tarime.

Lipumba alisema baada ya kikao cha viongozi wakuu, wamepeleka madaraka yao kwa viongozi wa vyama vyao Jimbo la Tarime.

``Vikao vya wenyeviti wa taifa havitoshi, tunataka wenzetu wa Tarime nao wakutane, wao wanajuana na wanaelewa mazingira yao zaidi. Tunataka nao watuletee mapendekezo yao,`` alisema.

Hata hivyo, kiongozi huyo alisema kwamba ushirikiano wa vyama hivyo, hauondoi haki ya kila chama kufanya shughuli zake kwa mujibu wa sera na katiba yake.

Awali akitoa taarifa za kikao hicho, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa NCCR, Faustine Sungura, alisema kwa kauli moja, viongozi hao wamependekeza mgombea wa Chama hicho apitishwe.

Alimtaja mgombea aliyependekezwa kuwa Enock Haruna Marwa maarufu kwa jina la Macho Manne.

Sungura alisema kikao hicho kilichofanyika siku nzima, viongozi wa Chadema waliingia mitini.

Alisema haelewi ni kwanini viongozi wa Chadema waliingia mitini bila kutoa taarifa yoyote.

Awali akizungumzia sakata hilo, Dk. Slaa alisema pamoja na kutengwa na wenzao, wataendelea na maandalizi yao ya kuingia vitani.

``Tutaingia vitani kivyetu vyetu, hatuwezi kurudi nyuma. Lazima jimbo la Tarime tutalirudisha mikononi mwetu,`` alisema.

Alisema kutokana Chadema kutengwa ghafla na wapinzani wenzake, kitachukua hatua kadhaa kuhakikisha Jimbo hilo haliendi CCM kama ilivyokusudiwa.

Alisema Tarime kuna rasilimali nyingi ambazo zinaporwa, hivyo waporaji wanaweza kuhakikisha wanasaidia mkakati wowote wenye lengo la kuifanya Tarime iwe ya CCM.

Mbunge huyo alisema Chadema kina mtaji mkubwa wa kisiasa Tarime, hivyo hakitishwi wala kubabaishwa na uamuzi wa kutengwa.

Vyama vya Chadema, TLP na CUF vilianza ushirikiano rasmi bungeni na kuunda kambi rasmi ya upinzani ambayo inatambulika rasmi bungeni.

Tangu kifo cha Wangwe kilichotokea kwa ajali ya gari Julai 28, 2008 iliyotokea kijiji cha Pandambili, Kongwa mkoani Dodoma akiwa safarini kwenda Dar es Salaam, kumekuwa na mvutano wa wazi baina ya viongozi wa kambi hiyo.

Tukio la kipekee lililotokea ni pale mazishi ya Wangwe yalipoahirishwa Julai 31, 2008 kutokana na familia kutaka uchunguzi wa kujitegemea juu ya chanzo cha kifo cha mbunge huyo, hali iliyowagawa viongozi hao kwenye makundi mawili.

Chadema wamekuwa wakilaumu wenzao kwamba walitaka kutumia msiba huo kupata faida ya kisiasa Tarime na kukiangamiza chama hao. Lawama ambazo pia zimeelekezwa kwa CCM.
• SOURCE: NIPASHE

NI kawaida usipokuwa na ushahidi wa uhakika chochote jaribu kinaweza kusaidia.
 
Uchaguzi mkuu CUF kufanyika leo Dar
Salim Said

MKUTANO Mkuu wa nne na wa mwisho kwa awamu inayomaliza muda wake wa uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) unaaza leo Dar es Salaam, huku homa ya uchaguzi ikiwa imetanda miongoni mwa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti.


Mkutano huo unafanyika ukiwa na lengo kuu la kuchagua timu mpya itakayoibeba CUF kwa kipindi kingine cha miaka mitano kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka 2014 baada ya ile iliyopo kumaliza muda wake.


Nafasi zinazogombewa na wanachama mbalimbali wa chamahicho ni za Mwenyekiti na makamu wake, katibu Mkuu na wajumbe 45 wa Baraza kuu la uongozi la chama.


Katika nafasi ya mwenyekiti vigogo watatu wanawania nafasi hiyo ambao ni Profesa Abdallah Safari, Profesa Ibrahimu Lipumba na Steven Masanja wakati Makamu Mwenyekiti wa sasa Machano Khamis Ali na Katibu Mkuu wa sasa Maalim Seif Sharif Hamad wakiwa wagombea pekee katika nafasi zao.


Kutokana na mazingira hayo, Hamad na Machano tayari wamejihakikishia ushindi kwa asilimia 90 katika nafasi zao katika kinyang’anyiro hicho.


Hayo yanathibitishwa na Hamad kwa kuwambia wagombea na wajumbe wa kikao cha Baraza kuu la chama hicho kuwa kikao hicho ni cha kuagana kwani kuna wengine watarudi na wengine watatupwa nje.


"Mimi nawajua baadhi yao ambao hawatarudi, akiwemo mheshimiwa Jussa Ismail na Suleiman Dedes. Hawa hawatarudi kwa sababu hawakuomba wala hawakujaza fomu za kugombea," alisema Hamad na kuongeza:


"Lakini hata kama umeomba na kujaza fomu, unaweza usipite kwa kuwa katika uchaguzi kitu chochote kinaweza kutokea, hivyo siwaombei mabaya lakini lazima mjue hilo, kuna kushinda na kushindwa."


Aidha, homa ya uchaguzi pia ipo kwa wagombea ujumbe wa Baraza kuu la uongozi la chama hicho ambapo hadi sasa kuna wagombea 107 katika nafasi hiyo, 70 kutoka bara na 37 kutoka Zanzibar.


"Kati ya wagombea hao tunahitaji wajumbe 45 tu watakaoviendesha vikao vya Baraza kuu la uongozi ndani ya kipindi cha miaka mitano, 25 kutoka Tanzania bara na 20 kutoka Zanzibar" anasema Joram Bashange Naibu Mkurugenzi wa oganaizesheni.


Naye Mkuu wa idara yaMambo ya nje na uhusiano wa kimataifa, Jussa Ismail alisema CUF itaitangaza rasmi itikadi yake katika mkutano mkuu unaoanza leo


"Siku nyingi watu walikuwa wakijiuliza kuhusu itikadi ya chama chetu, hivyo moja ya shughuli ambazo zitafanyika katika mkutano mkuu ni kutangaza rasmi kwamba CUF inafuata itikadi ya kiliberali," alisema Jussa.


Alisema shughuli nyingine za mkutano huo ni kupokea taarifa ya utendaji wa chama ya miaka mitano iliyopita na kupitisha marekebisho ya katiba.


"Vipengele ambavyo vimefanyiwa marekebisho ni pamoja na kile kinachohusu upatikanaji wa wagombea wa ubunge, uwakilishi na udiwani ambapo imependekezwa kuwa watapigiwa kura za maoni na wanachama katika majimbo yao," alisema Jussa.


Kwa mujibu wa Jussa, chama hicho pia kina mpango wa kuongeza uwakilishi wa wanawake katika vikao vya maamuzi ili kwenda sambamba na matakwa ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kiuchumi Kusini mwa Afrika (SADC).”


Mkutano huo unafanyika chini ya mgeni rasmi Msajili wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa na kuhudhuriwa na Mabalozi wa nchi mbalimbali, wajumbe kutoka vyama vyote vyenye usajili wa kudumu, Asasi za Kiraia (Azaki) na wasomi

Source: Gazeti la Mwananchi
 
CUF ni chama muflis. Huu uchaguzi wa leo, si lolote, si chochote ni zuga tuu ili kutimiza matakwa ya katiba yao. Wameweka wapinzani zuga ili umma uone CUF kuna demokrasia, hakuna demokrasia yoyote ndani ya cuf ni udikteta, umujahidina na usultani wa kisiri siri.

Seif Sharif Hamad anasemekana ni mwana haram wa Sultan Jamsid. Hii ni siri kubwa ya ndani. Akishika uongozi Zanzibar, anayakana Mapinduzi Matukufu ya Januari 64. Analivunja Baraza la Mapinduzi na kuutambua rasmi uhuru wa Zanzibar wa Desemba 63. Anatoa msamaha kwa kwa ukoo wa Kisultani na kurudisha Usultani Zanzibar maana yeye mwenywe ni Sultan kisiri siri. Usultan utakaorejeshwa sio wa utawala tena bali ceremonial tuu. Nasaba ya mwisho ya Sultan wa Persia ni Mfalme wa Brunei. Ukoo wa Ottoman Empire katika kujitanua, wanamfalme walisambaa maeneo mbalimbali, wale waliokuwa watiifu kwa Mfalme Baba yao, waliposhika visiwa walijitangaza ma Sultan chini ya Falme ya Persia na ndivyo alivyofanya Seyyid Said Bin Barghash alipoitwaa pwani ya Afrika Mashariki toka Sofala mpaka Lamu, na visiwa vyote na eneo lakilomita kumi/20 la bara toka usawa wa bahari. Nduguye alitwaa visiwa vya Brunei baada ya kukuta utajiri mkubwa wa mafuta, akauvua Usultani na kujitangazia ufalme.
Ni nasaba hii ya Kisultani ndio inamfanya mfalme huyo kuwa mfadhili mkubwa wa CUF kupitia kwa Seif Sharrif Hamad. Viongozi wa CUF Zanzibar wanalielewa hili ndio maana hawathubut kumpinga Seif hata chembe.

Sio siri CUF ina viongozi wazuri, waadilifu, wenye uwezo wa uongozi na upeo wa kuona mbali ka Juma Duni na Hamad Rashid, wana CUF wanajua Seif 'kwishney' hana uwezo wowote kwa sasa zaidi ya fedha za Mfalme lakini hakuna wa kukohoa kwa sababu ni Sultan.

Seif ana siasa za jazba, chuki, hasira na dalili za kulipiza kisasi ndio maana anautaka urais wa ZnZ kwa udi na uvumba, na siku zote huwa anashinda, lakini kamwe hapewi nchi, wenye nchi wayajua hayo yalijificha moyoni mwake.
Hata uchaguzi Zanzibar ukiitishwa kesho, Seif anashinda sio kwa sababu ni mahiri, bali anapendwa na wote waliolizwa na Mapinduzi. Hata asipopiga kampeni yoyote, bado atashinda kwa sababu Wapemba hawakushiriki Mapinduzi na Washirazi na masalia ya Sultan ndio watakao mchagua.
Kama CUF wangekubali kumsimamisha Juma Duni ama Hamad Rashid urais wa Zanzibar, nawahakikishia mpaka wana CCM wataichagua CUF na wenye nchi wataikabidhi nchi.

Lipumba nae hana jipya, ni nyimbo zile zile. Huyo mgombea Mkristu ameweka hapo boya tuu ili kufuta hisia za udini huku bara na watampa vijikura vya kuzugia ili demokrasia ionekane kumbe ni kiini macho.

Prof. Safari ndio hafai, hafai kabisa, kama Lipumba asipochaguliwa na akachaguliwa Safari, basi hiyo itakuwa ni kazi ya Seif kamtosa Lipumba.

Prof. Safari alinifundisha sheria pale Mlimani, hakuna ubishi ana uwezo mkubwa kiakili, ni mwanasheria mahiri na high convincing power. Tatizo jamaa ana ulimi wa upanga, Jamaa ni Mujahidina na Muslim Fundamentalist ambaye akiishika CUF, wakipokwa ushindi, jamaa atawaconvince wale Blue Guard wajitoe muhanga.
Kama Seif ni moto na Safari ni moto, kitakachofuatia ni mlipuko tuu. Wote wana jazba, seif ana kauli za ukali, Safari ana mdomo mchafu na anachukia ukiristo akiwaita Makafir.
Mikutano ya CUF itakuwa nu upanga wa makali kuwili.

Naona nisiseme sana hebu tusubiri matokeo.
















Lipumba
 
hakuna demokrasia yoyote ndani ya cuf ni udikteta, umujahidina na usultani wa kisiri siri.

Seif Sharif Hamad anasemekana ni mwana haram wa Sultan Jamsid. Hii ni siri kubwa ya ndani. Akishika uongozi Zanzibar, anayakana Mapinduzi Matukufu ya Januari 64. Analivunja Baraza la Mapinduzi na kuutambua rasmi uhuru wa Zanzibar wa Desemba 63. Anatoa msamaha kwa kwa ukoo wa Kisultani na kurudisha Usultani Zanzibar maana yeye mwenywe ni Sultan kisiri siri.

Sio siri CUF ina viongozi wazuri, waadilifu, wenye uwezo wa uongozi na upeo wa kuona mbali ka Juma Duni na Hamad Rashid, wana CUF wanajua Seif 'kwishney' hana uwezo wowote kwa sasa zaidi ya fedha za Mfalme lakini hakuna wa kukohoa kwa sababu ni Sultan.

Seif ana siasa za jazba, chuki, hasira na dalili za kulipiza kisasi ndio maana anautaka urais wa ZnZ kwa udi na uvumba, na siku zote huwa anashinda, lakini kamwe hapewi nchi, wenye nchi wayajua hayo yalijificha moyoni mwake.

Lipumba nae hana jipya, ni nyimbo zile zile. Huyo mgombea Mkristu ameweka hapo boya tuu ili kufuta hisia za udini huku bara na watampa vijikura vya kuzugia ili demokrasia ionekane kumbe ni kiini macho.

Prof. Safari ndio hafai, hafai kabisa, kama Lipumba asipochaguliwa na akachaguliwa Safari, basi hiyo itakuwa ni kazi ya Seif kamtosa Lipumba.

Prof. Safari alinifundisha sheria pale Mlimani, hakuna ubishi ana uwezo mkubwa kiakili, ni mwanasheria mahiri na high convincing power. Tatizo jamaa ana ulimi wa upanga, Jamaa ni Mujahidina na Muslim Fundamentalist ambaye akiishika CUF, wakipokwa ushindi, jamaa atawaconvince wale Blue Guard wajitoe muhanga.

Mhhhh, Pasco wakikusikia..... mimi nakaa kando. Mchambuzi mahiri wa mambo ya siasa. Unajua kuwa Serikali ya mapinduzi ilishamsamehe sultani, ama hilo hukuwahi kulisikia?. Kwa hiyo Seif hana haja ya kufanya hilo. Wapinzani bila kufunga masikio, CCM wanatumia kila njia CUF wadini, CHADEMA wakabila. Lakini suala ni moja tu, mfa maji...
 
Nina matatizo sana na ma Prof.Sijui kama watafanikiwa lengo lao kuweka Prof.Mwingine...
 
Nimekusoma Mwalimu,kimsingi hata mimi simjfahamu sana Profesa Safari(zaidi ya kufahamu kwamba ni mwanasheria na pia mchangiaji wa vipindi vya redio na luninga vinavyohusiana na Lugha yetu adhimu ya Kiswahili),ndo maana nikawaomba wanajamii humu ndani kama wanamfahamu watujuze Profesa huyu ni mtu wa aina gani hasa...Ubarikiwe sana Mwalimu Zawadi

Profile:
Profesa Safari alizaliwa June 3, 1951.
Education background:
1972- Secondary,
1979- University of Dar es salaam shahada ya sheria (LLB),
1985- Master (LLM),
1995- (PhD) University of Sussex England.Baada ya kupata shahada hiyo alibaki England akawa anafundisha,
2000- Alitunukiwa u Profesa.
Work Experience
1972-1974 Matafiti msaidizi katika taasisi ya Institutes of Kiswahili Research
1974-1976 Mhariri katika kampuni ya Tanzania Publishing House
1979-1986 Wakili wa serikali katika wizara ya sheria
1988-1991 Afisa Mtafiti na uchapishaji katika kituo cha Uhisiano wa nje then Mhadhiri mwandamizi wa sheria katika kituo hicho
Nyazifa(Vyeo) alivyowahi kushika;
1978-1986 Mwenyekiti wa Chama cha wanasheria wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam
1982-1984 Mhadhiri wa sheria university of Dar es Salaam
1983-1986 Mkuu wa Kitengo cha sheria ,wizara ya sheria
1984-1986 Mwakilishi wa wizara ya sheria katika baraza la elimu ya sheria Africa Mashariki
1990-1991 Kaimu Mkurugenzi wa masomo na program katika kituo cha mahusiano ya kimataifa
1996-Hadi sasa, Mwenyekiti wa chama cha wandishi wa Vitabu Tanzania (UWAVITA),pia Mkurugenzi wa Masomo na programu wa kituo cha uhusiano wa Kimataifa
1999-Hadi sasa, Katibu Mkuu wa Tanzania Center for Conflict Resolution, also Mkurugenzi wa bodi ya hakimiliki(COSOTA)
Makongamano:
1978-Alihudhuria mikutano kadhaa ya Kimataifa kuhusiana na mambo ya sheria barani Africa huko Nairobi (All African Law Students Association)
Aidha,amewahi kuhudhuria makongamano mbalimbali yaliyohusu mambo ya sheria katika sehemu zifuatazo,Africa Kusini,Sweden,Geneva,Botswana,Uganda na Marekani
Tuzo alizowahi kupata:
1991-alitunukiwa tuzo iitwayo Ford Foundation Scholarship for Doctor of Philosophy programme
1999-2001, Shaaban Robert Literary
Maisha yake:
Ameoa na ana watoto wawili.
Prof anasema anawania Uenyekiti wa CUF kwa kuwa anataka kuleta mabadiliko makubwa ndani ya chama ili kionekane ni cha kitaifa.Alisema bila mbadiliko chama kinaweza kufa.
Prof hivi sasa ni wakili katika Mahakama Kuu ya Tanzania,amekuwa katika uwakili tangu 1987.
 
CUF ni chama muflis. Huu uchaguzi wa leo, si lolote, si chochote ni zuga tuu ili kutimiza matakwa ya katiba yao. Wameweka wapinzani zuga ili umma uone CUF kuna demokrasia, hakuna demokrasia yoyote ndani ya cuf ni udikteta, umujahidina na usultani wa kisiri siri.

Seif Sharif Hamad anasemekana ni mwana haram wa Sultan Jamsid. Hii ni siri kubwa ya ndani. Akishika uongozi Zanzibar, anayakana Mapinduzi Matukufu ya Januari 64. Analivunja Baraza la Mapinduzi na kuutambua rasmi uhuru wa Zanzibar wa Desemba 63. Anatoa msamaha kwa kwa ukoo wa Kisultani na kurudisha Usultani Zanzibar maana yeye mwenywe ni Sultan kisiri siri. Usultan utakaorejeshwa sio wa utawala tena bali ceremonial tuu. Nasaba ya mwisho ya Sultan wa Persia ni Mfalme wa Brunei. Ukoo wa Ottoman Empire katika kujitanua, wanamfalme walisambaa maeneo mbalimbali, wale waliokuwa watiifu kwa Mfalme Baba yao, waliposhika visiwa walijitangaza ma Sultan chini ya Falme ya Persia na ndivyo alivyofanya Seyyid Said Bin Barghash alipoitwaa pwani ya Afrika Mashariki toka Sofala mpaka Lamu, na visiwa vyote na eneo lakilomita kumi/20 la bara toka usawa wa bahari. Nduguye alitwaa visiwa vya Brunei baada ya kukuta utajiri mkubwa wa mafuta, akauvua Usultani na kujitangazia ufalme.
Ni nasaba hii ya Kisultani ndio inamfanya mfalme huyo kuwa mfadhili mkubwa wa CUF kupitia kwa Seif Sharrif Hamad. Viongozi wa CUF Zanzibar wanalielewa hili ndio maana hawathubut kumpinga Seif hata chembe.

Sio siri CUF ina viongozi wazuri, waadilifu, wenye uwezo wa uongozi na upeo wa kuona mbali ka Juma Duni na Hamad Rashid, wana CUF wanajua Seif 'kwishney' hana uwezo wowote kwa sasa zaidi ya fedha za Mfalme lakini hakuna wa kukohoa kwa sababu ni Sultan.

Seif ana siasa za jazba, chuki, hasira na dalili za kulipiza kisasi ndio maana anautaka urais wa ZnZ kwa udi na uvumba, na siku zote huwa anashinda, lakini kamwe hapewi nchi, wenye nchi wayajua hayo yalijificha moyoni mwake.
Hata uchaguzi Zanzibar ukiitishwa kesho, Seif anashinda sio kwa sababu ni mahiri, bali anapendwa na wote waliolizwa na Mapinduzi. Hata asipopiga kampeni yoyote, bado atashinda kwa sababu Wapemba hawakushiriki Mapinduzi na Washirazi na masalia ya Sultan ndio watakao mchagua.
Kama CUF wangekubali kumsimamisha Juma Duni ama Hamad Rashid urais wa Zanzibar, nawahakikishia mpaka wana CCM wataichagua CUF na wenye nchi wataikabidhi nchi.

Lipumba nae hana jipya, ni nyimbo zile zile. Huyo mgombea Mkristu ameweka hapo boya tuu ili kufuta hisia za udini huku bara na watampa vijikura vya kuzugia ili demokrasia ionekane kumbe ni kiini macho.

Prof. Safari ndio hafai, hafai kabisa, kama Lipumba asipochaguliwa na akachaguliwa Safari, basi hiyo itakuwa ni kazi ya Seif kamtosa Lipumba.

Prof. Safari alinifundisha sheria pale Mlimani, hakuna ubishi ana uwezo mkubwa kiakili, ni mwanasheria mahiri na high convincing power. Tatizo jamaa ana ulimi wa upanga, Jamaa ni Mujahidina na Muslim Fundamentalist ambaye akiishika CUF, wakipokwa ushindi, jamaa atawaconvince wale Blue Guard wajitoe muhanga.
Kama Seif ni moto na Safari ni moto, kitakachofuatia ni mlipuko tuu. Wote wana jazba, seif ana kauli za ukali, Safari ana mdomo mchafu na anachukia ukiristo akiwaita Makafir.
Mikutano ya CUF itakuwa nu upanga wa makali kuwili.

Naona nisiseme sana hebu tusubiri matokeo.
















Lipumba


Chuki tupu. Lengo la chama chochote ni kutekeleza matakwa ya katiba yao kama ilivyoelekezwa na msajili wa vyama. Ni lazima katiba ifuatwe sasa wewe Pasco sijui unataka nini. Mi naona poa tu kama wanatekeleza katika na hiyo ndiyo democrasy. Mengine huko chini sikusoma maana nimeona waste of time baada ya kuona mwanzo statement yako. Unajua kila siku introduction ni muhimu sana kuvutia interest za wasomaji.
 
Siku kama 2 zilizopita nilimsikia Profesa huyu akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.Katika mahojiano hayo Profesa SAFARI alitangaza nia yake ya kutaka kugombea Uenyekiti wa Taifa Chama cha Wananchi(CUF)..Katika maelezo yake alisema kwamba lengo hasa la kugombe ni kutaka kurudisha uhai wa CUF ambacho(kwa mujibu wa maelezo yake) ni kama kimepoteza umaarufu na kwamba kinahitaji mabadiliko ya uongozi ngazi ya Taifa kwani uongozi wa sasa umekaa muda mrefu na haujaleta mabadiliko yoyote(alizungumzia suala la CUF kutokuwa na mbunge hata mmoja wa kuchaguliwa kutoka Tanzania bara),pia alizungumzia suala la mikutano ya CUF kutokuwa na mahudhurio ya kuridhisha kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo alisema kwamba sasa hivi mpaka wanachama waambiwe kuwa kutakuwa na Pilau ndio mahudhurio kidogo yanakuwa ya kuridhisha...Binafsi namfahamu Profesa SAFARI kama Mwanasheria maarufu na mtaalamu mahiri wa Lugha yetu adhimu ya Kiswahili...Swali,,Je kwa wanaomfahamu Profesa huyu,ana uzoefu gani katika mambo ya kisiasa???,anaweza kuvaa viatu vya Profesa Lipumba???,hivi uchaguzi mkuu wa CUF unafanyika lini???....Mkuu Mzee Mwanakijiji ninaomba kama inawezekana ufanye mahojiano na Profesa huyu na kuyaweka hapa maana kwa jinsi nilivyomsikia ana uchungu sana na jinsi CUF ilivyopoteza umaarufu(kwa mtizamo wake)..Naomba kuwasilisha wakuu...Mbarikiwe sana


Chama cha CUF kinatarajia kufanya Mkutano Mkuu wake Ijumaa February 27,mwaka huu ambapo Profesa Abdallah Jumbe Saffari anawania nafasi ya Uwenyekiti,nafasi ambayo kwa hivi sasa inashikiliwa na Profesa Ibrahimu Lipumba ambaye ameshika nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka kumi sasa.
 
Chuki tupu. Lengo la chama chochote ni kutekeleza matakwa ya katiba yao kama ilivyoelekezwa na msajili wa vyama. Ni lazima katiba ifuatwe sasa wewe Pasco sijui unataka nini. Mi naona poa tu kama wanatekeleza katika na hiyo ndiyo democrasy. Mengine huko chini sikusoma maana nimeona waste of time baada ya kuona mwanzo statement yako. Unajua kila siku introduction ni muhimu sana kuvutia interest za wasomaji.

Kinachonishangaza na mimi ni comments za Pasco hasa za mwanzoni zimenifanya sikusoma mengineyo. Mtu anavyojitambulisha inatosha kujua anakoelekea.
 
CUF huku bara ni very artificial, support base yake hasa ni ya waswahili, iliterates na baadhi ya vijana wenye jazba kutokana na kutambua kuwa uduni wao unatokana na sera mbaya za chama tawala. Bahati mbaya wameweza kupenetrate kwenye sehemu ndogo sana bara, lakini ZNZ ni hadithi nyingine. CUF ZNZ iko very organised, inaweza kuchukua na kutawala dola effectiveky hata in half hour notice. Kitu ambacho huku bara bado hakipo.
Profesa Lipumba nni mtu mwenye personality inayostahili kwa chama kikubwa kama CUF. Lakini sio profesa Safari, Profesa Safari anatakiwa aanzishe chama cha shari na atangaze itikadi zake zote for sure atapata wafuasi, lakini kama CUF wakitaka wabomoe mafanikio kidogo waliyoyapata bara basi wamchague Safari kuwa mwenyekiti.

Bongolander na wengineo;

Prof. Safari mansema ni mdini, mkorofi, ulimi wake ni mto .k ni kwa sababu moja tu, nayo anajiweka wazi kuwa yeye ni MUISLAM wa vitendo tu. Hayo mengine yote ni visingizio, kinachowakera nyinyi na wengineo wote hamtaki mtu aitwae prof, dokta n.k halafu akaweka UISLAM wake wazi. Huyo prof. safari angekuwa mtu wa pombe, totoz, n.k wala asingekuwa ajenda humu jamvini.

Ikumbukwe kuwa huyo bwana ndio wakili mkuu wa kesi zote za kipindi kileee cha kesi za kubambikiwa za Waislamu, alijitolea kuwatetea kwa hali na mali hadi kesi zote zikafutwa maana hakukuwa na ushahidi madhubuti.

Yeyote kati yao akisimama kuwa chair wa CUF bado CUF wamelamba dume all are strong people (Lipumba na Safari)

Kuna mdau m1 huko nyuma alisema CUF hawa organisation yoyote hasa bara; namkumbusha kuwa uchaguzi uliopita walikuwa 2nd na kura nyingi za urais zilitoka bara, je huo c ushahidi tosha wa kuwa nguvu ipo hadi huko milimani na mabondeni?
Jana CUF waliwaalika Wahriri wa vyombo mbalimbali vya habari ktk chakula cha jioni; akizungumza kwa niaba ya wahariri wengine, mhariri mkuu wa habari cooperation alisema "...nawasifu CUF kwa kuwa na oganaizesheni nzuri hapa nchini kuliko vyama vyote, kwa mfano huwezi kukuta kila mtu anaongea kuhusu mambo ya chama, huyu anaongea na huyu anaongea...."

Kuna huyo mwengine Pasco!

Ndio kama ametoka kulala, hivi Maalimu anawakera nini?maana kila cku Maalim atarudisha usultani, atawaleta waarabu, mara hivi... yaani ugoro mtupu!!!! Hivi kwa akili zako na muamko uliopo hivi sasa wa watanzania bado pasco anaamini propaganda za kurudiskwa usultani na mwarabu? Mbona wenye chama chao (ccm) washaachana nayo cku nyingi?maana waliona haina manufaa kwao tena ndio kwaanza anapendwa na watu kila kukcha.

JAMANI ACHENI CHUKI BINAFSI, kama huna cha kuchangia humu jamvinikaa kimya itakuwa kwako ni bora mara elfu zaidi, tusikubali hisia zetu zitutawale. Tufanye utafiti zaidi then tupime mizani.

Thnx
 
Back
Top Bottom