Hivi Tambwe Hiza ni asset? I am trying to think aloud
Ndio. Ana akili inayojitegemea kidogo. Huwezi kumlinganisha na Lipumba na usomi wake!
Safari Ni Mtaalam na asiekubali kuyumbishwa. Akina hamad rashid na wengine hawakumfanyia Uadilifu Prof Safari. Moja ya Sababu ya Prof. Safari kutolewa Chuo cha Diplomasia ni kuwa alikwenda kumhoji prof. Lipumba akiwa Jela. Wakuu wa nchi wakajua jamaa ni CUF, wakamtoa DIPLOMASIA.
Suala la kuandika kitabu ni fani yake, acha aweke wazi Uozo uliopo CUF may be wanaweza kubadilika, msimamo wake wa kimsingi kuwa tofauti yake na akina Seif na Lipumba ni juu ya kusisitiza kuwepo kwa katiba Huru na hilo ndio msimamo wa wadau wengi ambao wanapenda kuona nchi inabadilika. Uelewa wa wajumbe nalo ni Muhimu sana.
Moja ya tatizo la Upinzani ni kukosa wasomi wengi, na wasomi wetu wengi wamekuwa waoga na wengi wao wanaona bora kubakia CCM kulinda maslahi yao. Kuliko Ku-risk maisha yao.
Nimjuavyo hawezi ingia CCM...!!!