Bado hujaziona kweli au unatania mkuu? ok!Picha sijaziona kwani nina usongo wa kulinganisha na malalamiko ya CCM jana!Tuwekee basi tuone.au nawewe ulipewa bahasha jana?
Wakuu samahanini sana niliziweka kumbe kutokana na matatizo ya kimtandao huku zikawa hazijatokea nimemtumia invisible na Mwanakijiji ili waziweke na nyingine nitaweka usiku pamoja na maelezo ya kina .
Mkiziona picha ya kwanza ni ya gari la polisi ambalo lilienda kumchukua diwani aliyekamatwa na kikosi cha CHADEMA jana saa saba usiku akiwa ananunua shahada kwenye kata ya busanda, ya pili ni diwani aliyekakamatwa na ya tatu ni balozi mmoja wapo aliyekamatwa akiwa ananunua shahada na alikutwa na shahada 17 za wananchi na alipohojiwa alisema kuwa wameagizwa na ngazi za juu.
Wameshikiliwa na sasa wametolewa kwa dhamana ila watafikishwa mahakamani.
Nyingine ni za mkutano wa Zitto kata ya Katoro juzi .
Mengine baadae kwanni huku umeme shida na jenereta wanawasha usiku tuu hivyo ni hadi usiku tena.
Lengo la wapinzani ni kupata fursa ya kuongoza serikali na wakifanya jambo lolote la kufanikisha hili lengo shaka hakuna. tatizo linakuja kama wakifanya mambo ambayo ni kinyume na sheria kama mlivyoiba nyie kuiba fedha za umma ili mchaguliwe.....Laana tupu
yes, sasa zinaonekana vizuri. Du kweli Busanda wana hasira, sasa inabidi wakaipigie kura chadema, siyo wafike kwa wingi kwenye mikutano halafu kura waipe CCM. Hapo itakuwa haina maana. Sasa CCM kwisha habari yao. ama kweli ngoma mdundo.Nimerekebisha 1st post na naamini sasa zinaonekana vema.
CCM hawana mbinu mpya, ni zilezile chafu tu ambazo wapinzani wamezigundua na kula nazo sahani moja. Wataumbuka mwakani!!!Polisi waliwasili katika maeneo kadhaa na kufanikiwa kuwatia nguvuni makada wa CCM
Hii ndio kampeni ya nyumba kwa nyumba aliyobuni mzee Tingatinga. hataki majukwaa tena bali ananegotiate na mpiga kura nyumbani kwake. Shahada inathaminishwa mwanangu. Kama we ni wa upinzani na hutaki kupiga kura, unachukua chako mapema na kujikausha. Kwenye mikutano unaongeza idadi ya watu wakati wakaati wa kupiga kura we unaendelea kula vijisent vyoko kutoka kwa mafisadi.
Jamani kama kweli hao watapiga kura basi nahesabu CCM chaliiiiiiiiiiiii dah CHADEMA wamekula vichwa balaaa kitu nyomi kha!