Elections 2010 Uchaguzi 2010: ITV sasa imekuwa chombo cha CCM?

kuna station nyingi tu za tv; kwanini usihame itv na kuangalia station tofauti badala ya kulalamika?
 
Non stop, kuchakachua mpaka mwisho, hata matokeo
Watch out

Bado watanzania siwaamini kabisaaaaa
 
Mbona kituo cha itv kinajulikana......kwa kuto tangaza vichwa vya habari vya baadhi ya magazeti.ukiangalia habari ya saa mbili usiku,inachukua 45 minutes na 20 minutes wanazungumzia na kumtukuza mengi.navipongeza baadhi ya vituo vya tv.naisifu tbc kwa kuonyesha uzalendo kwenye nchi hii na ndio inayoongoza kwa vipindi vya maana na kuelimisha jamii
 
Bado ITV wanaendelea kudhihirisha kwamba wako nyuma ya JK. Leo Ijumaa ktk kipindi cha cha mapitio ya magazeti Joseph Ndamalya hakusoma Mwananchi, Majira, Tanzania Daima ambayo yana vichwa vya habari negative kwa JK -- ile habari ya Slaa kumwekea pingamizi JK.

Kwa hili nawasifu sana Channel 10 kwani wao wamesoma magazeti yote isipokuwa Nipashe ambalo ni kwa sababu zinazojulikana tangu huko nyuma.
 
Wajameni, habarizi za asubuhi. Ni imani yangu kuwa nyote hamjambo.

Nimesikitika sana wakati wa kuangalia kipindi cha magazeti ITV leo saa moja kasoro robo. Isac Gamba aalikuwa na magazeti mengi lakini alisoma vichwa vya habari vinavyozungumzia CCM tuu! Sasa nashindwa kuelewa kama ni kwa mataka yake binafsi kama mpiga kampeni wa CCM, au ni kwa mamlaka ya ITV?

It is so sad!
 
Wana-JF: Leo pia (Jumamosi tarehe 28 August) katika kipindi chake cha mapitio ya magazeti saa moja kasoro dak kumi, msomaji Isaack Gamba wa kituo hicho cha ITV alisoma magazeti yafuatayo tu: Nipashe, Uhuru, Habari Leo na Guardian. haya yote yalikuwa na vichwa vya habari chanya kwa kampeni za CCM.

Magazeti mengine, baadhi yao yametokea kujizolea usomaji mkubwa hivi karibuni kama vile Mwananchi, T. Daima, Majira, Jambo Leo, The Citizen hayakuwapo kabisa. Na kwa ITV sasa hii ndiyo imekuwa trend katika kipindi hiki cha uchaguzi inajitambulisha moja kwa moja inasimamia upande wa CCM. TCRA -- haya siyo matumizi mabaya ya matumizi ya TV uliyoipa liseni kwa ajili ya kuhudumia wananchi wote?
 
Wana-JF: Leo pia (Jumamosi tarehe 28 August) katika kipindi chake cha mapitio ya magazeti saa moja kasoro dak kumi, msomaji Isaack Gamba wa kituo hicho cha ITV alisoma magazeti yafuatayo tu: Nipashe, Uhuru, Habari Leo na Guardian. haya yote yalikuwa na vichwa vya habari chanya kwa kampeni za CCM.

Magazeti mengine, baadhi yao yametokea kujizolea usomaji mkubwa hivi karibuni kama vile Mwananchi, T. Daima, Majira, Jambo Leo, The Citizen hayakuwapo kabisa. Na kwa ITV sasa hii ndiyo imekuwa trend katika kipindi hiki cha uchaguzi inajitambulisha moja kwa moja inasimamia upande wa CCM. TCRA -- haya siyo matumizi mabaya ya matumizi ya TV uliyoipa liseni kwa ajili ya kuhudumia wananchi wote?

TBC wamesoma Habari leo, uhuru na majira(hili limesomwa nusu nusu)

ITV na TBC wanathiilisha kuwa ni wanaCCM
 
Leo asubuhi nimeshtushwa na kituo cha ITV kinachimilikiwa na IPP media pale msomaji wa mapitio ya magazeti aliposoma magazeti kama manne tu -- Nipashe, Uhuru, Habari Leo na Guardian, mengineyo kama vilw Mwananchi, Majira, Tanzania Daima na Mtanmzania hayakusoma kabisa.

Kwa upande wake, kituo cha Channel 10 katika kipindi kama hicho cha saa moja na robo, msomaji Hamis Mkotya alisoma magazeti yote na nikagundua kwamba yale ambayo ITV iliyaacha kusoma kama vile Mwananchi, Tanzania Daima na jambo Leo yalikuwa na habari kubwa kubwa za uzinduzi wa kampeni za Chadema Leo na pia kuhusu pingamizi la Chama hichi dhidi ya mgombea urais wa CCM, JK.

Yaani ghafla ITV imekuwa mpiga debe mkubwa wa kampeni za CCM? Si vyema wajitangaze hivyo tujue? Mimi nilifikiri ITV ni kituo huru cha ITV kumbe ni cha chama tawala? Aibu kubwa hii!!

Nawapa Hongera sana Channel 10, endeleeni na msimamo wenu mliojitambulisha kwamba mko huru.
 
WanaJF kuna thread zinaendelea zikionesha jinsi wafanyakzi wa ITV na TBC wanavyoujumu Habari, lakini kwa mtazamo wangu hawa tutakuwa tunawaonea bure wana wanapokea maelekezo kutoka kwa maboss wao

R Mengi na TIDO kama majasusi ndo wanawalazimisha vyombo vyao viwe na mlengo wa kiCCM
 
TBC hawana haki kufanya hivyo ni chombo cha umma ITV wapo huru kama lilivyo Tanzania Daima na Mwanahilisi !
 
WanaJF kuna thread zinaendelea zikionesha jinsi wafanyakzi wa ITV na TBC wanavyoujumu Habari, lakini kwa mtazamo wangu hawa tutakuwa tunawaonea bure wana wanapokea maelekezo kutoka kwa maboss wao

R Mengi na TIDO kama majasusi ndo wanawalazimisha vyombo vyao viwe na mlengo wa kiCCM

Mkuu mbona mwandiko wako hausomeki vizuri ulikuwa unatype huku unadrive au ulikuwa umetoka usingizini?
 
Huyu Mengi si ndiye alitangaza mafisadi papa na akina Mkuchika, Sofdia Simba na TCRA walimjia juu? Alipata sapoti kubwa kutoka kwa wananchi wengine na vyombo vingine vya habari, kwani mafisadi papa hap baadhi yao kweli walitinga mahakamani. Alitaja mafisadi papa kwa sababu aliona CCM haiwashugulikii vilivyo. lakini atambue kwamba hao mafisadi papa aliowatangaza ni wale wale aliotangaza Mpiganaji wetu, Dr Slaa kule Membe Yanga mwaka 2007.

Jee leo hii anaona akina Slaa hawafai kupigana na ufisadi isipokuwa CCM? Haoni kama CCM imeshindwa kupigana na kansa hii isipokuwa inafanya ujanjaujanja tu usanii kwa wananchi? Kama haoni hayo, then there is something very wrong with him.

Polepole naanza kutokwa imani na Mzee huyu, nilmuona ni mmojawapo as true sons of this country, kumbe ni just one of them!! Oh yes, he is!!! Shame on him for betraying the masses that had held you in high esteem!!!!
 
TBC hawana haki kufanya hivyo ni chombo cha umma ITV wapo huru kama lilivyo Tanzania Daima na Mwanahilisi !
nkubaliana na wewe kwa asilimia zote mkuu.
TBC hawana haki ya kuelemea chama kimoja kwa sababu ni tv ya Taifa ipo kwa manufaa ya Taifa na si chama.
 
Ndugu zangu,

Kulalamika tu humu kwenye jamii forums haitoshi, inabidi tuwaandikie barua NYINGI za kuwaonya uongozi wa ITV KUACHA mara moja kuwachagulia watanzanzania habari wanazozitaka wao na kuacha unafki wa kujipendekeza kwa JK kwani huo ni ufisadi wa hhabari, Tuandikene barua pepe na barua za kawaida kwenda kwa ITV sasa hivi kwenye email zifuatazo info@itv.co.tz , admin@itv.co.tz , ITV@ipp.co.tz or call them out right now on +255 (0)22 277 5914 / 5916 or send them a letter on Mikocheni Light Industrial Area, Plot 82 A
P.O. Box 4374
City Dar Es Salaam
Country Tanzania
 
TBC hawana haki kufanya hivyo ni chombo cha umma ITV wapo huru kama lilivyo Tanzania Daima na Mwanahilisi !
Ni kweli ITV ni chombo huru, ila tatizo liko kwa Mmiliki wake maana siku zote anataka kutuaminisha kuwa ni mtetezi wa wanyonge,mpiga vita rushwa na ufisadi hasa ufisadi papa, na muumini mzuri wa haki za binadamu pia mcha Mungu. Sasa iweje aviamrishe (kama ni hivyo) vyombo vyake vya habari viwatete na kuwanadi kwa nguvu zote wale waendao kinyume na hayo anayotuaminisha kuwa ndiyo anayofuata? Na wale waletao njia mbadala za kumkomboa Mtanzania kama asemavyo yeye hawapi nafasi ya kutosha? Imani yangu kwake inaanza kutoweka. Na ninadhani siko peke yangu.
 
Leo asubuhi nimeshtushwa na kituo cha ITV kinachimilikiwa na IPP media pale msomaji wa mapitio ya magazeti aliposoma magazeti kama manne tu -- Nipashe, Uhuru, Habari Leo na Guardian, mengineyo kama vilw Mwananchi, Majira, Tanzania Daima na Mtanmzania hayakusomwa kabisa.

Kwa upande wake, kituo cha Channel 10 katika kipindi kama hicho cha saa moja na robo, msomaji Hamis Mkotya alisoma magazeti yote na nikagundua kwamba yale ambayo ITV iliyaacha kusoma kama vile Mwananchi, Tanzania Daima na jambo Leo yalikuwa na habari kubwa kubwa za uzinduzi wa kampeni za Chadema Leo na pia kuhusu pingamizi la Chama hichi dhidi ya mgombea urais wa CCM, JK.

Yaani ghafla ITV imekuwa mpiga debe mkubwa wa kampeni za CCM? Si vyema wajitangaze hivyo tujue? Mimi nilifikiri ITV ni kituo huru cha ITV kumbe ni cha chama tawala? Aibu kubwa hii!!

Nawapa Hongera sana Channel 10, endeleeni na msimamo wenu mliojitambulisha kwamba mko huru.
Mkuu naona huwa huangalii Chanel 10 mara kwa mara.
Nao ni wanafki kama ITV, TBC1 na Star Tv.
Angalia taharifa za habari za Chanel 10 ndio utagundua kuwa na wao n vibaraka wa CCM.
 
Ndugu zangu,

Kulalamika tu humu kwenye jamii forums haitoshi, inabidi tuwaandikie barua NYINGI za kuwaonya uongozi wa ITV KUACHA mara moja kuwachagulia watanzanzania habari wanazozitaka wao na kuacha unafki wa kujipendekeza kwa JK kwani huo ni ufisadi wa hhabari, Tuandikene barua pepe na barua za kawaida kwenda kwa ITV sasa hivi kwenye email zifuatazo info@itv.co.tz , admin@itv.co.tz , ITV@ipp.co.tz or call them out right now on +255 (0)22 277 5914 / 5916 or send them a letter on Mikocheni Light Industrial Area, Plot 82 A
P.O. Box 4374
City Dar Es Salaam
Country Tanzania

Hali kadhalika TBC tuwaandikie maoni yetu sasa hivi Kijitonyama, Off Bagamoyo Road
P.O. Box 31519
City Dar Es Salaam
Country Tanzania
Telephone +255 (0)22 2700 011 / 062
Telefax +255 (0)22 2700 468
Email tvt-dg@africaonline.co.tz
 
Something more than can meet the eye!! hivi mliona uzinduzi wa Kampeni za CUF ulivyo onyeshwa IN DETAILS NA TBC. Kwa wale mliongalia taarifa ya habari jana Kupitia TBC mtakubaliana na mimi.
Hiki chombe kweli ni sisiemu. nasema na sitaogopa. Wanajua kabisa Lipumba hana Nguvu ya Slaa. Wanapompa Lipumba Nguvu ambaye wanajua kabisa nafasi yake ya kuchukua Uraisi ni sawa na ngamia kupita katika Tundu la sindano, Ni njama ya kugawa kura za Upinzani ili chama tawala kipite kilaini.
Na pia nimeanza kuamini linaloongelewa kuhusu ndoa ya CCM na CUF na lengo lao ni nini!
For your information guys, Watanzania we are gone. Mbinu chafu za CCM zimeshatu overtake. Nyie CCM endeleeni kututesa tu. Lakini ipo siku Tu.
 
TBC ni shirika la umma lipo kwa maslai ya umma,linaendeshwa kwa kodi za wananchi,wala si kitengo cha CCM wala CHADEMA.Kushindwa kufanya kazi yake ya msingi ya kutoa habari hata kama habari haziwapendezi watawala ni kukiuka maadili ya Uandishi.Ikifika wakati kinatoa habari za kupendelea sehemu mmoja,kiwajibishwe ipasavyo.
Kwa ITV hiyo haitabiliki,habari hutolewa zile anazotaka mmliki,yeye anaangalia maslahi yake,ukienda kinyume umeumia kama wengi walivyoumia.
TBC na ITV wanashindwa kutoa habari kwa sababu ya kuogopa watu waliowapa nyazifa hizo.
 
Back
Top Bottom