Uchadema Wamfanya Malisa atukane KKKT

Uchadema Wamfanya Malisa atukane KKKT

Hakuna mahali Malisa ametukana, pengine UCHAWA na UCCM wako umesababisha ushindwe kumuelewa. Nakurejeshea tena alichoandika ili usome na kuelewa:-
Shalom Baba Askofu Malasusa. Mimi ni Mlutheri kwa damu na nafsi (Lutheran by blood and soul). Mizizi yangu katika Ulutheri ni imara sana. Lakini nimekuzwa KIAKILI na Kanisa Katoliki. Nimesoma shule zao, vyuo vyao na nimefanya kazi na baadhi ya mashirika yao ya kitume.
Hata hivyo IMANI yangu kwa Kristo imekuzwa na Makanisa ya Kipentekoste. Nimeshiriki semina, mikutano na ibada zao. Mwaka 1999 nikiwa darasa la 6 nilikua natembea kwa miguu kutoka nyumbani Kidia hadi viwanja vya Mashujaa kusikiliza mahubiri ya Mwinjilisti Reinhard Bonnke.
Hii ni kusema kwamba pamoja na Ulutheri wangu wenye mizizi, lakini nayaheshimu madhehebu yote ya Kikristo yanayohubiri katika ROHO na KWELI.
Leo Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) limetoa tamko kulaani vitendo vya utekaji na mauaji nchini. Tamko hili limetolewa mbele ya viongozi wakuu wa serikali. Kuna makanisa yakiwaona viongozi wa serikali point zote za kukosoa zina-evaporate, wanaishia kujichekesha na kusifia. Lakini si kanisa katoliki, kamwe. Katoliki hata umuite Askofu Ikulu, atakuja, atakunywa juice yako na "atakuchana" bila kupepesa macho.
Kwa mujibu wa International Church Index 2022, KKKT ni Kanisa la pili kwa ukubwa nchini baada ya Katoliki. Maana yake ni Kanisa lenye nguvu na lenye sauti. Je lini litatumia sauti hiyo kukemea maovu yanayoendelea? Kanisa linawezaje kuona mtu akishushwa kwenye basi na kuuawa kikatili na likakaa kimya?
Baba yetu Martin Luther alitufundisha tunaokolewa kwa neema (Sola Gratia). Neema si kwa Walutheri pekee bali kwa watu wote. Ndio maana katika Kateksimo yake aliandika "Et alias oves habeo" akimaanisha na kondoo wengine ninao ambao si wa zizi hili. Nao wanastahili neema (Yohana 10:16). Ikitokea mtu ameuawa awe Mkristo, Muislamu, Mpagani etc, Kanisa lina wajibu wa kukemea.
Baba Askofu Shoo alipokua mkuu wa Kanisa, alikemea matukio yote maovu bila hofu. Bila shaka angekuwepo madarakani angeshatoa waraka wa kukemea utekaji na mauaji.
Tunaomba usimzimishe roho aliyekua na Kanisa kipindi cha Askofu Shoo. Lisimamie Kanisa libaki kwenye misingi yake. Tunaomba tamko la KKKT kulaani watu kutekwa na kuuawa. Tamko hilo litaokoa roho nyingi ambazo zimepangwa kuangamizwa na waovu. Mungu akubariki
asante kwa kutuhabarisha a;lichokiandika Malisa.
Anyway malasusa ni CCM, yuko hivi kichwani:
1726472566323.png
 

Attachments

  • 1726472477087.png
    1726472477087.png
    518.4 KB · Views: 18
  • 1726472597430.png
    1726472597430.png
    1 MB · Views: 21
Godlisten Malisa amemwaga tuhuma kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania na kejeli kwa baba askofu mkuu Alex Malasusa. Mimi ambaye siyo mlutheri bali Mkatoliki ninayeelewa matamko yaliyowahi kutolewa na KKKT tena askofu Malasusa akiwa kiongozi ama sehemu ya uongozi, na nikifahamu mchakato wa utaratibu wa kutoa tamko la kitaifa kwa KKKT, nimeona nitoe ufafanuzi huu, ili kusahihisha upotoshaji aliofanya Malisa kwa sababu ya mihemko ya kisiasa.

KKKT imekuwa mstari wa mbele kuikumbusha serikali umuhimu wa utawala bora na kuheshimu demokrasia. Kanisa lilitoa tamko wakati wa uchaguzi wa 2015 na 2020, likisisitiza haki za raia kupiga kura kwa uhuru na uwazi bila vitisho. Kanisa lilitaka serikali kuhakikisha kuwa vyombo vya dola haviingilii mchakato wa uchaguzi na kwamba haki za vyama vya upinzani zinaheshimiwa.

KKKT lilitoa matamko kuhusu kuzuia uhuru wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wanaharakati wa kijamii. Lilieleza wasiwasi wake juu ya sheria kandamizi, kama vile Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ya 2016, ambayo ilionekana kuzuia uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza. Kanisa lilisisitiza kuwa uhuru wa kujieleza ni haki ya msingi katika jamii yoyote ya kidemokrasia na kuitaka serikali iendeleze mazungumzo na vyombo vya habari badala ya kutumia nguvu za kisheria kuvidhibiti.

Kanisa limekuwa likikosoa mienendo ya serikali katika kushughulikia masuala ya haki za binadamu. Tamko muhimu lilitolewa mwaka 2017, ambapo KKKT ilionesha wasiwasi wake kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kupotea kwa watu, utekaji nyara, na ukandamizaji wa haki za kiraia. Kanisa liliitaka serikali kuchunguza matukio hayo na kuwajibisha waliohusika.

KKKT mara nyingi imekuwa ikihimiza amani na utulivu, hasa wakati wa matukio ya kisiasa yenye mvutano mkubwa. Wakati wa uchaguzi wa 2020, kanisa lilitoa tamko likihimiza wanasiasa na serikali kujiepusha na ghasia na vitendo vya uchochezi vinavyoweza kuvuruga amani ya nchi. Lilionya dhidi ya matumizi ya vyombo vya usalama kwa manufaa ya kisiasa.

Mwaka 2017-2018, KKKT Ilikwisha kutoa tamko lake zito kama Kanisa juu ya matendo haya ya utekaji na watu kupotea. Sasa anayeilaumu KKKT eti siyo kama Katoliki mara sijui haitoi matamko si ni mjinga tu kama wajinga wengine.

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) lina utaratibu maalum wa kutoa matamko katika ngazi ya kitaifa. Huu ni mchakato wa kimfumo na unaofuata taratibu za uongozi na mawasiliano ya ndani ya kanisa. Hatua muhimu katika mchakato huo ni kama ifuatavyo:

Utambuzi wa Tatizo au Suala. Kwanza, viongozi wa KKKT wanatambua suala linalohitaji tamko la kitaifa, ambalo linaweza kuwa la kijamii, kisiasa, kimaadili, au kidini. Suala hili linaweza kutambuliwa kupitia njia mbalimbali:
Ripoti kutoka kwa wachungaji au maaskofu wa dayosisi.

Malalamiko au maoni kutoka kwa waumini.

Ufuatiliaji wa hali ya kisiasa na kijamii nchini.

Ripoti za vyombo vya habari kuhusu masuala yanayoathiri haki za binadamu au ustawi wa jamii.

Mashauriano Ndani ya Uongozi wa Kanisa.
Baada ya suala kutambuliwa, hatua inayofuata ni mashauriano miongoni mwa viongozi wa kanisa. Hapa, maaskofu wa dayosisi mbalimbali na viongozi wengine wa ngazi ya juu wa KKKT hujadili suala husika ili kupata uelewa wa kina. Mikutano ya ndani inaweza kufanyika katika ngazi ya Dayosisi au Sinodi Kuu, ambapo viongozi wa kanisa wanapata nafasi ya kujadili na kutoa maoni yao juu ya suala lililojitokeza.

Baraza Kuu la KKKT, ambalo ni chombo cha juu cha uamuzi ndani ya kanisa, hujadili na kuamua kama tamko linahitajika kutolewa. Baraza hili linajumuisha:

Askofu Mkuu wa KKKT.

Maaskofu wa dayosisi mbalimbali.

Wajumbe wa sinodi za dayosisi.

Wawakilishi wa vyama vya makanisa ndani ya KKKT.
Katika kikao cha Baraza Kuu, suala linajadiliwa kwa kina, na hatua ya kutoa tamko inaweza kupitishwa kwa maamuzi ya pamoja. Ikiwa ni suala lenye umuhimu wa kitaifa, Baraza Kuu linaweza kuunda kamati ndogo ya kuandaa tamko rasmi.

Baada ya uamuzi kufanyika kwamba tamko linahitajika, kamati ndogo ya viongozi wa KKKT au sekretarieti kuu ya kanisa huandaa rasimu ya tamko. Rasimu hiyo inajumuisha msimamo wa kanisa kuhusu suala lililojadiliwa, mapendekezo ya kanisa kwa serikali au umma, na wito wa kimaadili kwa viongozi na jamii kwa ujumla.

Mara baada ya rasimu ya tamko kuandaliwa, inawasilishwa tena kwa uongozi wa juu wa KKKT kwa ajili ya kuthibitishwa. Viongozi wa kanisa wanahakikisha kuwa tamko hilo linaendana na mafundisho ya dini, maadili ya Kikristo, na malengo ya kanisa. Pia, wanahakikisha kwamba lugha inayotumika ni ya hekima, heshima, na inayozingatia hali ya kijamii na kisiasa ya wakati huo.

Baada ya kuthibitishwa, tamko hutangazwa kwa umma. Hii inaweza kufanyika kwa njia mbalimbali:

Kupitia mkutano wa waandishi wa habari ambapo Askofu Mkuu wa KKKT au viongozi wengine waandamizi wanatangaza tamko rasmi kwa vyombo vya habari.

Tamko linaweza kusambazwa kwa njia ya maandishi kwa dayosisi zote, makanisa, na vyombo vya habari ili kuwafikia waumini na umma kwa ujumla.

Viongozi wa KKKT wanaweza kutumia jukwaa la mikutano ya kidini au matukio maalum kama vile Sinodi Kuu au hafla za kitaifa za kanisa kutangaza tamko hilo rasmi.

Baada ya tamko kutolewa, KKKT inaweza kuchukua hatua za ufuatiliaji kuhakikisha kuwa serikali au wadau wengine wanaolengwa wanachukua hatua stahiki. Kanisa linaweza pia kuendelea kuzungumzia suala hilo kupitia vyombo vya habari, mikutano ya kidini, au mawasiliano na viongozi wa kisiasa na kijamii. Utetezi huu ni sehemu ya dhamira ya KKKT ya kuhakikisha masuala ya kijamii na haki za binadamu yanazingatiwa ipasavyo.Kwa ujumla, mchakato wa kutoa tamko katika KKKT ni wa uwazi na wa kimfumo, ukihusisha hatua za mashauriano, tathmini ya kina, na uandaaji wa taarifa rasmi, huku ukilenga kutoa mwongozo wa kimaadili na kijamii.

Ni makosa na utovu wa uchaji kwa Malisa ambaye ni muumini wa KKKT na ambaye amejitabahisha kuwa mchambuzi kutaka KKKT itoe tamko eti kwa sababu TEC imetoa tamko.. Nikosa na kujiongoza vibaya kwa Malisa kutaka askofu mkuu Malasusa aamke na kukimbia kutoa tamko eti kwa sababu kaona TEC wametoa tamko. Malisa alipaswa kufahamu "rationale" Na "procedure" Ya kutoa tamko la kitaifa la KKKT.

KKKT ilikwisha kutoa tamko zito kabisa juu ya matukio ya watu kutekwa na kupotea. Ikiwa bado wanafuatilia utekelezaji na hatua gani wataamua baada ya matukio hayo kuonekana bado yangalipo ni suala la utaratibu wa ndani wa KKKT ambao Malisa anapaswa kuwa anaufahamu. Tunamsihi Malisa, Mihemko yake kisiasa isiwe juu ya imani yake ya dini. Ataharibikiwa.
Labda sijui maana ya Matusi...Embu yaeleze Matusi aliyotukana tuyaone
 
Kwa nini yalizaliwa madhehebu lukuki?, Kanisa haliondoshwi kama chama cha siasa, Isipokuwa linazaliwa lingine kuimarisha mapungufu.
Kwahiyo mapungufu hayawei kurekebishwa mpaka yazaliwe mengine? Yanazaliwa kwa ruhusa ya nani? Yesu? Kwa andiko lipi? Fallacy! (a mistaken belief, especially one based on unsound arguments.)
 
ndilo hilo aliliacha Rome kwa Papa (Pope) as per catholic teachings. I stand to be corrected
Peter aliacha kwa papal? Mafundisho, hadithi unayohadithi ni ya juzi tu, je Constantine alikuwa ni nani?

Jesus Christ is quoting a scripture from the Hebrew part of the Bible. Research will help you to see that he quoted Deuteronomy 6:13
 
KKKT ILISHATOA TAMKO MWAKA 2017-2018 NA NDILO TAMKO LINALOISHI MPAKA LEO HII, HATUWEZI KUWA NA MADHEHEBU YA MATAMKO KILA WAKATI, WALA SI HEKIMA KURUDIA MATAMKO YALE YALE KILA WAKATI, NA HUU NDIYO UDHABITI WA DHEHEBU.
WANASIASA UCHWARA WASIYAGEUZE MADHEHEBU YETU KAMA NYUMBA ZA SIASA, NA NDILO WANALOKUSUDIA WE SAY NO!
Ni kukosa maarifa kwa kiwango cha hali ya juu sana, kuamini kuwa kukemea uovu, ni siasa. Kuteka na kuua watu kunakofanywa na vyombo vya Serikali ni uovu wa hali ya juu. Wanasiasa wanatakiwa kupaza sauti. Watu wa dini wanatakiwa kupaza sauti kwa sababu jambo hili ni uovu. Wanasheria wanatakiwa kupaza sauti kwa sababu uovu huu unakiuka haki za msingi za kibinadamu. Wanadiplomasia wanatakiwa kupaza sauti kwa sababu ushetani huu unaofanywa na vyombo vya Setikali ya Tanzania, unakiuka maazimio mbalimbali ya umoja wa mataifa.

Ni Punguani na mwendawazimu pekee anaweza kufikiria kuwa kupaza sauti dhidi ya uharamia huu wa kutekwa na kuuawa watu wanaoikosoa Serikali na Rais , ni suala la wanasiasa pekee yao.

Nchi yetu, na hasa CCM, wana bahati mbaya sana ya kuwa na mapunguani na wajinga wengi wasioelewa chochote lakini wanajifanya wana uelewa.
 
Godlisten Malisa amemwaga tuhuma kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania na kejeli kwa baba askofu mkuu Alex Malasusa. Mimi ambaye siyo mlutheri bali Mkatoliki ninayeelewa matamko yaliyowahi kutolewa na KKKT tena askofu Malasusa akiwa kiongozi ama sehemu ya uongozi, na nikifahamu mchakato wa utaratibu wa kutoa tamko la kitaifa kwa KKKT, nimeona nitoe ufafanuzi huu, ili kusahihisha upotoshaji aliofanya Malisa kwa sababu ya mihemko ya kisiasa.

KKKT imekuwa mstari wa mbele kuikumbusha serikali umuhimu wa utawala bora na kuheshimu demokrasia. Kanisa lilitoa tamko wakati wa uchaguzi wa 2015 na 2020, likisisitiza haki za raia kupiga kura kwa uhuru na uwazi bila vitisho. Kanisa lilitaka serikali kuhakikisha kuwa vyombo vya dola haviingilii mchakato wa uchaguzi na kwamba haki za vyama vya upinzani zinaheshimiwa.

KKKT lilitoa matamko kuhusu kuzuia uhuru wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wanaharakati wa kijamii. Lilieleza wasiwasi wake juu ya sheria kandamizi, kama vile Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ya 2016, ambayo ilionekana kuzuia uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza. Kanisa lilisisitiza kuwa uhuru wa kujieleza ni haki ya msingi katika jamii yoyote ya kidemokrasia na kuitaka serikali iendeleze mazungumzo na vyombo vya habari badala ya kutumia nguvu za kisheria kuvidhibiti.

Kanisa limekuwa likikosoa mienendo ya serikali katika kushughulikia masuala ya haki za binadamu. Tamko muhimu lilitolewa mwaka 2017, ambapo KKKT ilionesha wasiwasi wake kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kupotea kwa watu, utekaji nyara, na ukandamizaji wa haki za kiraia. Kanisa liliitaka serikali kuchunguza matukio hayo na kuwajibisha waliohusika.

KKKT mara nyingi imekuwa ikihimiza amani na utulivu, hasa wakati wa matukio ya kisiasa yenye mvutano mkubwa. Wakati wa uchaguzi wa 2020, kanisa lilitoa tamko likihimiza wanasiasa na serikali kujiepusha na ghasia na vitendo vya uchochezi vinavyoweza kuvuruga amani ya nchi. Lilionya dhidi ya matumizi ya vyombo vya usalama kwa manufaa ya kisiasa.

Mwaka 2017-2018, KKKT Ilikwisha kutoa tamko lake zito kama Kanisa juu ya matendo haya ya utekaji na watu kupotea. Sasa anayeilaumu KKKT eti siyo kama Katoliki mara sijui haitoi matamko si ni mjinga tu kama wajinga wengine.

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) lina utaratibu maalum wa kutoa matamko katika ngazi ya kitaifa. Huu ni mchakato wa kimfumo na unaofuata taratibu za uongozi na mawasiliano ya ndani ya kanisa. Hatua muhimu katika mchakato huo ni kama ifuatavyo:

Utambuzi wa Tatizo au Suala. Kwanza, viongozi wa KKKT wanatambua suala linalohitaji tamko la kitaifa, ambalo linaweza kuwa la kijamii, kisiasa, kimaadili, au kidini. Suala hili linaweza kutambuliwa kupitia njia mbalimbali:
Ripoti kutoka kwa wachungaji au maaskofu wa dayosisi.

Malalamiko au maoni kutoka kwa waumini.

Ufuatiliaji wa hali ya kisiasa na kijamii nchini.

Ripoti za vyombo vya habari kuhusu masuala yanayoathiri haki za binadamu au ustawi wa jamii.

Mashauriano Ndani ya Uongozi wa Kanisa.
Baada ya suala kutambuliwa, hatua inayofuata ni mashauriano miongoni mwa viongozi wa kanisa. Hapa, maaskofu wa dayosisi mbalimbali na viongozi wengine wa ngazi ya juu wa KKKT hujadili suala husika ili kupata uelewa wa kina. Mikutano ya ndani inaweza kufanyika katika ngazi ya Dayosisi au Sinodi Kuu, ambapo viongozi wa kanisa wanapata nafasi ya kujadili na kutoa maoni yao juu ya suala lililojitokeza.

Baraza Kuu la KKKT, ambalo ni chombo cha juu cha uamuzi ndani ya kanisa, hujadili na kuamua kama tamko linahitajika kutolewa. Baraza hili linajumuisha:

Askofu Mkuu wa KKKT.

Maaskofu wa dayosisi mbalimbali.

Wajumbe wa sinodi za dayosisi.

Wawakilishi wa vyama vya makanisa ndani ya KKKT.
Katika kikao cha Baraza Kuu, suala linajadiliwa kwa kina, na hatua ya kutoa tamko inaweza kupitishwa kwa maamuzi ya pamoja. Ikiwa ni suala lenye umuhimu wa kitaifa, Baraza Kuu linaweza kuunda kamati ndogo ya kuandaa tamko rasmi.

Baada ya uamuzi kufanyika kwamba tamko linahitajika, kamati ndogo ya viongozi wa KKKT au sekretarieti kuu ya kanisa huandaa rasimu ya tamko. Rasimu hiyo inajumuisha msimamo wa kanisa kuhusu suala lililojadiliwa, mapendekezo ya kanisa kwa serikali au umma, na wito wa kimaadili kwa viongozi na jamii kwa ujumla.

Mara baada ya rasimu ya tamko kuandaliwa, inawasilishwa tena kwa uongozi wa juu wa KKKT kwa ajili ya kuthibitishwa. Viongozi wa kanisa wanahakikisha kuwa tamko hilo linaendana na mafundisho ya dini, maadili ya Kikristo, na malengo ya kanisa. Pia, wanahakikisha kwamba lugha inayotumika ni ya hekima, heshima, na inayozingatia hali ya kijamii na kisiasa ya wakati huo.

Baada ya kuthibitishwa, tamko hutangazwa kwa umma. Hii inaweza kufanyika kwa njia mbalimbali:

Kupitia mkutano wa waandishi wa habari ambapo Askofu Mkuu wa KKKT au viongozi wengine waandamizi wanatangaza tamko rasmi kwa vyombo vya habari.

Tamko linaweza kusambazwa kwa njia ya maandishi kwa dayosisi zote, makanisa, na vyombo vya habari ili kuwafikia waumini na umma kwa ujumla.

Viongozi wa KKKT wanaweza kutumia jukwaa la mikutano ya kidini au matukio maalum kama vile Sinodi Kuu au hafla za kitaifa za kanisa kutangaza tamko hilo rasmi.

Baada ya tamko kutolewa, KKKT inaweza kuchukua hatua za ufuatiliaji kuhakikisha kuwa serikali au wadau wengine wanaolengwa wanachukua hatua stahiki. Kanisa linaweza pia kuendelea kuzungumzia suala hilo kupitia vyombo vya habari, mikutano ya kidini, au mawasiliano na viongozi wa kisiasa na kijamii. Utetezi huu ni sehemu ya dhamira ya KKKT ya kuhakikisha masuala ya kijamii na haki za binadamu yanazingatiwa ipasavyo.Kwa ujumla, mchakato wa kutoa tamko katika KKKT ni wa uwazi na wa kimfumo, ukihusisha hatua za mashauriano, tathmini ya kina, na uandaaji wa taarifa rasmi, huku ukilenga kutoa mwongozo wa kimaadili na kijamii.

Ni makosa na utovu wa uchaji kwa Malisa ambaye ni muumini wa KKKT na ambaye amejitabahisha kuwa mchambuzi kutaka KKKT itoe tamko eti kwa sababu TEC imetoa tamko.. Nikosa na kujiongoza vibaya kwa Malisa kutaka askofu mkuu Malasusa aamke na kukimbia kutoa tamko eti kwa sababu kaona TEC wametoa tamko. Malisa alipaswa kufahamu "rationale" Na "procedure" Ya kutoa tamko la kitaifa la KKKT.

KKKT ilikwisha kutoa tamko zito kabisa juu ya matukio ya watu kutekwa na kupotea. Ikiwa bado wanafuatilia utekelezaji na hatua gani wataamua baada ya matukio hayo kuonekana bado yangalipo ni suala la utaratibu wa ndani wa KKKT ambao Malisa anapaswa kuwa anaufahamu. Tunamsihi Malisa, Mihemko yake kisiasa isiwe juu ya imani yake ya dini. Ataharibikiwa.
Hawa akina Godlisten Malisa ni aina ya watu waliokosa "guidance"....

Kukosa "mwongozo mwema" hukufanya kuiona elimu uliyonayo ni silaha ya kiliberali juu ya kila kitu....mtazamo mbovu na hasi wa kitaaluma......

Elimu bila busara ni sawa na "empty vessel".....

Busara busara busara busara

Waliberali wa kizazi hichi kila jambo hulipima kwa rejea ya waliberali wa kizungu ,hisia na mitazamo yao.......

#KKTT ni taasisi kubwa haikurupuki😍😍
 
Peter aliacha kwa papal? Mafundisho, hadithi unayohadithi ni ya juzi tu, je Constantine alikuwa ni nani?

Jesus Christ is quoting a scripture from the Hebrew part of the Bible. Research will help you to see that he quoted Deuteronomy 6:13
Mafundisho niliyonayo ni hivyo. hata huyo costantine ni descendant wa Peter
 
Godlisten Malisa amemwaga tuhuma kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania na kejeli kwa baba askofu mkuu Alex Malasusa. Mimi ambaye siyo mlutheri bali Mkatoliki ninayeelewa matamko yaliyowahi kutolewa na KKKT tena askofu Malasusa akiwa kiongozi ama sehemu ya uongozi, na nikifahamu mchakato wa utaratibu wa kutoa tamko la kitaifa kwa KKKT, nimeona nitoe ufafanuzi huu, ili kusahihisha upotoshaji aliofanya Malisa kwa sababu ya mihemko ya kisiasa.

KKKT imekuwa mstari wa mbele kuikumbusha serikali umuhimu wa utawala bora na kuheshimu demokrasia. Kanisa lilitoa tamko wakati wa uchaguzi wa 2015 na 2020, likisisitiza haki za raia kupiga kura kwa uhuru na uwazi bila vitisho. Kanisa lilitaka serikali kuhakikisha kuwa vyombo vya dola haviingilii mchakato wa uchaguzi na kwamba haki za vyama vya upinzani zinaheshimiwa.

KKKT lilitoa matamko kuhusu kuzuia uhuru wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wanaharakati wa kijamii. Lilieleza wasiwasi wake juu ya sheria kandamizi, kama vile Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ya 2016, ambayo ilionekana kuzuia uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza. Kanisa lilisisitiza kuwa uhuru wa kujieleza ni haki ya msingi katika jamii yoyote ya kidemokrasia na kuitaka serikali iendeleze mazungumzo na vyombo vya habari badala ya kutumia nguvu za kisheria kuvidhibiti.

Kanisa limekuwa likikosoa mienendo ya serikali katika kushughulikia masuala ya haki za binadamu. Tamko muhimu lilitolewa mwaka 2017, ambapo KKKT ilionesha wasiwasi wake kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kupotea kwa watu, utekaji nyara, na ukandamizaji wa haki za kiraia. Kanisa liliitaka serikali kuchunguza matukio hayo na kuwajibisha waliohusika.

KKKT mara nyingi imekuwa ikihimiza amani na utulivu, hasa wakati wa matukio ya kisiasa yenye mvutano mkubwa. Wakati wa uchaguzi wa 2020, kanisa lilitoa tamko likihimiza wanasiasa na serikali kujiepusha na ghasia na vitendo vya uchochezi vinavyoweza kuvuruga amani ya nchi. Lilionya dhidi ya matumizi ya vyombo vya usalama kwa manufaa ya kisiasa.

Mwaka 2017-2018, KKKT Ilikwisha kutoa tamko lake zito kama Kanisa juu ya matendo haya ya utekaji na watu kupotea. Sasa anayeilaumu KKKT eti siyo kama Katoliki mara sijui haitoi matamko si ni mjinga tu kama wajinga wengine.

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) lina utaratibu maalum wa kutoa matamko katika ngazi ya kitaifa. Huu ni mchakato wa kimfumo na unaofuata taratibu za uongozi na mawasiliano ya ndani ya kanisa. Hatua muhimu katika mchakato huo ni kama ifuatavyo:

Utambuzi wa Tatizo au Suala. Kwanza, viongozi wa KKKT wanatambua suala linalohitaji tamko la kitaifa, ambalo linaweza kuwa la kijamii, kisiasa, kimaadili, au kidini. Suala hili linaweza kutambuliwa kupitia njia mbalimbali:
Ripoti kutoka kwa wachungaji au maaskofu wa dayosisi.

Malalamiko au maoni kutoka kwa waumini.

Ufuatiliaji wa hali ya kisiasa na kijamii nchini.

Ripoti za vyombo vya habari kuhusu masuala yanayoathiri haki za binadamu au ustawi wa jamii.

Mashauriano Ndani ya Uongozi wa Kanisa.
Baada ya suala kutambuliwa, hatua inayofuata ni mashauriano miongoni mwa viongozi wa kanisa. Hapa, maaskofu wa dayosisi mbalimbali na viongozi wengine wa ngazi ya juu wa KKKT hujadili suala husika ili kupata uelewa wa kina. Mikutano ya ndani inaweza kufanyika katika ngazi ya Dayosisi au Sinodi Kuu, ambapo viongozi wa kanisa wanapata nafasi ya kujadili na kutoa maoni yao juu ya suala lililojitokeza.

Baraza Kuu la KKKT, ambalo ni chombo cha juu cha uamuzi ndani ya kanisa, hujadili na kuamua kama tamko linahitajika kutolewa. Baraza hili linajumuisha:

Askofu Mkuu wa KKKT.

Maaskofu wa dayosisi mbalimbali.

Wajumbe wa sinodi za dayosisi.

Wawakilishi wa vyama vya makanisa ndani ya KKKT.
Katika kikao cha Baraza Kuu, suala linajadiliwa kwa kina, na hatua ya kutoa tamko inaweza kupitishwa kwa maamuzi ya pamoja. Ikiwa ni suala lenye umuhimu wa kitaifa, Baraza Kuu linaweza kuunda kamati ndogo ya kuandaa tamko rasmi.

Baada ya uamuzi kufanyika kwamba tamko linahitajika, kamati ndogo ya viongozi wa KKKT au sekretarieti kuu ya kanisa huandaa rasimu ya tamko. Rasimu hiyo inajumuisha msimamo wa kanisa kuhusu suala lililojadiliwa, mapendekezo ya kanisa kwa serikali au umma, na wito wa kimaadili kwa viongozi na jamii kwa ujumla.

Mara baada ya rasimu ya tamko kuandaliwa, inawasilishwa tena kwa uongozi wa juu wa KKKT kwa ajili ya kuthibitishwa. Viongozi wa kanisa wanahakikisha kuwa tamko hilo linaendana na mafundisho ya dini, maadili ya Kikristo, na malengo ya kanisa. Pia, wanahakikisha kwamba lugha inayotumika ni ya hekima, heshima, na inayozingatia hali ya kijamii na kisiasa ya wakati huo.

Baada ya kuthibitishwa, tamko hutangazwa kwa umma. Hii inaweza kufanyika kwa njia mbalimbali:

Kupitia mkutano wa waandishi wa habari ambapo Askofu Mkuu wa KKKT au viongozi wengine waandamizi wanatangaza tamko rasmi kwa vyombo vya habari.

Tamko linaweza kusambazwa kwa njia ya maandishi kwa dayosisi zote, makanisa, na vyombo vya habari ili kuwafikia waumini na umma kwa ujumla.

Viongozi wa KKKT wanaweza kutumia jukwaa la mikutano ya kidini au matukio maalum kama vile Sinodi Kuu au hafla za kitaifa za kanisa kutangaza tamko hilo rasmi.

Baada ya tamko kutolewa, KKKT inaweza kuchukua hatua za ufuatiliaji kuhakikisha kuwa serikali au wadau wengine wanaolengwa wanachukua hatua stahiki. Kanisa linaweza pia kuendelea kuzungumzia suala hilo kupitia vyombo vya habari, mikutano ya kidini, au mawasiliano na viongozi wa kisiasa na kijamii. Utetezi huu ni sehemu ya dhamira ya KKKT ya kuhakikisha masuala ya kijamii na haki za binadamu yanazingatiwa ipasavyo.Kwa ujumla, mchakato wa kutoa tamko katika KKKT ni wa uwazi na wa kimfumo, ukihusisha hatua za mashauriano, tathmini ya kina, na uandaaji wa taarifa rasmi, huku ukilenga kutoa mwongozo wa kimaadili na kijamii.

Ni makosa na utovu wa uchaji kwa Malisa ambaye ni muumini wa KKKT na ambaye amejitabahisha kuwa mchambuzi kutaka KKKT itoe tamko eti kwa sababu TEC imetoa tamko.. Nikosa na kujiongoza vibaya kwa Malisa kutaka askofu mkuu Malasusa aamke na kukimbia kutoa tamko eti kwa sababu kaona TEC wametoa tamko. Malisa alipaswa kufahamu "rationale" Na "procedure" Ya kutoa tamko la kitaifa la KKKT.

KKKT ilikwisha kutoa tamko zito kabisa juu ya matukio ya watu kutekwa na kupotea. Ikiwa bado wanafuatilia utekelezaji na hatua gani wataamua baada ya matukio hayo kuonekana bado yangalipo ni suala la utaratibu wa ndani wa KKKT ambao Malisa anapaswa kuwa anaufahamu. Tunamsihi Malisa, Mihemko yake kisiasa isiwe juu ya imani yake ya dini. Ataharibikiwa.
Unahangaika sana siku hizi kama kuku aliyekatwa kichwa. Dhambi ya usaliti uliyomfanyia Lwakatare itakutesa sana maisha yako yote
 
Tungebaki na RC TU
HAYA MENGINE VISIMBIZI VYA KUJILIMBIKIZIA MALI ZA WASHARIKA
 
Back
Top Bottom