UBUNGO, DAR: Uchaguzi wa Umeya waahirishwa

UBUNGO, DAR: Uchaguzi wa Umeya waahirishwa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
Uchaguzi Mayor wa Ubungo umeahirishwa mpaka itakapotangazwa tena. Sababu za kuahirishwa hazijawekwa wazi tutaendelea kuwaletea taarifa kamili

Mwanahabari Huru.

=======

IMG_9987.JPG


Wajumbe wa CHADEMA na CUF wamesusia uchaguzi na kutokana na kile walichokiita kuwa baadhi ya wajumbe wa CCM kuwa wameongezwa na kisha wajumbe wawili wa UKAWA wamehamishwa na kuwapeleka ubungo ili kujipatia ushindi

Na miongoni kwa wajumbe walioongezwa Waziri wa Elimu.
 
Hao ndio Ccm bana, chama kilichodumisha amani ya Tanzania kwa miaka 55 huku kikiiletea maendeleo makubwa

Nasikia na wateuzi wa Magufuli Arusha wanafanya ipasavyo kazi aliyowatuma wanawaseka ndani madiwani wa upinzani na kuwapangia posho ya 10,000 kwenye vikao
 
Hili ndio tatizo la Serikali hii,huwezi kuleta maendeleo katikati ya "mitifuano" ya kisiasa.Maendeleo ni pamoja na amani ya kisiasa ndani ya nchi...Maendeleo huendena na uvumilivu wa kisiasa.Unaposema nchi hii imeendelea,huangalii fly-overs,barabara,madara na viwanja vya ndege na ndege kama bombadia.Unaangalia pia amani ya moyo,uvumilivu na ustahimilivu wa wananchi wako katikati ya tofauti zao za kisiasa.

Kwa hali hii,tusipokuwa makini,ndani ya miaka kumi tunaweza kuwa Taifa lililo salama ktk ubaguzi wa Kikabila kuliko nchi zote zinazotuzunguka,lkn tukawa Taifa lenye ubaguzi wa hovyo sana wa itikadi za kisiasa.Hii ni hatari sana...Political Tolerance ina nafasi kubwa sana ktk kufikia maendeleo ya pamoja.Chuki za kisiasa ni kama moto wa kifuu,unaweza kukaa week nzima bila kufumuka,siku ukifumuka unaivisha mpaka maharage.

We opted for Political Pluralism.Hii ni dhana ya kuleta maendeleo kwa kujumlisha watu wa itikadi,mitazamo na hulka tofauti.Political Pluralism ni aina ya falsafa ya kimaendeleo ambapo juhudi za maendeleo zinafikiwa katikati ya watu wenye mitizamo tofauti,hulka tofauti,hisia na hata mtindo tofauti wa maisha.Hapa unaacha nafasi kwa wanasiasa aina ya Godbless Lema wawepo,unaacha watu kama Zitto wawepo,unatoa nafasi kwa Kituo cha Mama Kijo Bisimba,unaaacha Bunge liwe live,unawaacha Mwanahalisi na Mawio waongee mpaka wachoke wakati wewe unapiga kazi.

Sasa hii sanaa ya kika mahali hata sisi watu wako tutachoka kutetea huku mtaani.Kama Dsm walitukataa,basi tujipange upya 2020.Kutumia nguvu na madaraka ya kidola ni kujenga chuki miongoni mwa watu.Tuikumbatie Political Pluralism tulioamua wenyewe kuibeba toka mwaka 1992.
 
ccm imejipanga kuhujumu umeya wa kwote sio kinondoni mpaka ubungo. lengo la kuhairisha ni kujipanga upya...
 
CCM WANAJUA NAMBA, HAWAJUI HESABU!!!

Na. Mtatiro J.

Nimerejea jana DSM. Usiku huo huo nimekutana na madiwani wa UKAWA ambao leo watakuwa wanapambana kulinda ushindi wa wananchi wa Oktoba 25 kwa kuhakikisha Mameya na Manaibu Meya wa Manispaa za Ubungo na Kinondoni wanatoka UKAWA.

NAMBA ZIKOJE KINONDONI:

Madiwani wa CCM kwenye Manispaa ya Kinondoni wako 17 (ukimjulisha hadi Dk. Tulia Ackson - mbunge wa kuteuliwa na Rais). Madiwani wa UKAWA kwa Manispaa ya Kinondoni wako 20.

MCHEZO UKOJE KINONDONI:

Kwanza, Mkurugenzi wa Kinondoni (DED) amewaandikia barua Madiwani wanne wa UKAWA na kuwajulisha kuwa wao si wapiga kura wa Manispaa ya Kinondoni, madiwani hao ni pamoja na Salma Mwasa (Mbunge wa CUF) ambaye amepatia Ubunge wake Jimbo la Kawe lililoko Manispaa ya Kinondoni na hata michakato yote ya kupata Ubunge wake imefanyikia Kawe na NEC na Mkurugenzi wanazo nyaraka zote zinazothibitisha kuwa Mwassa ni diwani wa Kinondoni.

Wakati huo huo mhe. Suzan Lyimo (Mbunge wa Viti Maalum Chadema wa Manispaa ya Kinondoni naye amehamishwa kwa nguvu kwa barua akipelekwa Manispaa ya Ubungo). Uhuni anaofanyiwa Lyimo ndio anaofanyiwa Salma Mwassa wa CUF.

Pili, Mkurugenzi (DED) wa Kinondoni amekokotoa upya idadi ya madiwani wa UKAWA na kumuondoa mmoja, kinyume kabisa na sheria. Mkurugenzi anajisahaulisha kwamba, mamlaka yenye majukumu ya kukokotoa idadi ya madiwani au wabunge wa kila chama ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na tume hiyo hufanya hivyo mara baada ya uchaguzi mkuu. Ukokotozi huu mpya wa DED wa Kinondoni ni aibu kuu isiyotekelezeka kisheria, kimantiki na kikanuni.

Tatu, DED wa Kinondoni ameitisha Mkutano wa Uchaguzi ndani ya saa 24 (kwa dharura) huku akiuita Mkutano Maalum. Nimepitia Kanuni za Uendeshaji wa Manispaa na kujiridhisha kuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Meya na Naibu Meya hauingii kwenye "mikutano maalum". Huu pia ni uhuni wa karne, DED alipaswa kutoa notisi walau ya siku 7 ili madiwani wajiandae na uchaguzi huu kwa mujibu wa kanuni. Kinyume chake, anazivunja kanuni za Manispaa kwa makusudi kabisa.

Hayo ni baadhi ya masuala yanayoweza kuitwa UHUNI, ambayo nimeyabaini. Yapo mengine kadhaa siwezi kuyataja.

WITO WANGU;

Mwaka jana (2015) wananchi wa DSM walizungumza, tena walizungumza kwa sauti kuu. Manipaa ya Temeke wakasema madiwani wengi watoke CCM, Ilala wakasema ni UKAWA, Kinondoni wakasema ni UKAWA pia. Hakuna maajabu yoyote yatakayobadilisha hali hiyo, hakuna ushindi wa mezani wala kujuana na REFA.
Serikali ya Magufuli isilazimishe mambo yasiyowezekana. Manispaa ya Kinondoni madiwani wengi ni UKAWA, wako 20. Hakuna namna ya leo kuwafanya wawe 16, hakuna atakayekubali. "PUNDA ATAKUFA LAKINI MZIGO UTABAKI" na lazima ushindi wa UKAWA hapa Dar ulindwe kwa gharama yoyote.

Nawatakia kila la heri madiwani wa Manispaa ya Kinondoni, wakalinde na kutetea SAUTI na Maamuzi ya wananchi. 20 ni kubwa kuliko 17, hata mwanangu Alexa anajua hivyo. Upande wa Manispaa ya Ubungo ushindi wa UKAWA hauhujumiki.

Mpenda haki
23 Okt 2016.
 
Back
Top Bottom