Ubungo Bus Terminal

Mokoyo

JF-Expert Member
Mar 2, 2010
15,145
5,553
Jana nimeingia DSM kutoka kijijini kwetu Masasi na kufika Ubungo Stendi saa moja na nusu usiku. Nilichokikuta pale ni aibu, hakuna utaratibu kabisa kwenye kuingia na kupaki mabasi na magari madogo yanayokuja kuchukua abiria pale.

Pili nilifadhaishwa na jinsi ambavyo hawa watoa huduma hapa wamekazania kukusanya pesa kwanza kibabe na kwa maringo pasipo kujali uhuru na haki za watu wengine.

Nini kinaendelea hapa, mimi nilifikiri baada ya kurudi kwenye mikono ya serikali ya Jiji miundombinu na huduma nyingine zingeboreshwa lakini naona hakuna jipya zaidi ya kukomaa kwenye kukusanya ushuru kwa vita na mbwembwe
 
Jana nimeingia DSM kutoka kijijini kwetu Masasi na kufika Ubungo Stendi saa moja na nusu usiku. Nilichokikuta pale ni aibu, hakuna utaratibu kabisa kwenye kuingia na kupaki mabasi na magari madogo yanayokuja kuchukua abiria pale.

Pili nilifadhaishwa na jinsi ambavyo hawa watoa huduma hapa wamekazania kukusanya pesa kwanza kibabe na kwa maringo pasipo kujali uhuru na haki za watu wengine.

Nini kinaendelea hapa, mimi nilifikiri baada ya kurudi kwenye mikono ya serikali ya Jiji miundombinu na huduma nyingine zingeboreshwa lakini naona hakuna jipya zaidi ya kukomaa kwenye kukusanya ushuru kwa vita na mbwembwe

Na wewe kwanini uingie na ngalangala la masasi hadi ndani usiku wote huo ?? hukuona kituo njiani?
 
Na wewe kwanini uingie na ngalangala la masasi hadi ndani usiku wote huo ?? hukuona kituo njiani?

je kama ni mgeni jijini, na unaweza kuta anakaa sinza au mwenge, huko njiani atashukia wapi?
 
Ndiyo serikali yetu hiyo.huduma za jamii zote hazina afya nzuri.
Ukweli serikali inatakiwa iwe makini na ifanye haraka kurekebisha mazingira ya pale, au mpaka mwekezaji?
 
Pole sana mkuu sheria na taratibu za nchi hii nazo hulala ifikapo usiku. Na sijui kama kuna hata senti ya makusanyo inarudi kuboresha huduma za kituo hicho pengine wanachoweza kulipia ni umeme tu.
 
Pale mahali pananishangaza sana mimi binafsi. Hivi unavyoingia baa mathalan si unapata huduma kama vile choo ambazo ni bure? Inakuwaje ukiingia ubungo ambapo unalipia ama tuketi au kwa kulipa kiingilio bado huduma muhimu kama choo unalipia tena? Hivi Watanzania tuna nini? Hiyo ndiyo njia pekee ya kupata mapato? na je hayo mapato yameboresha nini kwenye hili wanja la ndege za aridhini? Aibu aibu Watanzania.
 
Muulizeni mwendeshaji kampuni ya familia ya kada mashuhuri wa CCM Kingunge au ni wengine wanaiendesha siku hizi?
 
Ukweli serikali inatakiwa iwe makini na ifanye haraka kurekebisha mazingira ya pale, au mpaka mwekezaji?
Mkuu, UBT inasikitisha sana. Jiji wamesema wana-test kukusanya mapato wenyewe kwa 3 months ili wajue kituo kinaweza kuingiza kisasi gani. thereafter watafute operator.

Kinachinisikitisha ni kwamba, wale waajiriwa wa jiji sasa ndo wamekuwa balaa....ukitoa mia, wanachukua, ukitoa mia mbili wanachukua, kama kuna-popportunity ya kutokukupa receipt wanafanya hivyo. This means, mapato yataonekana ni madogo, hivyo wanampa operator ambaye atabid chini. BUT.....kwa vile wanaye JINI LIKUJUALO.....(Kinjeketile) watampa tena, kwani wataona kuwa yeye alikuwa analiingizia jiji hela nyingi kuloko matarajio yao.

Mchezo unakuwa umeisha kiivyo......Huwa natamani kutengeneza kiwanda cha hand grenade, then nilipue kila mla kodi yangu.
 
Mkuu, UBT inasikitisha sana. Jiji wamesema wana-test kukusanya mapato wenyewe kwa 3 months ili wajue kituo kinaweza kuingiza kisasi gani. thereafter watafute operator.

Kinachinisikitisha ni kwamba, wale waajiriwa wa jiji sasa ndo wamekuwa balaa....ukitoa mia, wanachukua, ukitoa mia mbili wanachukua, kama kuna-popportunity ya kutokukupa receipt wanafanya hivyo. This means, mapato yataonekana ni madogo, hivyo wanampa operator ambaye atabid chini. BUT.....kwa vile wanaye JINI LIKUJUALO.....(Kinjeketile) watampa tena, kwani wataona kuwa yeye alikuwa analiingizia jiji hela nyingi kuloko matarajio yao.

Mchezo unakuwa umeisha kiivyo......Huwa natamani kutengeneza kiwanda cha hand grenade, then nilipue kila mla kodi yangu.
Ni kweli Mkuu, seriously pale panatia kichefuchefu na sio mahala pana huduma njema tena. Kuna kitu hapa umeongea ni ukweli mtupu
 
-Unajua serikali yetu imekosa watumishi waadilifu na wenye nidhamu

Kimsingi ilitakiwa hela inayokusanywa hapo iwe ndo mtaji wa kukarabati stendi yenyewe,kulipa wafanyakazi wa hapo stendi na usafi kwa ujumla.Haihitaji akili nyingi kuifanya stendi ya ubungo kuwa na hadhi stahiki
 
-Unajua serikali yetu imekosa watumishi waadilifu na wenye nidhamu

Kimsingi ilitakiwa hela inayokusanywa hapo iwe ndo mtaji wa kukarabati stendi yenyewe,kulipa wafanyakazi wa hapo stendi na usafi kwa ujumla.Haihitaji akili nyingi kuifanya stendi ya ubungo kuwa na hadhi stahiki
Ila utashangaa pesa ya hpo ndio ya kununua mashangingi mapya ya wakubwa
 
Ila utashangaa pesa ya hpo ndio ya kununua mashangingi mapya ya wakubwa

Mkuu,ndiyo maana unaona kila sasa Dar inatolewa kwenye list yakuwa among dirtiest cities in the world.Pia Meya wa jiji sijui kazi zao ni nini hasa
 
Mkuu,ndiyo maana unaona kila sasa Dar inatolewa kwenye list yakuwa among dirtiest cities in the world.Pia Meya wa jiji sijui kazi zao ni nini hasa
Hata mimi inanikera sana kuona jiji kama hili ni chafu kila kona. Sasa nashangaa hata hapo kituoni ambako ni eneo liko chini ya usimamizi unaotambulika na eneo ambalo liko fenced bado kuna uzembe mkubwa vile
 
mm nimeingia pale jana asubuhi sana..........wakati natoka, nimetoa 300 yangu, naona yule mama ananikodolea macho, kama vile ....si uende tu kwani unahitaji receipt? nikawa mkali, nikamwambia leta receipt hapa!
 
Hata mimi inanikera sana kuona jiji kama hili ni chafu kila kona. Sasa nashangaa hata hapo kituoni ambako ni eneo liko chini ya usimamizi unaotambulika na eneo ambalo liko fenced bado kuna uzembe mkubwa vile

Unajua tatizo ni kupeana vyeo pasipo kujua uwezo au bila kujali uadilifu na nidhamu ya kazi ya mhusika na mbaya zaidi kupeana vyeo kwa maslahi yetu binafsi

Bongo spirit ya kuwajibika patriotically iko chini sana kwa kweli

Pia ubunifu umekosekana na kila anayefanya kazi ilimradi ni ya serikali basi haangalia future ya mradi wenyewe na lengo lilokusudiwa lka huduma bora kama dalili au kiashiria cha kujenga welfare state inakuwa haramu
 
mm nimeingia pale jana asubuhi sana..........wakati natoka, nimetoa 300 yangu, naona yule mama ananikodolea macho, kama vile ....si uende tu kwani unahitaji receipt? nikawa mkali, nikamwambia leta receipt hapa!


Imagine ni picha gani inajengeka pale hata machoni pa wageni maanake ile ndiyo terminal na kuna watalii wanaosafiri kwa mabasi kwenda mikoani

Pia kwa hali kama hii yaani majirani zetu hasa kenya ambao ndiyo competitors wetu kwenye utalii hwahitaji tena negative campaign au propaganda against sisi ili kuvuta watalii kwao kwani tumejimaliza wenyewe

Pia,hata kama case si watalii lakini sisi wananchi wa tanzania tunastahili huduma bora
 
Back
Top Bottom