Ubunge wa Lema uliibua uminywaji mkubwa wa haki - mmoja wa wahanga alikuwa RPC Basilio Matei

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Kama mtakumbuka, Basilio Matei ndie alikuwa RPC Arusha wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010. Matei ni miongoni mwa RPC wachache sana ambao katika utendaji wao huzingatia zaidi haki kuliko matakwa ya chama tawala, na hivyo serikali ya chama hicho hakupendezewa na alichokifanya Arusha siku ile ya kutangaza matokea ya kura za ubunge ambapo kulikuwa na ucheleweshaji mkubwa sana wa bila sababu za msingi.

Kama mtakumbuka, ilipofika majira ya jioni na bado matokeo yalikuwa hayajatangazwa na umati mkubwa wa watu kufurika nje ya ofisi za halmashauri -- wafuasi wa CDM na pia wa CCM, RPC Matei personally alikwenda kwenye ofisi hizo kuwasihi wahusika (Mkurugenzi na timu yake) kutangaza matokeo (yoyote yale) kabla giza halijaingia lau sivyo jeshi la polisi lisingeweza kumudu ghasia ambazo zingetokea iwapo matokeo yangeendelea kutotangazwa na kutangazwa usiku
.

Alikuwa na sababu za msingi kabisa kufanya vile katika kusimamia usalama na amani katika eneo lake.

Hatimaye yalitangazwa kwa Lema kuwa msindi. hata hivyo serikali haikupendezwa na alichokifanya RPC huyo -- yaani kushinikiza matokeo yatangazwe haraka kwani hatua hiyo iliikosesha serikali na 'vyombo' vyake muda wa kuchakachua matokeo na kumtangaza Batilda kuwa mshindi.
Tusisahau poia hapa kwamba vigogo kadha wa CCM walikwenda katika ofisi za kuhesabu kura mchana ule wakati matokeo yanangojewa, akiwemo si mwingine bali EL.

Siku chache tu baadaye alihamishwa ghafla, nakupelekwa makao makuu Dsm na badala yake kumuweka Andangenye.
 
Mungu amsaidie huyo RPC wa zamani alitenda haki na alitenda yale aliyofunzwa kwenye taaluma yake,sasa Mbona Adengenye hakumaliza hata mwaka,Lema amuombe sana Mungu kwa kumsimamia na zaidi heshima kubwa iende kwa wana arusha ambao hawakuteteleka hata siku moja wala kukata tamaa walisimama na mbunge wao mwanzo mwisho tuna mengi ya kujifunza toka kwa wananchi wa Arusha
 
Mkuu nalikumbuka tukio hilo, lilishangaza wengi. Ila nauliza: Matei wanatoka sehemu moja Uchagani na Mbowe?
Aidha kama sikosei kulikuwa wakurugenzi kama wawili hivi ambao ndiyo wasimamizi wa uchaguzi (returning officers) walihamishwa kutoka vituo vyao vya kazi siku au wiki chache tu kabla ya uchaguzi na kupelekwa halmashauri nyingine. Mmojawapo hakuwa wa Arusha?
 
hata mimi niliona "live" kutoka daslam...ushindi wa lema ni ushindi dhidi ya jk aliyemshawishi lema agombee kupitia mafisadi,akakataa,kwa hasira baba division four akamvua ubunge,cdm wakakomaa kwenye rufaa,..jk kasurrender pamoja na simu zilizokuwa zinapigwa kwa majaji kutoka magogoni...arusha is back in the hands of wanyonge..jk haendi tena arusha kuuza sura,..si anamuogopa lema!!!!
 
Mkuu nalikumbuka tukio hilo, lilishangaza wengi. Ila nauliza: Matei wanatoka sehemu moja Uchagani na Mbowe? Aidha kama sikosei kulikuwa wakurugenzi kama wawili hivi ambao ndiyo wasimamizi wa uchaguzi (returning officers) walihamishwa kutoka vituo vyao vya kazi siku au wiki chache tu kabla ya uchaguzi na kupelekwa halmashauri nyingine. Mmojawapo hakuwa wa Arusha?
huwezi kuchangia bila kuingiza ukabila?pambaf
 
Mkuu nalikumbuka tukio hilo, lilishangaza wengi. Ila nauliza: Matei wanatoka sehemu moja Uchagani na Mbowe?
Aidha kama sikosei kulikuwa wakurugenzi kama wawili hivi ambao ndiyo wasimamizi wa uchaguzi (returning officers) walihamishwa kutoka vituo vyao vya kazi siku au wiki chache tu kabla ya uchaguzi na kupelekwa halmashauri nyingine. Mmojawapo hakuwa wa Arusha?
hapana basilio mattei si mtu wakaskazini yeye ni mtu wa MARA!
 
Ukiangalia mambo haya ya uchaguzi:

Igunga: Mahakama yatengua ushindi wa Mbunge (CCM)

Sumbawanga: Mahakama yetengua ushindi wa Mbunge (CCM)

Arusha: Mahakama kuu yatengua uamuzi wa mahakama kuu juu ya mbunge (CDM)


Utaona jinsi ambavyo chaguzi zetu bado kabisa kufuata haki. Ingeweza kuwa kwingi tu lakini kwingine rufaa haikukatwa.

Lesson kwa CCM:
Kote ambako ushindi ni wa kuiba, watu wanapoteza imani na upinzani unaimarika huko. Hili mlifikirie katika mikakati yenu.
 
Kusema kweli ile hatua aliyochukuwa matei kwenda kuhimiza kutangazwa matokeo ilikwa ni hatua ya kuigwa na ma-RPC wengi.

Na sasa naamini kwamba kuchelewsha matokeo lengo lake ilikuwa ni kuchochea wafuasi wa CDM wafanye vurugu ili kuki-brand chama hicho kuwa ni chama cha vurugu.
 
hata mimi niliona "live" kutoka daslam...ushindi wa lema ni ushindi dhidi ya jk aliyemshawishi lema agombee kupitia mafisadi,akakataa,kwa hasira baba division four akamvua ubunge,cdm wakakomaa kwenye rufaa,..jk kasurrender pamoja na simu zilizokuwa zinapigwa kwa majaji kutoka magogoni...arusha is back in the hands of wanyonge..jk haendi tena arusha kuuza sura,..si anamuogopa lema!!!!

nimeipenda hiyo "baba division four"
 
Mkuu umenikumbusha kamanda Nyakoro siro wakati akiwa RPC mwanza 2010, na yeye alifanya kama Mattei
 
Siku ile ya uchaguzi nilikuwa Arusha, atmosphere niliyoiona nilijua asubihi pengekuwa na maiti zaidi ya sabini kila mahali mjini.Ila yalipotoka matokeo kuwa lema kashinda, niliweza ona jinis mji ulivyo na watu mafundi wa kuendesha pikipiki kwa kasi , na magari ktk umati wa watu wengi yeti asubuhi hakuna hat amajeruhi. Ningependa Jk aende arusha hata kwa siri siku kama hii ya kuja Lema au uchaguzi, pengine angerudi tongotongo limemtoka.Lema hajawahi kuwa just a contestant ktk chaguzi zozote Arusha.Mweny ekujua akamuulize Mrema.Lema amekuwa na nguvu za ajabu kisiasa arusha kwa miaka mingi sana.CDM yenyewe ni brand Arusha. NI akina Ritz na uafahamu wao wa kuunga uunga ktk bao na kashata, ndio wanatoa maeneo ya kike tuu bila jua.
 
HUyu jamaa niliwahi kuw ana mazungumzo naye ktk office yake ni mtu mwelewa na unayeweza sikilizana naye tofauti na askari wengine ambao kila dkk lazima wajikute wamekwenda mbele vibaya na kubidi kuwarudisha na kuwaelewesha(askari wengi huishi na kusema kwa maoea ktk fikra zao,hivyo kurukia conclusion tuu).Huyu jamaa alikuw ana personality na ukimkuta uraiani si rahisi san akufahamu kuw ani askari. Kwake isingewezekana kufanya ujinga wa kiasi cha CCM hata kama naye yeye ni matokeo ya mfumo wa kiovu wa CCM na polisi.
 
Huyo Andengenye ndo akaja kuwaharibia zaidi ccm.. Maana ikafika wakati akaundiwa zengwe toka makao makuu na wizarani..
 
Majira ya saa 10 jioni nilikuwa nimesimama karibu na viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Arusha. Alikuwepo Mwenyekiti wa mkoa Samson Mwigamba, Katibu wake Amani Golugwa, Mratibu wa Vijana Mkoa Ephata Nanyaro na Mratibu wa Wanawake Cecilian Ndossi. Nakumbuka Mwenyekiti wao alimpigia RPC simu na baadaye nilisikia akiwaambia wenzake kwamba RPC amesema ameshafika ofisi za halmashauri na kumwambia Mkurugenzi kwamba asipotangaza matokeo hali itakuwa mbaya na jeshi halitaweza kuhimili. na kwamba pia alishampigia mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya. RPC akasema wasipotekeleza ushauri wake wa kutangaza matokeo, kitakachotokea yeye hana kosa.

Lakini kuna taarifa pia kwamba baada ya uchaguzi Matei alimwita Lema na kumshauri aondoke mara moja kwenda mahali akatulie halafu apitilize huko kwenda kuapishwa Dodoma na arudi Arusha akiwa ameshaapa kuwa mbunge. Inasemekana kulikuwa na mipango hata ya kummaliza Lema ndo maana alimshauri hivyo.

Walioshughulikiwa ni wengi ikiwa ni pamoja na Mkuu wa Upelelezi wa wilaya (OC-CID) wa wakati huo Salva na pia Mkurugenzi wa halmashauri wa wakati huo pia alihamishwa na kushushwa cheo muda mfupi kabla ya uchaguzi.
 
Back
Top Bottom