Ubunge na kuajiriwa - sheria inaruhusu?

Shishye

JF-Expert Member
Feb 26, 2009
269
1
Kuna jambo linanitatiza kwa muda sasa, nimefikiria sana jibu lake silipati. Nimeona niliweke hapa mbele yenu muweze kunisaidia. Mtu anapoamua kugombea ubunge anakuwa na kazi yake anayoifanya labda mkulima, mfanyakazi au biashara. Je akishaupata huo ubunge, kuna sheria yoyote inayomtaka aachane na shughuli alizokuwa anazifanya? Nimekuwa nikiona waajiriwa wengi wakiacha kazi au kuchukua likizo bila malipo pindi wapatapo ubunge, mfano Prof. Mgombelo kipindi kilichopita alikuwa mbunge na aliacha kufundisha chuo muda wote wa ubunge wake. Wapo pia akina Victor Mwambalasi ambaye alikuwa ameajiriwa kwenye kampuni binafsi na ameendelea na kazi hiyo hata baada ya kuwa mbunge. Wapo pia wafanya biashara kadhaa kama Karamagi wanaoendelea na bishara zao na wakati huo huo ni wabunge. Swala langu ni kuwa, unapokuwa mfanyakazi sehemu fulani na huku ni mbunge; kama mbunge unatakiwa kusimamia utendaji wa taratibu na sheria za nchi na utekelezaji wa maswala mbalimbali; kama mwajiriwa wakati mwingine wewe uko katika utendaji au maslahi yako yanaathirika kwa utekelezaji wa sheria fulani. Napata shida kujua kuna mwongozo gani katika hili. Good governance inahusika hapa, na inakuwaje?
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haimzuii mtu kuchaguliwa au kushika madaraka ya Ubunge endapo ameajiriwa na taasisi Binafsi (si Mtumishi wa Serikali) au anafanya biashara zake mwenyewe. Ibara ya 67 ya Katiba hiyo inaelezea mahitaji ya mtu kuchaguliwa kuwa Mbunge.

Kwa mtazamo wangu, kinachoweza kuzuia mtu kuendelea kuajiriwa baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge ni mambo yafuatayo (busara binafsi za Mbunge):

1. Kushindwa kuwajibika kikamilifu kwa mwajiri wake andapo ataendelea na ajira (kushindwa kukidhi mahitaji ya Mwajiri)
2. Kuhisi kuwa majukumu ya uBunge yanaitaji muda wake mwingi hivyo kushindwa kufanya yote kwa pamoja (kushindwa kukidhi mahitaji ya Ubunge)
3. Kuhisi heshima aliyopewa ni kubwa kuliko ajira aliyonayo. Hivyo kuhisi amepanda chart na hivyo hawezi kuendelea na ajira
4. Kuepuka kutumiwa na mwajiri kwa maslahi ya biashara au maslahi binafsi ya mwajiri wake.
 
Back
Top Bottom