Kanyunyu
JF-Expert Member
- May 2, 2012
- 335
- 495
Tayari Chama Cha Mapinduzi kimepitisha majina ya wanachama wake watakaopigiwa kura za maoni na kamati ya wabunge wa CCM kwaajili Ubunge wa Africa mashariki (EALA).
Mchakato huu tayari umegubikwa na rushwa za kutisha, ambapo wagombea wa nafasi hiyo wanalazimika kutoa rushwa kubwa kushawishi kupigiwa kura na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Chanzo chetu kimenasa jinsi rushwa inavyotembea jijini Dar es Salaam na Dodoma ambapo wagombea wanawahonga wabunge ili kupata kura.
Tumejiridhisha pasina shaka kwamba wabunge wana njaa kupita maelezo hivyo wanadai kupewa rushwa ili kutoa kura zao. Kiasi cha rushwa kinachotolewa ni kuanzia sh 1,000,000/= hadi sh 3,000,000/= kwa Mbunge mmoja.
Mpaka sasa mgombea anayetajwa kutoa rushwa kufuru ni Dkt. Ngwaru Maghembe mtoto wa Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii Jumanne Maghembe. Ambaye anatajwa kutoa Sh 2,000,000/ hadi 3,000,000/ kwa kila Mbunge . Ngwaru anatajwa kuanza kutoa rushwa kwa wabunge tangu mwaka 2021 na wabunge wamethibitisha hilo.
"Aisee huyu Ngwaru anatoa pesa na amedhamiria kununua Ubunge kwa gharama yeyote na ameteka wabunge wote," alidokeza Mbunge wa Jimbo moja la Nyanda za Juu Kusini. Ngwaru Maghembe anafanya fujo zote hizi bila woga na tayari amepitishwa kugombea nafasi hiyo na chama chake.
Hii ni salamu na ishara ya wazi kwamba siasa za rushwa na ukubwa wa mfuko ndani ya CCM zimerudi upya, hivyo wanyonge wajiandae kisaikolojia. Na hiyo ni dalili kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, ndani ya CCM ni mnada wa ushindani wa ukubwa wa mifuko Ili upate uongozi.
CCM chini ya Samia Suluhu Hassan, Godfrey Chongolo na Abdurhaman Kinana imeanza kutoa taswira halisi huko mbele tuendako, ambapo rushwa ndiyo itakuwa sifa na mtindo wa kupata uongozi.
Mchakato huu tayari umegubikwa na rushwa za kutisha, ambapo wagombea wa nafasi hiyo wanalazimika kutoa rushwa kubwa kushawishi kupigiwa kura na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Chanzo chetu kimenasa jinsi rushwa inavyotembea jijini Dar es Salaam na Dodoma ambapo wagombea wanawahonga wabunge ili kupata kura.
Tumejiridhisha pasina shaka kwamba wabunge wana njaa kupita maelezo hivyo wanadai kupewa rushwa ili kutoa kura zao. Kiasi cha rushwa kinachotolewa ni kuanzia sh 1,000,000/= hadi sh 3,000,000/= kwa Mbunge mmoja.
Mpaka sasa mgombea anayetajwa kutoa rushwa kufuru ni Dkt. Ngwaru Maghembe mtoto wa Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii Jumanne Maghembe. Ambaye anatajwa kutoa Sh 2,000,000/ hadi 3,000,000/ kwa kila Mbunge . Ngwaru anatajwa kuanza kutoa rushwa kwa wabunge tangu mwaka 2021 na wabunge wamethibitisha hilo.
"Aisee huyu Ngwaru anatoa pesa na amedhamiria kununua Ubunge kwa gharama yeyote na ameteka wabunge wote," alidokeza Mbunge wa Jimbo moja la Nyanda za Juu Kusini. Ngwaru Maghembe anafanya fujo zote hizi bila woga na tayari amepitishwa kugombea nafasi hiyo na chama chake.
Hii ni salamu na ishara ya wazi kwamba siasa za rushwa na ukubwa wa mfuko ndani ya CCM zimerudi upya, hivyo wanyonge wajiandae kisaikolojia. Na hiyo ni dalili kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, ndani ya CCM ni mnada wa ushindani wa ukubwa wa mifuko Ili upate uongozi.
CCM chini ya Samia Suluhu Hassan, Godfrey Chongolo na Abdurhaman Kinana imeanza kutoa taswira halisi huko mbele tuendako, ambapo rushwa ndiyo itakuwa sifa na mtindo wa kupata uongozi.