Ubora wa Shahada za Uzamili kutoka Chuo Kikuu Mzumbe

Bwana Mwendakulima, nina mashaka juu ya uwezo wako wa analysis. Sijui hata kama unaelewa maana ya rapid transformation from IDM to Mzumbe University na pia inaonekana umesikia ju ju kuhusu transformation lakini hujui transformation process ya IDM ilianza lini. Unaongelea suala la MA na PhDs ambalo unaonekana kuwa less informed. Kwanza unaonekana umekariri, Mzumbe University hakuna MA programme yoyote hadi leo hii. Kama una maana ya masters programmes basi hebu tukusaidie. Masters programmes zinazotolewa Mzumbe ni MPA, MBA, na MSc. Probably MA is in the pipeline to be offered in the future but currently not offered. Lakini unaonekana hujui historia ya Mzumbe katika kutoa programmes za masters ilianza lini. Ni kama vile unadhani masters programmes zimeanza kutolewa na Mzumbe University mwaka 2002. Ukweli ni kwamba masters programmes zilianza kutolewa tangu mwaka 1989 by defunct IDM. Naamini huu ni wakati ambao hata ulikuwa hujui kinachoendela katika masuala ya elimu Tanzania. PhD zimeanza kutolewa mwaka 2005/2006. Mwanafunzi wa kwanza kutunukiwa PhD ni Dr. Eleuter Mushi (2009) ambaye sasa ni Mhadhiri Mzumbe, wa pili ni Dr. Modesta Opiyo na orodha imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka. Mwaka 2011, Chuo kiliwatunuku PhD wahitimu 7 akiwemo Dr. Emmanuel Nchimbi, wengine ni wahadhiri kutoka hapa nchini na moja toka Nigeria. Swali langu ni je, Mwanasiasa John Pombe Magufuli na John Ndunguru wakitunukiwa PhD na UDSM hakuna shida, ila Emmanuel Nchimbi akitunukikwa PhD Mzumbe basi kuna shida na kelele nyingi. (You seem to have prejudice in this matter). Do you want to force everyone to go to UDSM?, people must have choice and for them Mzumbe is their choice and above all external examiners wa Mzumbe University ni hao hao Professors wa UDSM na kwenye Viva Voce Examinations wanaalikwa na kutoa comments sasa hizo quality assurance zenye shida ni zipi? Je hao wanasiasa ambao leo hii wameshaonekana ni wengi ni akina nani zaidi ya Nchimbi na Kamala? Kwa nini hakuna aliyeenda mahakamani kuomba mahakama itengue uhalali wa PhD zao?

Ni haki kuwa na wasiwasi mkuu, naomba nikutoe wasiwasi kuhusu uelewa wangu na uwezo wangu wa analysis. Nimeandika maneno machache sana (ukilinganisha na huo mkeka wako) tena very shallow kuonesha wasiwasi wangu kuhusu hicho kinachoitwa Mzumbe University,ni wajibu wako wewe mtaalam kunitoa huo wasiwasi kwa maelezo mujarab siyo kuanza kunishambulia. ukisoma kwa umakini sikuandika popote kuhusu kuwashawishi watu waende UDSM,ukisoma vizuri utagundua hata hiyo UDSM nimeonesha ina tatizo (changamoto?) sugu ya human resource pamoja na kuwa ndiyo University kongwe zaidi ya umma hapa nchini. Mkuu ule mjadala wa mafisadi wa elimu ulikupita kando?maana usingediriki kuwatetea hao wanasiasa wako uliowataja. Nahitaji ufafanuzi wako hapo kwenye red tafadhali
 
  • Thanks
Reactions: SpK
Hapo kwenye red, mimi ni graduate wa Mzumbe na siko kwenye public sector. Na ninakubalika sana sehemu yangu ya kazi. si najisifu, ni bora kuelezana ili niweke kumbukumbu sawa.

Inashangaza sana. Mleta mada anategemea kila kitu aelezwe na Lecturer ambaye kimantiki anatakiwa kutoa 20% ya unachotakiwa kufahamu. Labda ndiyo wale wale mliosoma shule mayai, na ufaulu wenu unapimwa na kiwango cha ada mnacholipa.

Kwa taadhari tu, kama shule ya Mzumbe imemshinda, basi ESAMI watakula kichwa kweupe tu, semister ya kwanza.
hivyo wewe unaunga mkono hoja!!
 
Unaonekana umekuja kwa mtindo tofauti lakini ujumbe wako ni ule ule wa siku zote nao ni USHINDANI WA VYUO. Jipya katika thread yako sijaliona kwa maana haaingii akilini kwamba Master degree za Mzumbe ni kimeo, je wewe umesoma masters zote? Pili ni kuna jumla ya credit points 40 katika masomo 10 ya MBA in Corporate Management, je inaingia akilini kwamba walimu wanapiga stori somo la kwanza hadi la kumi? Tatu imekuwaje umemaliza masomo yote kumi ndipo ugundue udhaifu huo? hukuona udhaifu huo ulipokuwa semester ya kwanza?

Mzumbe shule ni ngumu hadi watu wana disco katika level ya masters. Kwa maelezo yako sichelei kuamini kwamba course work imekushinda, hujapata sifa za kufanya dissertation (umedisco) ndo maana unajifanya shule Masters za Mzumbe ni kimeo hivyo unataka kwenda ESAMI.

kwann hajachagua kwenda UDSM, UDOM, IFM n.k
 
unaonekana umekuja kwa mtindo tofauti lakini ujumbe wako ni ule ule wa siku zote nao ni ushindani wa vyuo. Jipya katika thread yako sijaliona kwa maana haaingii akilini kwamba master degree za mzumbe ni kimeo, je wewe umesoma masters zote? Pili ni kuna jumla ya credit points 40 katika masomo 10 ya mba in corporate management, je inaingia akilini kwamba walimu wanapiga stori somo la kwanza hadi la kumi? Tatu imekuwaje umemaliza masomo yote kumi ndipo ugundue udhaifu huo? Hukuona udhaifu huo ulipokuwa semester ya kwanza?

Mzumbe shule ni ngumu hadi watu wana disco katika level ya masters. Kwa maelezo yako sichelei kuamini kwamba course work imekushinda, hujapata sifa za kufanya dissertation (umedisco) ndo maana unajifanya shule masters za mzumbe ni kimeo hivyo unataka kwenda esami.
masters ya mzumbe ni kama maharage ya mbeya ,hutaki cha tafuta thread zinazozungumzia hilo zipo kibao humu kwanini wengi walalamikie??????????????
 
ila kwenye ukwei tuambiane na turekebishane kuna msichana mmoja alimaliza chuo cha social works nafikiri ndio ustawi akamaenda mzumbe kusoma MBA na alikuwa na lower second tena advanced diploma kipindi hicho ilipofikia muda wa dissertation akaniomba ya kwangu nikamuambia master level kuna programme ya plagiarism check up kamwe usijaribu na tena not more than 20% ya plagiarism alinijibu hicho kitu kwao hakipo kabisa nikampa bila hata ku edit huwezi amini alitoka na 65% nilisikitika sana nikaona kweli sisi hatupo serious huyo ni mmoja nimemuona sasa wengine ambao hawajulikani? nahisi vifaa vya ufundishaji, kama vitabu, na hizo soft ware na mazingira mazuri kwa ma lecturers ingekuwa fundisho kubwa, nilisoma undergraduate bongo ila nilijionea kwa wenzetu kwenye master level ukicopy hata sentence moja kwenye internet tayari imenaswa mpka utoe reference kuwa umeitoa wapi. ila kwetu sisi na uwezo wa kifedha hiyo software tu kama ya turnitin ni gharama pia
 
Ni haki kuwa na wasiwasi mkuu, naomba nikutoe wasiwasi kuhusu uelewa wangu na uwezo wangu wa analysis. Nimeandika maneno machache sana (ukilinganisha na huo mkeka wako) tena very shallow kuonesha wasiwasi wangu kuhusu hicho kinachoitwa Mzumbe University,ni wajibu wako wewe mtaalam kunitoa huo wasiwasi kwa maelezo mujarab siyo kuanza kunishambulia. ukisoma kwa umakini sikuandika popote kuhusu kuwashawishi watu waende UDSM,ukisoma vizuri utagundua hata hiyo UDSM nimeonesha ina tatizo (changamoto?) sugu ya human resource pamoja na kuwa ndiyo University kongwe zaidi ya umma hapa nchini. Mkuu ule mjadala wa mafisadi wa elimu ulikupita kando?maana usingediriki kuwatetea hao wanasiasa wako uliowataja. Nahitaji ufafanuzi wako hapo kwenye red tafadhali

Ni kweli ulikuwa wajibu wangu, kukutoa wasiwasi ndo maana nilipaswa kutoa maelezo mengi, ingawa kwa maelelezo hayo umeona nimeandika mkeka. Mzumbe University sio tu kinaitwa hivyo, bali ni Chuo Kikuu kilichoanzishwa kwa mujibu wa sheria chenye ithibati kamili. Matatizo yaliyopo ya rasilimali sio tu kwa Mzumbe bali ni matatizo sugu kwa taasisi nyingi hapa nchini. Maelezo yangu yalikuwa ni mengi kwa kuwa lengo halikuwa kukujibu wewe moja kwa moja bali pia ni mchango kwa thread, hiyo ndiyo sababu ya kuitaja UDSM kwa kuwa kuna wengine wengi walifanya ulinganifu na hiyo imekuwa ni thinking trend katika jamii forums. Mjadala wa mafisadi wa elimu naufahamu sana na kwa kweli haukunipita, lakini hatupaswi kufanya analysis incrementally badala ya kuchambua hoja kwa upekee ili nao kwa kadiri ya wakati pia. Kuhusu sehemu yenye red, ni tahadhari niliyoitoa kutokana na watu kufanya generalization ya masters programme kuwa ni Master of Arts (MA). Kwa hiyo nilichosema ni kwamba Mzumbe hakuna Master of Arts ila kuna Master of Public Adminstration (MPA), Master of Business Administration (MBA) Master of Science in (Economics, HRM, Project Planning and Management, Local Governement Management, Health Services, Accounting and Finance, Marketing Management, Development Policy na nyingine nyingi). Usichoshwe kwa maelezo marefu na kuona kuwa ni mkeka bali hii ndi namna pekee ya kukufahamisha ukweli. I know for most of we Africans, readership is a major challenge especially for the young generation.
 
Ni haki kuwa na wasiwasi mkuu, naomba nikutoe wasiwasi kuhusu uelewa wangu na uwezo wangu wa analysis. Nimeandika maneno machache sana (ukilinganisha na huo mkeka wako) tena very shallow kuonesha wasiwasi wangu kuhusu hicho kinachoitwa Mzumbe University,ni wajibu wako wewe mtaalam kunitoa huo wasiwasi kwa maelezo mujarab siyo kuanza kunishambulia. ukisoma kwa umakini sikuandika popote kuhusu kuwashawishi watu waende UDSM,ukisoma vizuri utagundua hata hiyo UDSM nimeonesha ina tatizo (changamoto?) sugu ya human resource pamoja na kuwa ndiyo University kongwe zaidi ya umma hapa nchini. Mkuu ule mjadala wa mafisadi wa elimu ulikupita kando?maana usingediriki kuwatetea hao wanasiasa wako uliowataja. Nahitaji ufafanuzi wako hapo kwenye red tafadhali

Ni kweli ulikuwa wajibu wangu, kukutoa wasiwasi ndo maana nilipaswa kutoa maelezo mengi, ingawa kwa maelelezo hayo umeona nimeandika mkeka. Mzumbe University sio tu kinaitwa hivyo, bali ni Chuo Kikuu kilichoanzishwa kwa mujibu wa sheria chenye ithibati kamili. Matatizo yaliyopo ya rasilimali sio tu kwa Mzumbe bali ni matatizo sugu kwa taasisi nyingi hapa nchini. Maelezo yangu yalikuwa ni mengi kwa kuwa lengo halikuwa kukujibu wewe moja kwa moja bali pia ni mchango kwa thread, hiyo ndiyo sababu ya kuitaja UDSM kwa kuwa kuna wengine wengi walifanya ulinganifu na hiyo imekuwa ni thinking trend katika jamii forums. Mjadala wa mafisadi wa elimu naufahamu sana na kwa kweli haukunipita, lakini hatupaswi kufanya analysis incrementally badala ya kuchambua hoja kwa upekee ili nao kwa kadiri ya wakati pia. Kuhusu sehemu yenye red, ni tahadhari niliyoitoa kutokana na watu kufanya generalization ya masters programme kuwa ni Master of Arts (MA). Kwa hiyo nilichosema ni kwamba Mzumbe hakuna Master of Arts ila kuna Master of Public Administration (MPA), Master of Business Administration (MBA) Master of Science (MSc) in (Economics, HRM, Project Planning and Management, Local Government Management, Health Services, Accounting and Finance, Marketing Management, Development Policy na nyingine nyingi). Usichoshwe kwa maelezo marefu na kuona kuwa ni mkeka bali hii ndi namna pekee ya kukufahamisha ukweli. I know for most of we Africans, readership is a major challenge especially for the young generation.
 
Ni kweli ulikuwa wajibu wangu, kukutoa wasiwasi ndo maana nilipaswa kutoa maelezo mengi, ingawa kwa maelelezo hayo umeona nimeandika mkeka. Mzumbe University sio tu kinaitwa hivyo, bali ni Chuo Kikuu kilichoanzishwa kwa mujibu wa sheria chenye ithibati kamili. Matatizo yaliyopo ya rasilimali sio tu kwa Mzumbe bali ni matatizo sugu kwa taasisi nyingi hapa nchini. Maelezo yangu yalikuwa ni mengi kwa kuwa lengo halikuwa kukujibu wewe moja kwa moja bali pia ni mchango kwa thread, hiyo ndiyo sababu ya kuitaja UDSM kwa kuwa kuna wengine wengi walifanya ulinganifu na hiyo imekuwa ni thinking trend katika jamii forums. Mjadala wa mafisadi wa elimu naufahamu sana na kwa kweli haukunipita, lakini hatupaswi kufanya analysis incrementally badala ya kuchambua hoja kwa upekee ili nao kwa kadiri ya wakati pia. Kuhusu sehemu yenye red, ni tahadhari niliyoitoa kutokana na watu kufanya generalization ya masters programme kuwa ni Master of Arts (MA). Kwa hiyo nilichosema ni kwamba Mzumbe hakuna Master of Arts ila kuna Master of Public Administration (MPA), Master of Business Administration (MBA) Master of Science (MSc) in (Economics, HRM, Project Planning and Management, Local Government Management, Health Services, Accounting and Finance, Marketing Management, Development Policy na nyingine nyingi). Usichoshwe kwa maelezo marefu na kuona kuwa ni mkeka bali hii ndi namna pekee ya kukufahamisha ukweli. I know for most of we Africans, readership is a major challenge especially for the young generation.

Thanks a million mkuu kwa maelezo mazuri.Ila changamoto bado ni nyingi katika mfumo wa elimu hapa nchini.Binafsi ni Civil engineer na nimetamani kwa muda sasa kujiunga na Msc.(related to my field) lakini my instincts tell me hakuna nitakachoongeza kwa aina ya elimu inayotolewa na hizi institutions zetu (i stand to be corrected). BTW hapo kwenye red umeniacha kidogo didi you mean an interest to read? If so,I'm an avid reader don't worry
 
Sitaki kukihukumu chuo chote kwa ujumla lakini binafsi nina rafiki yangu anajisifia mtaani kwamba alinunua dissertation ya masters yake ya MPA na amefanikiwa kupata upper second kutoka Mzumbe University. Naomba wadau wanaohusika na hiki chuo wasichukuliwe kukosolewa kama ni kosa la jinai bali waichukulie kama changamoto na waifanyie kazi. Huyu mtu anajisifia kuwa pale ni wewe tu na hela yako hata PHD utaipata, ingawa sitaki kumuamini kwa 100% lakini naona kuna kitu kinatakiwa kifanyike kwenye hili.
 
nimeziona product za mzumbe ni ovyo ovyo ovyooo!! mfano ni meneja wa shirika la posta mkoa wa mbeya na mwenzie wa mkoa wa rukwa, yaani mzumbe mnatia aibu sana kwenye MBA zenu, MTABISHA SANA LAKINI UKWELI NDIO HUO!
 
Mimi binafsi nimesoma Mzumbe na nathibitisha kuwa ukiwa na pesa za kuhonga Mzumbe unapata degree yako ukiwa umelala kitandani. MZUMBE ni "DEGREE MILL" kwa bongo. MZUMBE imekuwa CBE No.2.
 
hivi yule Vice Chancellor wa Mzumbe vp PhD yake? maana kuna kipindi alituhumiwa kuwa ana PhD feki
 
kasome kijana acha uvivu,mkibakia majungu ayo mtakufa masikini. wenye akili zao wanasoma na ndo hao wanapata ujuzi na wanasonga mbele,
 
Elimu ya Masters sio Undergraduate. Inategemea zaidi juhudi binafsi ktk course work na hasa dissertation. Uzuri wa Mzumbe kuna policy inayowabana ma supervisor kuhakikisha watu wanamaliza dissertations on time tofauti na udsm na vyuo vingine unaweza kaa miaka mitatu hujagraduate. Kuandikiwa disertation ni suala la mtu binafsi halihusisni na chuo.
 
Nimekuwa najiluliza maswali mengi sana kuhusu hiki chuo, rapid transformation from IDM-Mzumbe to Accredidated University yenye hadhi ya kutoa hizo MA na Phd's kwa fujo. UDSM chuo kikongwe bado kinastruggle na human resources especially lecturers hadi leo (tafakari). Na ninapoona wanasiasa ( kumbuka dunia ya tatu hili ndilo kundi linalopenda njia za mkato pengine kuliko mengine) wanakimbilia Mzumbe napata wasiwasi zaidi!!

Wameanza kutoa masters tokea ikiwa IDM, that is 1990's kwa hiyo hakuna rapid transformation hapo. Jua historia ya Mzumbe kwanza kabla ya kuanA comments zenu za kuangalia Chuo kipi zaidi. Ok fine how about IFM??
 
Nakuabaliana na mleta hoja. bosi wangu alisoma hiyo kitu baada ya mm kupiga MSC akaona wivu. Sijamwona akisoma ila dissertation yake ni kama ya mtoto wa form six. Eti nae kagraduate mwaka jana.Mzumbe ninyi vipi bana au ndio sera za kigamba?
 
ni chuo gani bongo kina detect plagarism??.........ni chuo gani bongo wanafunzi hawaandikiwi dissertation??...tukiacha unafiki nchi itasonga,tatizo bongo walioenda shule(sio wasomi) ndio vinara wa unafiki...mkimaliza kutambiana kama wahaya vile, mtuambie sasa izo mastaz zimeleta change gani kwa taifa
 
Back
Top Bottom