Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Ndiyo Mchungaji kakulia kwenye Ujamaa, kalewa mvinyo wa Nyerere na Azimio la Arusha, anapenda haki sawa kwa wananchi.
Lakini leo Mchungaji anasema "Ubepari" ndio suluhisho la matatizo yetu.
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa kumuwezesha mzawa awe bwanyenye, tajiri, kabaila na mwenye mali, alimradi kila kitu ni halali.
Ubepari wa Mchungaji ni ule ambao unasema Serikali kazi yake ni kutunga sheria, ,kusimamia sheria na udhibiti wa kanuni na kujenga misingi imara ya kuwezesha uzalishaji mali, misingi kama Barabara, Maji, Reli, Mtandao wa Umeme, Simu na kisha kuachia sekta binafsi iendeshe shughuli za kila siku na Serikali ikinge mikono kupata kodi na pato lake!
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa kumtaka kila mtu aanze kuchangia huduma na kulipa kodi. Bure imefika tamati, ni buriani bin hayati, hatuwezi kuendelea kudai tu-masikini, maana tunalelea umasikini kwa kuendekeza jamii isiyotaka ondokana na umasikini!
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa Mtanzania mbunifu na mchapa kazi ambaye atatumia njia na mifumo halali bila kupita njia fupi kujijenga kiuchumi na ni ruksa kuwa nyapara na kuajiri wenzake wasiotaka kujituma!
Tukisha anza kujijenga kama mabepari, kila mtu atachangia uzalishaji mali na tutaanza kupiga hatua za maendeleo tukiwa huru wa utegemezi wa Serikali na misaada kutoka nje.
Kwa upande wa pili wa Ubepari wa Soko Huria, Mchungaji anasema, nafasi ya kwanza ni kuhamasisha wazawa na uzalishaji wa mali wa ndani, iwe ni viwanda, kilimo, madini na huduma. Misingi imara ya uzalishaji iwekwe ili wazawa wapate fursa ya kushindana na wawekezaji kutoka nje.
Mwisho, kwenye Ubepari wa Mchungaji, Serikali inakuwa wabanifu wa matumizi na si Pedeje wa kuzimwaga hovyo hovyo!
Heri ya 2009!
Lakini leo Mchungaji anasema "Ubepari" ndio suluhisho la matatizo yetu.
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa kumuwezesha mzawa awe bwanyenye, tajiri, kabaila na mwenye mali, alimradi kila kitu ni halali.
Ubepari wa Mchungaji ni ule ambao unasema Serikali kazi yake ni kutunga sheria, ,kusimamia sheria na udhibiti wa kanuni na kujenga misingi imara ya kuwezesha uzalishaji mali, misingi kama Barabara, Maji, Reli, Mtandao wa Umeme, Simu na kisha kuachia sekta binafsi iendeshe shughuli za kila siku na Serikali ikinge mikono kupata kodi na pato lake!
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa kumtaka kila mtu aanze kuchangia huduma na kulipa kodi. Bure imefika tamati, ni buriani bin hayati, hatuwezi kuendelea kudai tu-masikini, maana tunalelea umasikini kwa kuendekeza jamii isiyotaka ondokana na umasikini!
Ubepari wa Mchungaji ni ule wa Mtanzania mbunifu na mchapa kazi ambaye atatumia njia na mifumo halali bila kupita njia fupi kujijenga kiuchumi na ni ruksa kuwa nyapara na kuajiri wenzake wasiotaka kujituma!
Tukisha anza kujijenga kama mabepari, kila mtu atachangia uzalishaji mali na tutaanza kupiga hatua za maendeleo tukiwa huru wa utegemezi wa Serikali na misaada kutoka nje.
Kwa upande wa pili wa Ubepari wa Soko Huria, Mchungaji anasema, nafasi ya kwanza ni kuhamasisha wazawa na uzalishaji wa mali wa ndani, iwe ni viwanda, kilimo, madini na huduma. Misingi imara ya uzalishaji iwekwe ili wazawa wapate fursa ya kushindana na wawekezaji kutoka nje.
Mwisho, kwenye Ubepari wa Mchungaji, Serikali inakuwa wabanifu wa matumizi na si Pedeje wa kuzimwaga hovyo hovyo!
Heri ya 2009!
Last edited: