Tanzania hakina diplomat ni wapumbavu fulani wanaojinafikisha kwa Utawala ndio hupewa hivyo vyeo kama Chaka lao wakale maisha au wengine hupewa kama adhabu wapotee nchini wanapelekwa nchi za hovyo kama Togo huko unakaa hauna kazi hakuna hata mtanzania mmoja.balozi zetu zote ni vituko, tofauti kabisa na balozi za wenzetu. unajua kwamfano mmarekani akija hapa tz akaamua kutembelea ubalozi wake, treatment anayopewa ni nzuri ila mbongo ukiwa nje ukatembelea ubalozi wetu wowote ule, cha kwanza wanakuona kama umeenda pale kuomba msaada labda maisha yamekupiga, wanaanza kujidistance awali kabisa wakikuona. niliwahi kutembelea ubalozi mmoja hivi tena nikiwa mwanafunzi,nina hela yangu na sikwenda pale kuomba hela ila kuongewa tu mhuri kwenye nyaraka fulani ambayo ilitakiwa nirudi nigongewe bongo, nikasema niende tu ubalozini hapa wanigongee...nilihisi kama mtu akipata tatizo bora ukimbilie ubalozi wa mzungu kuliko ubalozi wao. hawa madiplomat wetu wanatakiwa wafundishwe kabla hawajaenda huko wajue wameenda huko kwa kodi zetu na ndizo zinazowalipa mishahara. over.
Kesi ha ngedele uipeleke kwa Nyani?Mmemripoti huyo balozi kwa Mulamula au mama kabisa ili amzingue??
Huu unaweza kuwa ukweli mtupuSiri usio ijua mabalizi wakipangiwa kwenda sehemu mara nyingi wanaajiri watoto waonau ndugu zao ambao hawana knowld6 hata kidogo ya wanachofanya.
Kuhusu watu wa kuja kwenye gala usishangae ndio mfumo wa huu utawala hata kwenye musafara ya chief wamo watu ambao wako humu sio watumishi wa serikali lakini wamewekwa kama wafanya biashara huku hata biashara qanazofanha hazieleweki
Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
We're heading there at a frightening speed!Tanzania is potentially a failed state,.......
View attachment 2027542 Huyu tayari ameteuliwa na anabarua mkononi anasubiri kuapishwa tu balozi malawi kigezo kigezo kikubwa kinachomtofautisha na wana ccm wenzake cc ni kuwa anaweza kuongea kimalawi. Ila wote cc ni std 4 la zamani. Hcn
Hahaaa, mama D wewe unajipitia zako tu 🤣🤣👣👣👣👣
Tatizo wamejaa mahawala, chawa na ndugu wa wazee wa nchi, usitegemee chochote zaidi ya frustrations tuuYaani maafisa wa ubalozini kwa balozi za Tanzania, ni Zero brain. Wako so local yaani hata hawafai kuitwa Diplomats. Wanafanya mambo kama ofisi za mtendaji wa kijiji.
Nilishawahi kukataliwa kuingia ubalozini kisa wanakikao. Yaani ilibidi nitumie nguvu, na kuuliza ni sheria ipi inayozuia nisiingie ubalozini kisa wanakikao? Kama natishiwa usalama wangu nikaona nikimbilie ubalozini, na wao hawataki niingie si ndiyo unauwawa hapo hapo nje ya ubalozi. Sasa huduma niliyoifuata hata sikupewa kwanza hawajui hata utendaji wa serikali katika nyanja za idara kadhaa nchini. Ilikuwa ni vituko. Si huo ubalozi mmoja ni balozi nyingi kadhaa. Ubalozi fulani dada mmoja namuhifadhi huyu analugha za ajabu kwenye simu, na anaongea kwanyodo, unauliza jambo ati hajui, sasa unashangaa hivi hawa watu hawana uzoefu wa kiserikali? Wanapopelekwa huko nje, je nini kinazingatiwa?
Kwasasa napokuwa nje nimeamua kujiona sina balozi, wala sihitaji kuwaona, nachofanya ni kupiga simu moja kwa moja Tanzania katika wizara husika au Idara ambayo nahitaji huduma. Kuliko hawa madiplomats wa kuzuga.
Yaani maafisa wa ubalozini kwa balozi za Tanzania, ni Zero brain. Wako so local yaani hata hawafai kuitwa Diplomats. Wanafanya mambo kama ofisi za mtendaji wa kijiji.
Nilishawahi kukataliwa kuingia ubalozini kisa wanakikao. Yaani ilibidi nitumie nguvu, na kuuliza ni sheria ipi inayozuia nisiingie ubalozini kisa wanakikao? Kama natishiwa usalama wangu nikaona nikimbilie ubalozini, na wao hawataki niingie si ndiyo unauwawa hapo hapo nje ya ubalozi. Sasa huduma niliyoifuata hata sikupewa kwanza hawajui hata utendaji wa serikali katika nyanja za idara kadhaa nchini. Ilikuwa ni vituko. Si huo ubalozi mmoja ni balozi nyingi kadhaa. Ubalozi fulani dada mmoja namuhifadhi huyu analugha za ajabu kwenye simu, na anaongea kwanyodo, unauliza jambo ati hajui, sasa unashangaa hivi hawa watu hawana uzoefu wa kiserikali? Wanapopelekwa huko nje, je nini kinazingatiwa?
Kwasasa napokuwa nje nimeamua kujiona sina balozi, wala sihitaji kuwaona, nachofanya ni kupiga simu moja kwa moja Tanzania katika wizara husika au Idara ambayo nahitaji huduma. Kuliko hawa madiplomats wa kuzuga.
Msitutie aibu kama dinner itakua hotelini lipa uende.
Kwani lazima?huna hela kausha tu we umepewa mwaliko baada ya kuloloma sana bado unaloloma tu.muwage na mipaka
Hao watu waliopo hapo ubalozini nahisi si Watanzania sababu hata historia rahisi tu ya Tanzania hawaijui.Tunasikitika ubalozi wetu wa Tanzania US unejaa wafanyakazi wasiojua wanachofanya. Ili watu waelewe hili nimewapa barua mbili hapa. Barua yenye kumbukumbu namba moja imetumwa kwenye miji miwili tofauti. Ukipiga simu wanasema Dallas eti hawaendi. Cha kushangaza vilevile pamoja na viongozi wa Dallas kuwepo kwenye list ya viongozi wa jumuia walipata barua kwenye mitandao.
Pamoja na kusema kwenye simu sasa kwamba hawaji Dallas kwenye website ya ubalozi wanasema watakuja Dallas kwenye Gallas hotelini. Baada ya viongozi kuona kwenye mitandao wakafikiri watanzania na balozi anakuja kushererekea sikukuu wa uhuru wa miaka 60 na Watanzania. Cha ajabu baada ya viongozi kuhoji waliwaruhusu viongozi wanne tu kuwepo kwenye gala hii tarehe 3. Ingawa ubalozi huohuo sasa unasema hautaweza kuja tena kuwasaidia Watanzania kupata passport zao hapa Dallas,Texas. Cha kujiuliza ni nani anaenda kwenye gala? gharama ni za nani? kwanini sasa wanasema hawawezi kukutana na watanzania?. Hata kama ni wafanya bishara ni kwanini watanzania wasiambiwe wazi ili wahimize wafanyabiashara kuwepo kwenye huu mkutano na wameweka siri mpaka mwenyekiti wa jumuia apige simu. Cha ajabu kingine hawajui tofauti ya jimbo na mji!
Embassy of Tanzania in Washington D.C, USA
Embassy of the United Republic of Tanzania in Washington D.C, USAwww.us.tzembassy.go.tz
View attachment 2027518
View attachment 2027519
Hii hapa watanzania wamepigwa stop hawaja alikwa kabisa! baada ya kelele nyingi wakaruhusu mwenyekiti na wengine wawili lakini eti ni sherehe za miaka 60!!
The Embassy of Tanzania in the USA would like to cordially invite you to the inaugural Tanzania-USA corporate GALA dinner in honor of the 60th Anniversary of independence for Tanzania mainland , as well as the 60th Anniversary of Diplomatic relations between Tanzania and the USA.
VENUE: OMNI DALLAS HOTEL , 555 S Lamar St. Dallas, Tx 75202
DATE: Friday, 3 December 2021.
For more Information please visit : Tanzania at 60 | Tanzania Imara, Kazi iendelee
Tatizo jumuiya zenyewe za watanzania ni ovyo. Wakiambiwa wapeleke orodha unakuta wana chama hai awazidi 10. Na kama wapo wengi mara nyingi kuna mgogoro wa uongozi.
Ubalozi ukiongea na uongozi mmoja, anatokea mwingine kusema awamtambui huyo bwana/bibi kama kiongozi wao.
Sasa hapo kuna issue ya kujipendekeza kuna watanzania ughaibuni wana penda kujikuza na ukikutana na balozi waovyo mfano Kalaghe au wale wanaopenda mialiko ya misosi wanajiingiza kwenye migogoro ya diaspora isiyowahusu na kuchukua upande.
Lakini mabalozi wapya overtime washajifunza kutoingilia migogoro ya diaspora provided kundi linajielewa wao wanashirikiana nao; na as far as they are concerned kila mtanzania ana haki sawa mbele yao uwe diaspora mbeba boksi au Phd na lecturer at top university kwao wote sawa.
Watu wakijapanga na kuwa na uongozi mzuri awana shida, kasheshe sasa kuna sakapoko wanajionaga wao bora kushinda wengine upuuzi huo ndio ubalozi autaki tena.
PS maswala ya passport ni uhamiaji Tanzania. Ubalozi wao awahusiki na lolote siku hizi zaidi ya kufacilitate tu, ukipangiwa siku ya finger print ubalozini ukaenda system ikiwa down sio wao ni Tanzania na awawezi fungua ofisi kila mji sababu awana hiyo budget na watu; ila kuna mapendekezo ya diaspora kufungua ofisi zao wenyewe na kuziendesha ubalozi utashirikiana nao kwa namna moja au nyingine kutatua changamoto zao.
Haya maswala mama Migiro kayatolea ufafanuzi kwa kina UK kuna watu ni vichwa maji tu katika diaspora wao kila siku wanatakupeleka upuuzi wa jumuiya zao ubalozini mambo ambayo siku hizi awataki tena.
Ukiona kiongozi mkubwa anakuja kuna diaspora viherehere wanagawa tshirt na kusafiri elewa siku hizi balozi ahusiki huyo anatumwa na kavuta mpunga kwa kupitia either watu wa usalama, serikalini au CCM (wahusika nyuma ya pazia wanaishi nchi hizo hizo na awapo ubalozini) lakini ubalozi auna raia bora kushinda mwingine.