Bondpost
JF-Expert Member
- Oct 16, 2011
- 6,581
- 9,295
Tanzania hakina diplomat ni wapumbavu fulani wanaojinafikisha kwa Utawala ndio hupewa hivyo vyeo kama Chaka lao wakale maisha au wengine hupewa kama adhabu wapotee nchini wanapelekwa nchi za hovyo kama Togo huko unakaa hauna kazi hakuna hata mtanzania mmoja.balozi zetu zote ni vituko, tofauti kabisa na balozi za wenzetu. unajua kwamfano mmarekani akija hapa tz akaamua kutembelea ubalozi wake, treatment anayopewa ni nzuri ila mbongo ukiwa nje ukatembelea ubalozi wetu wowote ule, cha kwanza wanakuona kama umeenda pale kuomba msaada labda maisha yamekupiga, wanaanza kujidistance awali kabisa wakikuona. niliwahi kutembelea ubalozi mmoja hivi tena nikiwa mwanafunzi,nina hela yangu na sikwenda pale kuomba hela ila kuongewa tu mhuri kwenye nyaraka fulani ambayo ilitakiwa nirudi nigongewe bongo, nikasema niende tu ubalozini hapa wanigongee...nilihisi kama mtu akipata tatizo bora ukimbilie ubalozi wa mzungu kuliko ubalozi wao. hawa madiplomat wetu wanatakiwa wafundishwe kabla hawajaenda huko wajue wameenda huko kwa kodi zetu na ndizo zinazowalipa mishahara. over.
We jiulize yule alikuwa miss anapewa ubalozi anajua nini kuhisi diplomasia???? Mabalozi walikuwa zamani akina mzee Lusinde nk.