Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 875
- 960
*UBALOZI WA MAREKANI, MBONA KWENYE HILI LA RAIA WENU KUINGIA TANZANIA AKIWA NA CORONA MMEKAA KIMYA?.*
Jana raia mmoja wa Marekani mwenye umri wa miaka 61 ambaye ni mfanyakazi wa Ubalozi wa Marekani hapa nchini Tanzania amekua mtu wa pili kuingia nchini Tanzania akiwa na virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid-19).
Raia huyu wa Marekani amekuwa mtu wa pili kubainika kuingiza virusi vya Corona hapa Tanzania baada ya mtu wa Kwanza aliyetambulika kwa jina la Isabela Mwampamba ambaye aliingia nchini kupitia uwanja wa ndege wa KIA kutangazwa jana na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.
Mara baada ya kutangazwa kwa Isabela kuwa mtu wa kwanza kugundulika kuwa na virusi vya Corona, Ubalozi wa Marekani hapa nchini harakaharaka walitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kuchapisha katika akaunti zao za mitandaoni kwa lugha ya Kiswahili na kiingereza juu ya kuwepo kwa Corona nchini Tanzania.
Nilitarajia kwa kasi ileile ambayo walikuwa nayo kumtangaza mtu wa kwanza ambaye ni Mtanzania aliyekuwa safarini nchi za Ulaya, wangekuwa na kasi hiyo hiyo kumtangaza Raia wao wa Marekani aliyetuletea virusi vya Corona kutoka Marekani.
Maana hapa ni kwamba Isabela kavileta kutoka Ulaya na huyu Babu Mmarekani kavileta kutoka Marekani.
Cha ajabu wamekaa kimya na wanajifanya wanaendelea kutoa elimu ya Corona, na wakati Mama Isabela Mwampamba akijitokeza kuwaomba radhi Watanzania, huyu Mmarekani amebanisha kimya, na haielezwi yupo wapi.
Mpaka sasa Watanzania hawajaambiwa kama Mmarekani huyu amepita kuambikiza watu wengine wangapi, wawe ni Watanzania aliokutana nao au Wamarekani wenzake ambao amekutana nao ofisi za Ubalozini anakofanyia kazi.
Kwa Isabela, tulielezwa mpaka dereva wa taxi aliyemtumia na akafuatiliwa, wafanyakazi wa hoteli alikofikia wamefuatiliwa na hoteli aliyofikia imefungwa, halikadhalika wafanyakazi wa KIA waliomhudumia tumewajua.
Sasa huyu Mmarekani jamani kaambukiza wangapi? Hata kujitoleza kuomba radhi tu hakuna!!!
Mbona mambo mengine ya nchi yetu yanapotokea Wamarekani kupitia Ubalozi wao huwa wanashabikia sana??? Hili wanaliona dogo au kwa sababu wanaona linawachafua?
Hivi mtu wao kutuletea Corona na kale katishio ka mabomu kakutengeneza kipi muhimu kwa Ubalozi huu wa Marekani?
Mimi naona kuna haja ya huyu Kaimu Balozi wa Marekani kujitafakari sana. Mienendo yake inatia mashaka sana kwetu Watanzania hasa wakati huu ambapo kumekuwa na maneno mengi dhidi ya nchi yetu.
Lakini inaumiza zaidi, hivi huyu Mfanyakazi wa Ubalozi alijua kabisa kuwa anatoka katika nchi yenye maambukizi ya virusi vya Corona kwa nini hakufikia mahali pa kujihifadhi kipekee ili asiambukize wengine? Hivi Balozi wa Marekani hapa nchini na ofisi yake hawakufikiria kwamba kwa afisa wao huyu kuingia nchini akitokea Marekani ambako tayari kuna maambukizi kwa idadi kubwa ya wananchi ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kwa makusudi?
Nafikiri hapo ndio Watanzania tunapaswa kupima, ukiona Marekani inashabikia mambo ujue kuna jambo ambalo ina maslahi lao, na pale linapotokea jambo linalowachafua ni wepesi sana kujificha na kulipotezea.
Sasa huyu Mmarekani haijulikani alipo, haijulikani kaambukiza wangapi na wala haijulikani kama kuna karantini ya Ubalozi iliyowekwa kwa ajili ya wanaopatwa na virusi vya Corona.
Ndugu zetu Wamarekani kwenye hili mmetukosea sana sana, na bahati mbaya hamtaki kuomba radhi.
Mwisho, nikiwa Mtanzania mwenye uchungu na nchi yangu nawaomba ndugu zangu Watanzania tuwe na utulivu na tuzingatie maelekezo ya Wataalamu kuhusu kujikinga na ugonjwa huu wa hatari.
Tuwakinge watoto wetu ambao wametoka shule baada ya serikali kutangaza kuzifunga kwa mwezi mmoja na tuwakinge zaidi wazee wetu ambao wataalamu wanasema wapo katika hatari zaidi ya kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huu.
Nawatakia usiku mwema.
Mzee Juma Pangadumu.
Ilala, Dar es salaam.
18 Machi, 2020.
Sent using Jamii Forums mobile app
Jana raia mmoja wa Marekani mwenye umri wa miaka 61 ambaye ni mfanyakazi wa Ubalozi wa Marekani hapa nchini Tanzania amekua mtu wa pili kuingia nchini Tanzania akiwa na virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid-19).
Raia huyu wa Marekani amekuwa mtu wa pili kubainika kuingiza virusi vya Corona hapa Tanzania baada ya mtu wa Kwanza aliyetambulika kwa jina la Isabela Mwampamba ambaye aliingia nchini kupitia uwanja wa ndege wa KIA kutangazwa jana na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.
Mara baada ya kutangazwa kwa Isabela kuwa mtu wa kwanza kugundulika kuwa na virusi vya Corona, Ubalozi wa Marekani hapa nchini harakaharaka walitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kuchapisha katika akaunti zao za mitandaoni kwa lugha ya Kiswahili na kiingereza juu ya kuwepo kwa Corona nchini Tanzania.
Nilitarajia kwa kasi ileile ambayo walikuwa nayo kumtangaza mtu wa kwanza ambaye ni Mtanzania aliyekuwa safarini nchi za Ulaya, wangekuwa na kasi hiyo hiyo kumtangaza Raia wao wa Marekani aliyetuletea virusi vya Corona kutoka Marekani.
Maana hapa ni kwamba Isabela kavileta kutoka Ulaya na huyu Babu Mmarekani kavileta kutoka Marekani.
Cha ajabu wamekaa kimya na wanajifanya wanaendelea kutoa elimu ya Corona, na wakati Mama Isabela Mwampamba akijitokeza kuwaomba radhi Watanzania, huyu Mmarekani amebanisha kimya, na haielezwi yupo wapi.
Mpaka sasa Watanzania hawajaambiwa kama Mmarekani huyu amepita kuambikiza watu wengine wangapi, wawe ni Watanzania aliokutana nao au Wamarekani wenzake ambao amekutana nao ofisi za Ubalozini anakofanyia kazi.
Kwa Isabela, tulielezwa mpaka dereva wa taxi aliyemtumia na akafuatiliwa, wafanyakazi wa hoteli alikofikia wamefuatiliwa na hoteli aliyofikia imefungwa, halikadhalika wafanyakazi wa KIA waliomhudumia tumewajua.
Sasa huyu Mmarekani jamani kaambukiza wangapi? Hata kujitoleza kuomba radhi tu hakuna!!!
Mbona mambo mengine ya nchi yetu yanapotokea Wamarekani kupitia Ubalozi wao huwa wanashabikia sana??? Hili wanaliona dogo au kwa sababu wanaona linawachafua?
Hivi mtu wao kutuletea Corona na kale katishio ka mabomu kakutengeneza kipi muhimu kwa Ubalozi huu wa Marekani?
Mimi naona kuna haja ya huyu Kaimu Balozi wa Marekani kujitafakari sana. Mienendo yake inatia mashaka sana kwetu Watanzania hasa wakati huu ambapo kumekuwa na maneno mengi dhidi ya nchi yetu.
Lakini inaumiza zaidi, hivi huyu Mfanyakazi wa Ubalozi alijua kabisa kuwa anatoka katika nchi yenye maambukizi ya virusi vya Corona kwa nini hakufikia mahali pa kujihifadhi kipekee ili asiambukize wengine? Hivi Balozi wa Marekani hapa nchini na ofisi yake hawakufikiria kwamba kwa afisa wao huyu kuingia nchini akitokea Marekani ambako tayari kuna maambukizi kwa idadi kubwa ya wananchi ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kwa makusudi?
Nafikiri hapo ndio Watanzania tunapaswa kupima, ukiona Marekani inashabikia mambo ujue kuna jambo ambalo ina maslahi lao, na pale linapotokea jambo linalowachafua ni wepesi sana kujificha na kulipotezea.
Sasa huyu Mmarekani haijulikani alipo, haijulikani kaambukiza wangapi na wala haijulikani kama kuna karantini ya Ubalozi iliyowekwa kwa ajili ya wanaopatwa na virusi vya Corona.
Ndugu zetu Wamarekani kwenye hili mmetukosea sana sana, na bahati mbaya hamtaki kuomba radhi.
Mwisho, nikiwa Mtanzania mwenye uchungu na nchi yangu nawaomba ndugu zangu Watanzania tuwe na utulivu na tuzingatie maelekezo ya Wataalamu kuhusu kujikinga na ugonjwa huu wa hatari.
Tuwakinge watoto wetu ambao wametoka shule baada ya serikali kutangaza kuzifunga kwa mwezi mmoja na tuwakinge zaidi wazee wetu ambao wataalamu wanasema wapo katika hatari zaidi ya kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huu.
Nawatakia usiku mwema.
Mzee Juma Pangadumu.
Ilala, Dar es salaam.
18 Machi, 2020.
Sent using Jamii Forums mobile app