Ubalozi umemwambia watoto sio wake

Ubalozi umemwambia watoto sio wake

Kuna mbeba boksi mmoja nchi za Ulaya alikwenda huko kutafuta maisha sasa baada ya miaka kama saba(7). Alifanikiwa kupata uraia wa nchi hio ndio akaanza kufanya mipango ya kuivuta familia yake yote huko ughaibuni (mkewe na watoto wake). Katika kuanza mipango akatakiwa kujaza form zote na kwenda kwa daktari kwa kupima afya na kuangaliwa DNA kama hawa watoto wake wa kuwazaa(biological kids) kweli. Mkewe alikuwa ndio mtu wa mwanzo kufanikiwa katika kupata visa ya huko ughaibuni wakabakia watoto wake wanne(4). Baada ya kama wiki jamaa akaitwa aende ofisi ya ubalozi kwasababu aliambiwa kuna masuala anatakiwa kuulizwa. Bila ya kukosa siku ya appointment yake jamaa alifika ubalozini na zamu yake ikafika na kuanza kuhojiwa. Katika kuhojiwa akaulizwa unataka kuidanganya serikali kwa kuforge document za birth certificate za watoto? Jamaa akasema hapana hao wote ni wanangu wa kuwazaa na mke wangu. mtoto wa kwanza akiwa na miaka 15 wa pili 13 wa tatu 10 na wa mwisho ni miaka 9 watatu ni wa kiume mmoja wa kike. Ndipo officer wa ubalozi akatoa zile karatasi za daktari za DNA na kumuonesha jamaa na zina alama za Negative kwa watoto wote. Mbeba boksi akaanza kulia na machozi yakimtoka huku yule mfanyakazi wa ubalozini akijaribu kumfariji, hapo jamaa na kumwambia yule afisa wa ubalozini kuwa aCancel application zote za mkewe na watoto wake na kuondoka zake. Huyu jamaa hakurudi tena kwa mkewe na kufanya safari ya kurudi zake ughaibuni sasa ni mwaka wa 2 huu hajawasiliana na mkewe wala wanawe. Dada zetu kuweni na huruma za kuwabambika waume zenu watoto wa wanaume wengine.
Guyz ebu watu kuweni serious, unachomekewaje bundi kwenye familia bila kujua??? watu watumie muda na watoto, wachunguzeni tabia, maumbile na hata uelewa(akili), utajua tu kama ni wako au la!...watoto wanne wote wa nje??? huyo mke inabidi apelekwe kwa Mungu ili akasamehewe huko juu.
 
Haiwezekani watoto wote wasiwe wake...
Si bure ...
Isijekuwa mkewe alikuwa anatafuta watoto nje ili kumsitiri mumewe...
Maana kukiwa hakuna watoto analaumiwa mwanamke kuwa hazai...
Wengine wanaamua kujisovia tatizo kwa kutafuta donor wa mbegu...
Ni sawa, ila angecheza rafu kwa wawili tu...wanne noma sana
 
hapa ndio huwa inafikia mtu kujuta kuowa ,nashkuru sana mitoto yangu huhitaji DNA ila kuna kimoja bado kama sina uhakika,lakini haina shaka mtoto mtoto tu
Amekuchezea rafu kale ka katikati au ka mwisho??
 
Haiwezekani watoto wote wasiwe wake...
Si bure ...
Isijekuwa mkewe alikuwa anatafuta watoto nje ili kumsitiri mumewe...
Maana kukiwa hakuna watoto analaumiwa mwanamke kuwa hazai...
Wengine wanaamua kujisovia tatizo kwa kutafuta donor wa mbegu...
Mkuu kama ungelikuwepo labda ungeliamini mimi mwenyewe kwanza nilibisha sana mpaka nikamuamini huyo mshakji yaliyomkuta. Pia nitakuja na uzi hapa kuna jamaa anaharamia mkewe kumbe kishakwenda mahakamani kuomba talaka na kishaolewa na mume mwengine lakini huyu mbeba boksi akizania yeye bado mume na akiharamia kila mwezi.
 
Kama mtoto hafanani na mimi,babaangu,mamaangu,babu au bibi basi akatafutiwe babaake maana huyo sio wangu,na akifanana na mamaake pia haisaidii
 
hapa ndio huwa inafikia mtu kujuta kuowa ,nashkuru sana mitoto yangu huhitaji DNA ila kuna kimoja bado kama sina uhakika,lakini haina shaka mtoto mtoto tu
Mkuu hii post yako nimecheka mno...kwamba kuna kamoja bado hukaelewi....lol hawa wanawake wanajijua wenyewe tu aisee.
 
Guyz ebu watu kuweni serious, unachomekewaje bundi kwenye familia bila kujua??? watu watumie muda na watoto, wachunguzeni tabia, maumbile na hata uelewa(akili), utajua tu kama ni wako au la!...watoto wanne wote wa nje??? huyo mke inabidi apelekwe kwa Mungu ili akasamehewe huko juu.
Mimi nilipokuwa mdogo ami yangu (kaka yake baba yangu) alinita na kuniangalia kidole cha Gumba. akasema wewe kweli mtoto wa ndugu yangu akasema kabila yetu wote lazima kidole gumba kiwe kama hivi. akanionesha chake kipo sawa na changu na kaka zangu na baba yetu sote vimefanana na kila akija mtu wa kabila yetu ni kweli vimefanana. hii ni alama kubwa mpaka sasa ndio natumia.
 
Haiwezekani watoto wote wasiwe wake...
Si bure ...
Isijekuwa mkewe alikuwa anatafuta watoto nje ili kumsitiri mumewe...
Maana kukiwa hakuna watoto analaumiwa mwanamke kuwa hazai...
Wengine wanaamua kujisovia tatizo kwa kutafuta donor wa mbegu...

Hiyo ni wrong approach kusolve tatizo.
Hapo ndo ameharibu zaidi. Labda alikuwa hampendi huyo jamaa.
 
Mimi nilipokuwa mdogo ami yangu (kaka yake baba yangu) alinita na kuniangalia kidole cha Gumba. akasema wewe kweli mtoto wa ndugu yangu akasema kabila yetu wote lazima kidole gumba kiwe kama hivi. akanionesha chake kipo sawa na changu na kaka zangu na baba yetu sote vimefanana na kila akija mtu wa kabila yetu ni kweli vimefanana. hii ni alama kubwa mpaka sasa ndio natumia.
FINGER PRINT....Sawasawa kabisa mkuu...hawa wazee wetu walijua kutumia fingerprint kwenye utambuzi wa watu, ilikuwa vigumu mno kwao kuchomekewa bundi...sasa sikuizi sijui imekuwaje yaani four kids yet both are bastards...ngumu kumeza.
 
Tunaofanana na babazetu Hapa tunasoma comment huku Tunashushia na kinywaji laini
 
Ni nchi gani hiyo ya Ulaya ambayo ukiomba makaratasi ya watoto wanawapima DNA?

Halafu, mtoto kuwa wa kwako legally lazima awe biological?

Na ni kwa nini aitwe kwenye ubalozi badala ya ofisi za uhamiaji?

Na kama mke alikuwa amepata visa kasoro watoto, hao watoto walipimwa DNA wakiwa wapi, Mwananyamala Hospital?

Na ni nchi gani ambayo daktari anatoa matokeo ya uchunguzi kwa ubalozi na wewe mwenyewe hutaarifiwi na daktari?

Taja hiyo nchi mzee!
 
Baba naniii ashukuru sana sijamchomekea... ila nyie vile tu hamna uwezo wa. kubeba mimba case zenu zingekua kubwa zaidi... pole kwa jamaa
 
Back
Top Bottom