Ubadhirifu Ofisi ya CAG

Naomba mnieleweshe wadau. Hivi ni nani anakagua hesabu sa CAG?
Hili ni jipu kubwa sana serikalini!! Wakianza ukaguzi katika taasisi ya umma wanatoa vitisho kwa lengo la kupata rushwa na wakiona hamtishiki basi watatoa hoja ambazo hazina miguu wala kichwa!!!

Kwa kifupi ofisi hii haikaguliwi na taasisi yo yote nchini na pia CAG mwenyewe ana kinga ambayo hata Rais hawezi kumchukulia hatua!!!
 
Naona huko Mtanzania kuna mradi wa kumchafua Prof.Asad,walianza na kwenda nje bila kibali.Na huyo afisa wa CAG anayetumiwa tutampata tu,asidhani yupo salama
Mkuu mimi sikutaka kuzungumza mengi lakini jambo hili li wazi, mlengwa mkuu wa upuuzi huu ni huyo Prof. wa watu!!! Hawana hata aibu vyeo havitafutwi kwa njia ya kihuni na fitina - piga kazi kwa uwadirifu mambo mengine yatajipa yenyewe.
 
Mimi naona kuna kila dalili la kutaka kumchafua Prof. Na tatizo kubwa ni watu wamekatiwa mirija waliyokuwa wakitumia kuinyonya serikali. Lakini baada ya muda ukweli utajulikana. Mungu yupo!!!
 
Ajira zimekua kama kufanya biashara kuaharibiana ili mwingine apate soko..hata kama ni mtendaji mzuri..habari ipo ipo tuu harafu ipo front page...
Mkuu na kibaya zaidi unaweza kukuta sataka zima ni an inside job - afisa/mafisa walio ajiriwa katika ofisi ya CAG ndio wanasambaza disinformation hizi kwa lengo la kumchafua CAG - wasitumie hasira zao za kushindwa kupewa Cheo cha u CAG kwa kimbilia kumchafua Prof. wakumbuke Rais ana uhuru wa kumtehuwa yeyote kutoka nje au ndani ya Ofisi ya CAG na silazima atakoke ndani ya Ofisi ya CAG, kwa hiyo msimpige vita Professor wa watu.
 
M
Isome uielewe.. Mbona ipo straight forward!!
CAG kakiri kw kusema akipatikana mtoa siri atafukuzwa kazi mara moja!
Majungu tu has a gazeti LA mtanzania pro umewekwa na Mungu na atakae kuondowa ni Mungu. Wewe ni msomi wa hali ya juu hivyo vidagaa visikubabaishe piga kazi tu na hichi kipeperushi achana nacho
 
Kama kweli kuna utaratibu wa kununua magari na Ofisi yake imekiuka pamoja na ushauri walipewa na GPSA hapo hamna cha kupakana matope ni Ubadhirifu . hata suala la safari alizoenda taritabu lazima zifuatwe kama alikiuka naye ni jipu
 
Tuna safari ndefu sana wabongo! Bado hatuna nia wala utashi wa kuuita uovu/ubadhirifu kwa jina lake! Ili uovu ukemewe au utetewe unategemea "nani mhusika"! Kama ofisi ya CAG imefanya ubadhirifu, utabakia ni ubadhirifu tu hata kama watu watamtetea vipi hapa Jukwaani! Na kama ni majungu, ofisi yenyewe ya CAG ina wajibu wa kulishitaki gazeti husika ili sheria iweze kuchukua mkondo wake!
 
Kuchafuana ni sifa yetu watanzania, uwezo wa kuchimbana na kutafuta habari za mtu tunao tena mkubwa sana, lakini uwezo wa kufanya research za kimaendeleo ili tuweze kufaidika na rasilimali zinazotuzunguka ni zero. Inasikitisha sana.
 
Kila mtu auchukue mzigo wake mwenyewe kama amefisadi na yeye atumbuliwe tu.
 

Si ndio CAG huyu huyu ambaye tunaambiwa amejenga msikiti ndani ya ofisi ya umma na kutumia pesa ya umma kusafiri kwenda Nairobi kuhudhuria mhadhara wa siasa kali?! JPM kazi anayo.
 
Makafiri washaanza kumchafua Alhaj Assad
Gazeti la Mtanzania linamilikiwa na Habari Corporation, na hi ni miongoni mwa makampuni ya bwn Rostam Aziz. Sijui naye ni kafiri? well, kama profesa Assad sio kafiri halafu kapiga mihela ya namna hiyo; kwa viwango vya UKAFIRI kama ulivyosema basi bora kua KAFIRI asiyemjua Mungu kuliko kumjua Mungu halafu unapiga namna hiyo. Sorry nimekumbuka, zipo dini nyingine zinafundisha kua, ukimuibia kafiri au serikali sio dhambi bali dhambi kumuibia "mwenzio" Sina hakika kama na wewe ni muumini mwa dini hiyo.
 
😳😳Kama naota vile yaani CAG anahitaji CAG kumCAG duh...............Kama ndiyo mambo yalivyo basi tukubali hakuna ofisi ya CAG kuna ofisi ya wapigaji.

Sitaki kuwalaumu tena BANDARI wala TRA pigeni tu maana nani ataMCAG, CAG
 
Kaka WIZI hauna mlokole,Kafiri,muislam swala tano wala muislamu swala moja.Mwizi ni mwizi tu.Tusiweke dini kwenye hili.Awajibike CAG na watu wake ,dini yake haiwajibiki hapa.

Ningeomba kwenye hili tutafute ukweli tuweke IMANI za dini zetu pembeni
 
Naona huko Mtanzania kuna mradi wa kumchafua Prof.Asad,walianza na kwenda nje bila kibali.Na huyo afisa wa CAG anayetumiwa tutampata tu,asidhani yupo salama
Kaka issue ni ukweli wa matumizi mabaya ya fedha za umma,kama ametumia madaraka yake vibaya tusimtetee kwa sababu ya IMANI yake.Imani yake ni yake yeye na Mungu wake,siye tutambana kama ametumia vibaya fedha za umma
 
Kaka WIZI hauna mlokole,Kafiri,muislam swala tano wala muislamu swala moja.Mwizi ni mwizi tu.Tusiweke dini kwenye hili.Awajibike CAG na watu wake ,dini yake haiwajibiki hapa.

Ningeomba kwenye hili tutafute ukweli tuweke IMANI za dini zetu pembeni
Nimekuelewa vizuri sana mkuu lakini pia umeyasoma maandishi ya mtu niliye quote? Badala ya yeye kujikita kwenye story analaumu mwandishi kwa maana ya IMANI yake, this is why nilimkumbusha kua mmiliki wa hilo gazeti wapo dini 1 na yeye mwenyewe na huyo mtuhumiwa.
 
Naona huko Mtanzania kuna mradi wa kumchafua Prof.Asad,walianza na kwenda nje bila kibali.Na huyo afisa wa CAG anayetumiwa tutampata tu,asidhani yupo salama
Hii ni vita ya wazi juu ya Prof.Assad!kuna sura hazitakiwi serikalini kwa njama za kuunga unga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…