Japo ni kweli tunadaiwa, na siku zote dawa ya deni ni kulipa, lakini kukamatwa au kuzuiliwa kwa ndege yetu ni janga kwa taifa letu. Watanzania tunapaswa kuwa wamoja katika hili, kushirikiana na serikali yetu kwa moral support ndege yetu inasuliwe, lakini kunaonekana kama kuna uzalendo wa ajabu wa watu kufurahia na kuliongelea kiushabiki majanga kwa nchi yako
Wanabodi, Jumatatu ya leo, nimeipata tena fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa. Leo nazungumzia Uzalendo wa Ajabu wa Watanzania, nchi yako inapatwa na majanga, halafu wewe unafurahi, huu ni Uzalendo wa aina gani?. Kiukweli huu ni Uzalendo wa Ajabu Kabisa kuwahi...
www.jamiiforums.com
P
Hili la kukamatwa ndege zetu mara kwa mara, wengi wetu hata wale tunaoamini ndio maguru wetu, wanalichukulia kisiasa sana badala ya kuangalia kwa upana zaidi, hasa kibiashara.
Binafsi naliona upo uwezekano kuwa ni vita ya biashara "trade war" dhidi ya hili shirika (la Rais, siyo letu) changa linalotaka kuanza biashara kimataifa.
Shirika hili linaloendeshwa kisiasa (siyo kibiashara) kwa kutumia kodi za wanyonge, bila ukaguzi wa matumizi na mapato, automatically linapata kile wanaita "undue advantage" dhidi ya washindani ambao mashirika yao yanakaguliwa kila baada ya miezi mitatu kuyapima uhai.
Kwa kutumia madhaifu yetu (au ya Rais wetu), washindani wamebuni mpango mkakati wa kuhakilisha shirika linaanza kwa taswira kuwa hampo serious na biashara, na wala hamuwezi kuwa reliable partners kwenye biashara.
Madhara yake tuliyaona from day one.
Mfano, badala ya wauzaji wa ndege kuingia makubaliano na sisi ya mikopo nafuu na ya muda mrefu kama wanavyoingia na makampuni mengine, wao wakataka wapewe chao kabisa. Ili mtakapoangukia pua msije mkaanza kusumbuana mahakamani.
Madhara mengine ambayo ni wazi tutayalipia kwa gharama kubwa ni uwezo wetu kuaminika na wateja wa huko nje tunakoamini kuwa tutawafata watalii. Huko sina uhakika kama kuna "mtalii" atakayekubali kupanda ndege ambayo inaweza kupigwa stop wakati wowote. Hii ni sawa na kumshawishi abiria apande basi ambalo anaamini kuwa linaweza kumlaza njiani wakati wowote.
Kwa mwendo huu, sina uhakika kama kodi za wanyonge bado zitatosha kulipia hasara zote hizo kwa ufahari tu wa kuwa angani. Sina uhakika kama wakija wenye akili kuongoza siku za mbeleni kuwa wataendelea kuunguza pesa za wanyonge ili tuwe angani basi.
Nihitimishe