Uarabuni hamna demokrasia, hamna umaskini

Valencia_UPV

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2016
Posts
7,682
Reaction score
9,557
1. Nimetembea na kuishi nchi kadhaa za Qatar, UAE (Dubai, Abu Dhabi na Sharjah), Oman, Kuwait, Saudi Arabia na Bahrain sikuwahi kuona wazawa maskini.

2. Hakuna NGO's kama Afrika.

3. Hakuna kinachoitwa "Demokrasia".

Sasa, huku Afrika 24/7 NGOs kila mtaa, vyama vya upinzani kila kukicha kiongozi wa chama cha upinzani ni tajiri ajabu, ni kupinga tu. Ila huyo kiongozi analipwa posho za ubunge kwa kodi za wananchi. Inasikitisha sana.









 
Siyo Uarabuni kote, Yemeni, Lebanon, hata Afrika ya Kaskazini kuna Waarabu pia na masikini sana tu.
Mtoa mada ametaja kabisa Nchi anazozingumzia Qatar, Kuwait, Oman, Bahrain, Saudi Arabia na UAE wewe umeenda kuongeza Yemen na Afrika Kaskazini. Haya weka na Somalia basi ufurahi maana Wagalatia huoni raha bila kuchomeka maneno ya kero
 
Mtoa mada ametaja kabisa Nchi anazozingumzia Qatar, Oman, Bahrain, Saudi Arabia na UAE wewe umeenda kuongeza Yemen an Afrika Kaskazini. Haya weka na Somalia basi ufurahi maana Wagalatia huoni raha bila kuchomeka maneno ya kero

Amesema Uarabuni, soma kichwa cha habari, isitoshe Wasomali siyo Waarabu!
 
Nchi ulizotaja nimezitembelea na zingine nimeishi kabisa. Saudi Arabia unajua mtiti na purukushani za upinzani katika maeneo kama Qatif? Bahrain bila kuenda mbali. Manama mpaka leo upinzani ni moto wa kuotea mbali, Qatar na UAE wanafanya mambo katika mtindo wa people centered na haki sawa kwa wote ndio maana husikii chochote.
 
Kwa hiyo Hashim Rungwe analipwa posho za kibunge? Haturudi kwenye uchaguzi.
 
Nenda kaishi huko.
 
Kichwa chako box tupo, inaonyesha ulikuwa huko unashinda bila nguo mudawote..
 
Hapo nchi ulizotaja hapo zinaongozwa kifalme kwani Tanzania inaongozwa kifalme
 
Walafi wachoyo na waroho wa madaraka ipo siku mtasema Wachina hawana dini siyo wakristu wala waislaam wanaabudu mizimu lakini wana maendeleo na siye tupige marufuku dini! Hao washindani wenu wa kisiasa mnawaita wapinzani wanalipwa kodi siyo za wanachama wenu pekee ni za watz wote! Acheni wananchi wachague viongozi wanaowataka msilete ukiritimba/monopoly ktk siasa
 
Kwa hiyo unataka kusema nini? Ya kwamba utawala wa kimabavu ndio unaleta maendeleo?
Mbona Afrika imejaa umasikini wa kutisha wakati ndio sehemu iliyojaa udkiteta? Kuliko eneo lolote duniani?
Sasa nyingine ukitaka kuongea kitu jifikirie kwanza.
 
Vipi uliona na NGOs/CSOs kule? Je Chaggema kuna demokrasia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…