Uanaharakati ndiyo njia pekee ya kuipata katiba ya wananchi

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,825
35,832
Hakuna asiyejua kuwa wakati kuna mchakato wa (akina Zitto na wenzao) kuandaa misingi ya tume huru ya uchaguzi, wahudumu wa tume hiyo wameendelea kuteuliwa bila hata ya mashauriano.

Ni wazi kuwa kwenye jambo hili nyeti kuna wenye maslahi yao binafsi ndani ya mchakato unaoendelea.

Wananchi kupitia tume huru ya uchaguzi wanahitaji mgombea aliyebora na aliyeshinda tu, ndiye atangazwe kuwa mshindi.

Hilo haliwezi kuamriwa na washindani. Wala suluhisho muafaka haliwezi kupatikana bila ya kuwa na katiba madhubuti ya wananchi.

Kupata katiba ya wananchi ndiyo ulio ukombozi kamili wa kuyaweka mamlaka ya nchi mikononi mwao. Ukweli mchungu, hilo haliwezi kuridhiwa na walio madarakani.

Katika hali isiyokuwa na uhuru kamili wa mihimili, hakuna lolote la maana linaloweza kutegemewa kwa mujibu wa sheria.

Hatupaswi kuogopa kulipa gharama zinazohitajika, kama nia yetu kweli ni kupata katiba ya wananchi. Mkono mtupu haulambwi.

Harakati zozote zinahitaji uongozi.

Chadema inayo nafasi ya kuendelea kutoa uongozi unaohitajika (ambao kwa bahati mbaya) umekosekana tangia Mh. Mbowe kukamatwa.

Ni muhimu kujipanga upya. Tena kukiwa na plan B mkononi katika kila ilipo lazima:

1. Pana haja ya kufanya mabadiliko ya msingi kiuongozi Chadema ili kukiwezesha chama hiki kuendelea kutoa uongozi unaohitajika kwenye harakati hizi.

2. Pana haja ya kuweka wazi mpango mkakati wa mapambano wa kuipata katiba hiyo mpya kwa maslahi ya taifa.

Hakipo cha kuficha kwa maana kinachotakiwa ni kupatikana kwa katiba mpya kwa njia za amani.

Waliweza kina Desmond Tutu wakauondoa ubaguzi wa rangi.

Kwanini isiwe sisi na katiba mpya?
--------------

Angalizo:
1. Minyukano ndani ya CCM haitusaidii kwenye madai yetu ya katiba mpya.
2. Mwendazake hayupo tena, makando kando yake tuhangaike nayo kwenye "haki na maridhiano" baada ya katiba mpya.
3. Agenda yetu ni ya kudumu si marafiki.
 
Tuliza mpira mjomba. Hii ngoma siyo size yako.

Huwa mnakuwa majasiri sana mkiwa nyuma ya baobonya..

Mwanaharakati wa hovyo hata majirani zako hawakujui,,,halafu una expect utaleta changes zozote...
 
Ccm hawawezi kubaki swala la katiba mpya au tume huru ya uchaguzi

Uanaharakati utawalazimisha hata kama hawataki.

Uanaharakati ni kwa mujibu wa sheria na njia pekee ya amani ya kuyafikia malengo.

Chadema wamejipambanua kuwa na utashi wa kuongoza harakati hizi.

Aina za majina haya: "John Heche, Benson Kigaila, Dr. Azavery Lwaitama, Mdude na wa namna zisizokopesha" ni muhimu kuanza kupasha miili moto kuchukua hatamu za uongozi.

Halipo la maana tunaloweza kulitegemea kutokea mahakamani.
 
Huwa mnakuwa majasiri sana mkiwa nyuma ya baobonya..

Mwanaharakati wa hovyo hata majirani zako hawakujui,,,halafu una expect utaleta changes zozote...

Nikukumbushe tena hii ngoma siyo size yako. Usiku sasa. Lala!
 
Panapokuwepo na jitihada za lazima za kuyafifisha madai ya msingi ya wapigania haki, ndio panatakiwa ziongezwe jitihada mara mbili, sio kuzipunguza.

Na hizi jitihada lazima ziongozwe kwa ufundi ili kufifisha mbinu za CCM na vibaraka wa wake watakazokuja nazo kudai Katiba Mpya.

Kuendelea kuidai Katiba Mpya kwa njia zinazoipendeza CCM hakutakaa kuzae matunda, kwani wanajua njia inayotumiwa inawazubaisha wanaoidai wenyewe, na mojawapo ya njia hiyo ni kama kuundwa tume au nyingine yoyote.

Hiyo ni kupoteza muda na pesa, watajumuika wanywe chai vikaoni na lunch mchana, mwishowe muda uishe waseme tunayafanyia kazi mapendekezo ya tume mpaka muda wa uchaguzi utakapofika hapatakuwa na jipya.
 
Panapokuwepo na jitihada za lazima za kuyafifisha madai ya msingi ya wapigania haki, ndio panatakiwa ziongezwe jitihada mara mbili, sio kuzipunguza.

Na hizi jitihada lazima ziongozwe kwa ufundi ili kufifisha mbinu za CCM na vibaraka wa wake watakazokuja nazo kudai Katiba Mpya.

Kuendelea kuidai Katiba Mpya kwa njia zinazoipendeza CCM hakutakaa kuzae matunda, kwani wanajua njia inayotumiwa inawazubaisha wanaoidai wenyewe, na mojawapo ya njia hiyo ni kama kuundwa tume au nyingine yoyote.

Hiyo ni kupoteza muda na pesa, watajumuika wanywe chai vikaoni na lunch mchana, mwishowe muda uishe waseme tunayafanyia kazi mapendekezo ya tume mpaka muda wa uchaguzi utakapofika hapatakuwa na jipya.

Kupigania haki au kupigania ukombozi ni jambo lile lile. Si rahisi, na mafanikio hayawezi kuja kwa kudra za Mola.

Kupigania haki kunataka mikakati na kujitoa kweli kweli.

Chama kinachojitoa kuongoza jitihada za kupigania haki ni lazima kiwe kimedhamiria haswa. Viongozi wake ni lazima waonekane kudhamiria kwa maneno na hata kwa vitendo.

Chama cha ukombozi hakiwezi kutegemea huruma wala hakiwezi kuendesha harakati zake kikiwa baridi. Chama cha ukombozi siyo Saccos.

"Mbona Katiba mpya inanukia?"

Platform ya kutufikisha (baada ya Mbowe kukamatwa) inahitaji ukarabati.

Zinahitajika harakati zaidi "on the ground."

Katiba mpya ipo.
 
Kupigania haki au kupigania ukombozi ni jambo lile lile. Si rahisi, na mafanikio hayawezi kuja kwa kudra za Mola.

Kupigania haki kunataka mikakati na kujitoa kweli kweli.

Chama kinachojitoa kuongoza jitihada za kupigania haki ni lazima kiwe kimedhamiria haswa. Viongozi wake ni lazima waonekane kudhamiria kwa maneno na hata kwa vitendo.

Chama cha ukombozi hakiwezi kutegemea huruma wala hakiwezi kuendesha harakati zake kikiwa baridi. Chama cha ukombozi siyo Saccos.

"Mbona Katiba mpya inanukia?"

Platform ya kutufikisha (baada ya Mbowe kukamatwa) inahitaji ukarabati.

Zinahitaji harakati zaidi "on the ground."

Katiba mpya ipo.
Organisation na new approach inahitajika.
 
Organisation na new approach inahitajika.

Organization na new approach ina maana uongozi. Tuna tatizo la uongozi.

Kwa hakika kama hadi sasa hakuna chama chochote kilichotoa hata tamko la mshikamano na askofu Mwingira, Mzee wa Upako au Askofu Shoo, hadharani basi bado tungali hatuko serious.

Tuna haja ya kurudi kwenye meza ya uchoraji (drawing table), tukaanze kujipanga upya.
 
Back
Top Bottom