Kwanini CCM inapiga chenga kupatikana kwa katiba ya wananchi na kung’ang’ania ambayo hatukushirikishwa?

Mzee wa Twitter

JF-Expert Member
Nov 5, 2023
1,271
2,025
Wadau nawasalimu, hebu tukumbushane kidogo.

Katiba iliyopo ya mwaka 1977 ilitungwa na kuandikwa na makada 40 wa chama kwa mgawanyo wa makada 20 kutoka Tanganyika na makada 20 kutoka Zanzibar.

Mwenyekiti wa jopo hili alikuwa Sheikh Thabit Kombo na Katibu wake alikuwa Mzee Pius Msekwa. Watu hawa 40 walipomaliza kuandika waliyoyataka wao na chama chao mchakato ukaenda bungeni badala ya kuupeleka kwa wananchi ambao kimsingi ndio wenye Katiba yao ukapitishwa ukawa sheria kwa ufupi ni Katiba ya Viongozi.

Hivi sasa wananchi tunataka Katiba ya Wananchi tuipendekeze wenyewe kwa jinsi tunavyoona inafaa kwetu na kwa viongozi wetu. Katiba ambayo itainua uchumi wa wananchi wote bila ubaguzi Katiba ambayo itatenda haki kwa vyama vyote katiba ambayo itasimamia chaguzi zote kwa haki

Katiba ambayo haitakuwa na upendeleo kwa makundi fulani kimaslahi lakini CCM ni kama haitaki kuwepo kwa Katiba ya Wananchi kwani kumekuwa na tume nyingi zilipendekeza hilo suala Rais Mstaafu Kikwete alianzisha mchakato wa Katiba Mpya lakini nao CCM kupitia wabunge wake wakauharibu.

Magufuli yeye aligoma kabisa kuusikia kwa kusema sio kipaumbele na Mama Samia akaturudisha tena nyuma eti tusome Elimu ya Katiba. Zote hizi ni hila za CCM kukataa Katiba ya Wananchi!

Ukweli wananchi tunataka Katiba ya Wananchi sio ile ya makada 40.
 
Wadau nawasalimu
Hebu tukumbushane kidogo
KATIBA iliyopo ya Mwaka 1977 ilitungwa na kuandikwa na MAKADA 40 wa Chama kwa mgawanyo wa Makada 20 kutoka TANGANYIKA na Makada 20 kutoka ZANZIBAR.

Mwenyekiti wa Jopo hili alikuwa Sheikh THABIT KOMBO na Katibu wake alikuwa Mzee PIUS MSEKWA.Watu hawa 40 walipomaliza kuandika Waliyoyataka wao na CHAMA chao mchakato ukaenda BUNGENI badala ya KUUPELEKA kwa WANANCHI ambao kimsingi ndio wenye KATIBA YAO ukapitishwa ukawa SHERIA kwa Ufupi ni KATIBA ya VIONGOZI.

Hivi sasa Wananchi tunataka KATIBA ya WANANCHI tuipendekeze Wenyewe kwa jinsi tunavyoona inafaa kwetu na kwa VIONGOZI wetu.

KATIBA ambayo itainua UCHUMI wa Wananchi wote bila UBAGUZI
KATIBA ambayo itatenda HAKI kwa VYAMA VYOTE KATIBA ambayo itasimamia CHAGUZI zote kwa HAKI
KATIBA ambayo haitakuwa na UPENDELEO kwa Makundi fulani kimaslahi LAKINI CCM ni kama HAITAKI kuwepo kwa KATIBA ya WANANCHI kwani Kumekuwa na TUME NYINGI zilipendekeza hilo suala Rais Mstaafu KIKWETE alianzisha MCHAKATO wa KATIBA MPYA lakini nao CCM kupitia WABUNGE wake wakauharibu
MAGUFULI yeye gautama KABISA kuusikia kwa kusema SIO KIPAU MBELE na MAMA SAMIA akaturudisha tena Nyuma ETI tusome Elimu ya KATIBA
ZOTE hizi ni HILA za CCM KUKATAA KATIBA ya WANANCHI
Ukweli WANANCHI tunataka KATIBA ya WANANCHI sio ile ya MAKADA 40.


Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Wanasubiri wamalize kugawana rasilimali za nchi, nasikia makaa ya mawe nayo yamekwenda, bandari zimeenda kizimkazi,
 
1.Nchi haiwezi kupokwa kwa kipande Cha Karatasi.

2.Washindi na watawala kamwe hawaruhusiwi kuwapa watawaliwa nafasi ya kuandika Historia upya .

Wanapambania kuinjoi katikati ya dhiki na kusherekea ngoma za wanaoteseka.
 
Back
Top Bottom