Uamuzi wa Russia kuivamia Ukraine ni mbinu iliyoshindwa (Strategic Failure)?

Fanfa

JF-Expert Member
Sep 25, 2009
1,815
2,862
Je, Uamuzi wa Russia kuivamia Ukraine ni mbinu au mkakati ulioshindwa (Strategic Failures)? hili ni swali linahitaji majibu.

Sababu mojawapo iliyotolewa na Russia kwa kuhalalisha uvamizi wake nchini Ukraine ilikuwa ni Ukraine kuwa na mpango wa kujiunga EU na baadae NATO.

Russia/Putin alitaka Ukraine iendelee kuwa Neutral country huku ikiendelea kuwa koloni la Russia kama ilivyo kwa jilani yake Belarus ya Lukashenko.

Putin/Russia alikuwa hataki Ukraine ijiunge EU na NATO kwa hoja ya kwamba alikuwa hataki EU na NATO wajitanue na kuisogelea mipaka ya Russia eti kwa hofu ya kuhatarisha usalama wa Russia.

Lakini baada ya kuivamia Ukraine tumeshuhudia nchi kama Sweden na Finland kujitoa kwenye uamuzi wa kuwa Neutral state na kuchukua hatua zaidi za kujiunga na NATO ili kujihakikisha ulinzi wa nchi zao dhidi ya Russia.

Matokea ya maamuzi ya Finland ukazaa matunda na kuruhusiwa kwa kasi ya mwendokasi kujiunga NATO. Sweden naye muda si mrefu ataruhusiwa kuwa mwanachama wa NATO.

Baada ya Finland kujiunga NATO sasa NATO iko ubavuni mwa Russia kwa eneo kubwa kuliko hata kabla hajaivamia Ukraine. NATO imejitanua maradufu na Russia hana cha kuifanya Finland na Sweden pamoja na vitisho vyake vya awali. Mbaya zaidi Ukraine naye mwisho wa siku atajiunga NATO baada ya vita kuisha. Hii itaifanya NATO kujitanua maradufu kwa muda mfupi na Russia asiwe na la kufanya.

Ukraine akiruhusiwa kujiunga na NATO baada ya vita huenda nchi zingine kama Moldova, Georgia, Azerbaijan, Armenia na zingine nazo zikaruhusiwa kujiunga na NATO.

Hivyo basi uamuzi wa Russia kuivamia Ukraine ni mkakati ulioshindwa (strategic Failure), ambapo Russia amepata hasara kuliko faida. Kama sababu ilikuwa ni kuogopa kusogelewa na NATO kwa kisingizio kuwa usalama wa Russia utakuwa hatarini sasa kasogelewa na hana la kufanya.

Hebu tutafakari hoja hizi;

1. Kwa kuwa Finland ni mwanachama wa NATO. Je, Russia atadhubutu kurusha hata bomu la mkono nchini Finland kwa sasa?

2. Russia ana ubavu wa kuizuia Sweden isijiunge na NATO kama ambavyo tuliaminishwa mwanzo na Russia?

3. Je, kitendo cha Russia kuivamia Ukraine ndo kajipalia mkaa zaidi na kujiweka kwenye hatari kuliko alivyofikiria kabla?

4. Je, Russia ataweza kuizuia NATO kutojitanua zaidi kama anavyojigamba au ni kelele za chura kwa ng'ombe kumzuia asinywe maji?

5. Kama Russia atashindwa hii vita na Ukraine kujiunga na NATO atakuwa amepata faida kwa kuanzisha vita dhidi ya Ukraine au hasara.

6. Kama Sweden na Finland wameomba kujiunga na NATO na kukubaliwa katikati ya vita. Je, Russia kapata faida gani?

7. Je, nchi zingine zikiomba kujiunga na NATO atakuwa na ubavu wa kuzizuia kama alivyojaribu kufanya kwa Ukraine na kushindwa?
 
Urusi mpaka Sasa ameweza kuiangusha dollar.

Urusi mpaka Sasa ameigaragaza NATO.

Ukumbuke Hii SMO Urusi akishinda, NATO imekufa,Sweden na Finland malengo Yao yameshatibuliwa.
20230411_222939.jpg
 
Kumbuka Ujerumani na whole European ni economic disaster.

Marekani gharama ya maisha imepanda

Global order imposed by the west ipo mashakani

Dollar dominance imeanza kucrumble

Halafu unasema strategic failure
Are you insane?
 
Urusi mpaka Sasa ameweza kuiangusha dollar.

Urusi mpaka Sasa ameigaragaza NATO.

Ukumbuke Hii SMO Urusi akishinda, NATO imekufa,Sweden na Finland malengo Yao yameshatibuliwa.View attachment 2645284
Sawa, jikite kwenye hoja badala ya porojo.

1. tueleze kivipi NATO imeshagalagazwa?

2. Tueleze ni malengo yapi ya Finland yaliyotibuliwa

3. Tueleze ni vipi USD imeangushwa na kwa kiwango gani?
 
Kumbuka Ujerumani na whole European ni economic disaster.

Marekani gharama ya maisha imepanda

Global order imposed by the west ipo mashakani

Dollar dominance imeanza kucrumble

Halafu unasema strategic failure
Are you insane?

Lete takwimu badala ya porojo. Inaelekea hata abc ya uchumi huna zaidi ya porojo.


1. Uchumi wa German na EU umeanguka kwa kiasi gani. Njoo na takwimu za economic indicators to justify.

2. Maisha ya USA yamepanda kutoka wapi hadi wapi. Tupe economic indicators hata 5 tu zinazoonyesha maisha ya USA yamepanda na kiwango.

3. Tueleze USD imeanguka kwa kiwango gani kwa vipimo vipi? Hebu tupe ulinganifu wa Ruble na $
 
Lete takwimu badala ya porojo. Inaelekea hata abc ya uchumi huna zaidi ya porojo.


1. Uchumi wa German na EU umeanguka kwa kiasi gani. Njoo na takwimu za economic indicators to justify.

2. Maisha ya USA yamepanda kutoka wapi hadi wapi. Tupe economic indicators hata 5 tu zinazoonyesha maisha ya USA yamepanda na kiwango.

3. Tueleze USD imeanguka kwa kiwango gani kwa vipimo vipi? Hebu tupe ulinganifu wa Ruble na $
1. Unataka nikupe takwimu za Ujerumani kiuchumi ila wewe huna sehemu uliyokuja na takwimu zaidi ya bla bla tu.
Unazitaka kwa base ya mwaka gani au ndani ya accounting period ya mwaka huu?

2. Eti USA hujataja economic indicator wakati fuel price imepanda hali ambayo inasababisha whole production sector kuwa na gharama zaidi.

Swali lako lilitakiwa lijikite kuonyesha nimetumia base year ipi na kulinganisha na ipi?

3.unaelewa hata nilichokielezea pale imeanza kucrumble au ni maamuma tu upo Dunia hujui la mbele Wala la nyuma.
 
1. Unataka nikupe takwimu za Ujerumani kiuchumi ila wewe huna sehemu uliyokuja na takwimu zaidi ya bla bla tu.
Unazitaka kwa base ya mwaka gani au ndani ya accounting period ya mwaka huu?

2. Eti USA hujataja economic indicator wakati fuel price imepanda hali ambayo inasababisha whole production sector kuwa na gharama zaidi.

Swali lako lilitakiwa lijikite kuonyesha nimetumia base year ipi na kulinganisha na ipi?

3.unaelewa hata nilichokielezea pale imeanza kucrumble au ni maamuma tu upo Dunia hujui la mbele Wala la nyuma.
Hatuhitaji porojo lete takwimu. Tatizo Pro Russia mlio wengi elimu yenu duni sana. Hamjui mambo mengi sana. Kila kitu porojo tu. Mkiambiwa lete data mnaishia kutukana tu.

Maswali huwa yana takwimu au unayejibu ndo unatakiwa utoe evidence to justify. Umesoma shule za kata nini?
 
Hatuhitaji porojo lete takwimu. Tatizo Pro Russia mlio wengi elimu yenu duni sana. Hamjui mambo mengi sana. Kila kitu porojo tu. Mkiambiwa lete data mnaishia kutukana tu.

Maswali huwa yana takwimu au unayejibu ndo unatakiwa utoe evidence to justify. Umesoma shule za kata nini?
Najua huna hoja
Ila umejaa vihoja
Mimi ni pro Africa
Ila ukileta data zitakazo Pinga hoja yangu nami nitakuletea data zinazosapoti hoja yangu.

Huna data na huna hoja nenda Facebook ukajifunze, huu sio mtandao wa mafanfa
 
Najua huna hoja
Ila umejaa vihoja
Mimi ni pro Africa
Ila ukileta data zitakazo Pinga hoja yangu nami nitakuletea data zinazosapoti hoja yangu.

Huna data na huna hoja nenda Facebook ukajifunze, huu sio mtandao wa mafanfa
Ungekuwa na takwimu ungerukaruka hivo. Threads zingine msiwe mnaziparamia. Zinahitaji great thinkers wanaojua mambo siyo porojo.
 
Ungekuwa na takwimu ungerukaruka hivo. Threads zingine msiwe mnaziparamia. Zinahitaji great thinkers wanaojua mambo siyo porojo.
Kama wewe ndio great thinker basi Tanzania yangu naionea huruma.

Mtu ambaye hata hujui athari ya vita ya Ukraine kiuchumi barani Ulaya na kule America.

Hujui hata mabank mangapi yashafirika kule Ulaya na America.

ndio unajiita great thinker?
You are great thinker indeed
 
Ndo maana mkuu wa Wagner marcinary anawaponda sana wanaomzunguka Putun. Walimdanganya Ukraine ni kama mlevi ukimsukuma. Sasa hivi putin anaishi kama digidigi.
Nikionacho mimi.hata ikitokea russia akashinda vita tayari nchi kama marekani na washirika wake wamefanikiwa kumpima nguvu na wameishajiridhisha kwamba akilianzisha anapigika kirahisi.

Mfano angalia warusi wanavyokufa,ukraine huku wakisaidiwa na mizinga ya masafa marefu kutokea urusi ndani
ambayo ukraine hana.
NATO na marekani walimnyima silaha za masafa marefu,kitu ambacho angekuwa nazo si ajabu sasa hivi wangekuwa ndani ya urusi.
Hivyo maamuzi ya putin kuvamia ukraine na hasara kwake badala ya faida.
Na ni fundisho kwetu .usimdharau jirani yako kwa sababu ya mwonekano,anawezakuwa na marafiki wenye nguvu kuliko zako ukaumbuka.
 
Je, Uamuzi wa Russia kuivamia Ukraine ni mbinu au mkakati ulioshindwa (Strategic Failures)? hili ni swali linahitaji majibu.

Sababu mojawapo iliyotolewa na Russia kwa kuhalalisha uvamizi wake nchini Ukraine ilikuwa ni Ukraine kuwa na mpango wa kujiunga EU na baadae NATO.

Russia/Putin alitaka Ukraine iendelee kuwa Neutral country huku ikiendelea kuwa koloni la Russia kama ilivyo kwa jilani yake Belarus ya Lukashenko.

Putin/Russia alikuwa hataki Ukraine ijiunge EU na NATO kwa hoja ya kwamba alikuwa hataki EU na NATO wajitanue na kuisogelea mipaka ya Russia eti kwa hofu ya kuhatarisha usalama wa Russia.

Lakini baada ya kuivamia Ukraine tumeshuhudia nchi kama Sweden na Finland kujitoa kwenye uamuzi wa kuwa Neutral state na kuchukua hatua zaidi za kujiunga na NATO ili kujihakikisha ulinzi wa nchi zao dhidi ya Russia.

Matokea ya maamuzi ya Finland ukazaa matunda na kuruhusiwa kwa kasi ya mwendokasi kujiunga NATO. Sweden naye muda si mrefu ataruhusiwa kuwa mwanachama wa NATO.

Baada ya Finland kujiunga NATO sasa NATO iko ubavuni mwa Russia kwa eneo kubwa kuliko hata kabla hajaivamia Ukraine. NATO imejitanua maradufu na Russia hana cha kuifanya Finland na Sweden pamoja na vitisho vyake vya awali. Mbaya zaidi Ukraine naye mwisho wa siku atajiunga NATO baada ya vita kuisha. Hii itaifanya NATO kujitanua maradufu kwa muda mfupi na Russia asiwe na la kufanya.

Ukraine akiruhusiwa kujiunga na NATO baada ya vita huenda nchi zingine kama Moldova, Georgia, Azerbaijan, Armenia na zingine nazo zikaruhusiwa kujiunga na NATO.

Hivyo basi uamuzi wa Russia kuivamia Ukraine ni mkakati ulioshindwa (strategic Failure), ambapo Russia amepata hasara kuliko faida. Kama sababu ilikuwa ni kuogopa kusogelewa na NATO kwa kisingizio kuwa usalama wa Russia utakuwa hatarini sasa kasogelewa na hana la kufanya.

Hebu tutafakari hoja hizi;

1. Kwa kuwa Finland ni mwanachama wa NATO. Je, Russia atadhubutu kurusha hata bomu la mkono nchini Finland kwa sasa?

2. Russia ana ubavu wa kuizuia Sweden isijiunge na NATO kama ambavyo tuliaminishwa mwanzo na Russia?

3. Je, kitendo cha Russia kuivamia Ukraine ndo kajipalia mkaa zaidi na kujiweka kwenye hatari kuliko alivyofikiria kabla?

4. Je, Russia ataweza kuizuia NATO kutojitanua zaidi kama anavyojigamba au ni kelele za chura kwa ng'ombe kumzuia asinywe maji?

5. Kama Russia atashindwa hii vita na Ukraine kujiunga na NATO atakuwa amepata faida kwa kuanzisha vita dhidi ya Ukraine au hasara.

6. Kama Sweden na Finland wameomba kujiunga na NATO na kukubaliwa katikati ya vita. Je, Russia kapata faida gani?

7. Je, nchi zingine zikiomba kujiunga na NATO atakuwa na ubavu wa kuzizuia kama alivyojaribu kufanya kwa Ukraine na kushindwa?
Mwenyewe umeona una point za nguvu 🤣🤣🤣🤣 Mleta uzi una tatizo la kukariri mambo.

Sababu y Russia kuitandika Ukraine ni nyingi sana lakini media za mgharibi hazisemi ukweri badala yake mmekaririshwa sbabu moja tu eti

Kuhusu Finland na Sweden kujiunga NATO, Russia walishasema hawana tatizo na hilo ila ita react iwapo mifumo na zana za kijeshi a NATO zikipelekwa Finland. Na kumbuka Russia akitoa ahadi huwa hatanii na ninakuahidi iwapo haya aliyoyaonya yakitokea, Finland itashambuliwa na joka la kibisa NATO hawataweza kufanya kitu chochote kile
 
Kama wewe ndio great thinker basi Tanzania yangu naionea huruma.

Mtu ambaye hata hujui athari ya vita ya Ukraine kiuchumi barani Ulaya na kule America.

Hujui hata mabank mangapi yashafirika kule Ulaya na America.

ndio unajiita great thinker?
You are great thinker indeed
Tutajie mabenki yaliyofirisika Ulaya na America sababu ya vita ni yapi?
 
Back
Top Bottom