singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,538
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imepigilia msumari wa mwisho katika kambi ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) bada ya kutangaza kuwa kura za urais, ubunge na madiwani zitahesabiwa kwenye vituo vya kupigia kur kwa uwazi.
Uamuzi huo ni pigo kwa Ukawa ambao tayari wameanza kuchungulia mgombea wao wa urais Edward Lowassa kushindwa na mgombea wa Ccm Dk. John Magufuli kuanza kutumia ujanja wa kulalamika kwmba wataibiwa kura wakati wa kusafiriisha masanduku ya kura wakati wa uchaguzi ili wafanye fujo.
Jumanne wiki hii Mwenyekiti wa NEC Jaji Mstaafu Damiani Lubuva, alisema kura zote za urais, wabunge na madiwani zitahesabiwa katika vituo vya kupiga kura na matokeo yote kutangazwa hapo hapo na marufuku kusafirisha masanduku ya kupigia kura kama ilivyokuwa zamani.
Alisema ktika uchaguzi w mwka huu marufuku kuhamisha masanduku ya kura kwa sababu vituo vya kupigia kura vitbdilika na kuwa vituo vy kuhesabia kura baada ya upigaji kura kumalizika.
" kura zote za urais, ubunge na udiwani zitahesabiwa katika kila kituo na matokeo yatabandikwa vituoni hapo hivyo sijui wanaosema kura zitaibiwa zitaibiwaje", alisema Jaji Lubuva na kuongeza " baada ya matokeo kubandikwa katika kila kituo yatapoelekwa katika kata husika kujumlishwa na hapo pia yatabandikwa,
"Mshindi wa udiwani atatangazwa hapo na Yule wa ubunge na urais yatapelekwa jimboni ambako yatajumlishwa na mshindi wa ubunge kutangazwa na kukabidhiwa cheti huku uris yakipelekwa makao makuu ya tume.
Alisema njia hiyo itasaidia matokeo kufika haraka kama inavyotakiwa na baada ya tume ya uchaguzi kupokea matokeo hayo yatatangazwa moja kwa moja kupitia luninga na redioni.
Kutokana na hali hiyo alivishauri vyama vya siasa viache kauli za kuwataka wafuasi waowasiondoke kwenye vituo vya kupiga kura kwa vile hakuna kura zitakazoibiwa.
Kauli ya Lubuva ni mwiba kwa Chadema na Ukawa kwa sababu tayari walishawamoinisha wafuasi wao wataibiwa kura hivyo wafanye fujo, wakati wakijua wazi kuwa mgombea wao atashindwa kihalali ktika uchaguzi huo.
Habari za zilizopatiakana kutoka ndani ya chadema zinaeleza kuwa mwenendo wa mgombea wao, Lowassa katika kampeni zmeanza kuwatia wasiwasi na kwamba sasa wameanza kushawishi wafuasi wao wafanye fujo ili kuvuruga uchaguzi.
Habari hizo zinaeleza kuwa tayari chama hicho kimetoa mafunzo mafunzo ya kwa vijana 3,000 nchini ambao watasambazwa katika vituo vya kupig kura ili wanzishe fujo baada ya matokeo kusambazwa.
Mtoa habari wetu aliye karibu na chama hicho anasema kuwa lengo kuwa la kufanya hizo ni kutaka kuiweka serikali ya rais Kikwete katika matatizo ya mahakama kimataifa ya uhalifu.
Wanasema urais wanajua hawatapata, lakini mgombea wao Lowassa na wafuasi wake hususani waliotoka ccm hivi karibuni wanataka kuona rais Kikwete naye anaishi katika matatizo mazito ya kupelekwa ICC.
Chanzo: Dira
Uamuzi huo ni pigo kwa Ukawa ambao tayari wameanza kuchungulia mgombea wao wa urais Edward Lowassa kushindwa na mgombea wa Ccm Dk. John Magufuli kuanza kutumia ujanja wa kulalamika kwmba wataibiwa kura wakati wa kusafiriisha masanduku ya kura wakati wa uchaguzi ili wafanye fujo.
Jumanne wiki hii Mwenyekiti wa NEC Jaji Mstaafu Damiani Lubuva, alisema kura zote za urais, wabunge na madiwani zitahesabiwa katika vituo vya kupiga kura na matokeo yote kutangazwa hapo hapo na marufuku kusafirisha masanduku ya kupigia kura kama ilivyokuwa zamani.
Alisema ktika uchaguzi w mwka huu marufuku kuhamisha masanduku ya kura kwa sababu vituo vya kupigia kura vitbdilika na kuwa vituo vy kuhesabia kura baada ya upigaji kura kumalizika.
" kura zote za urais, ubunge na udiwani zitahesabiwa katika kila kituo na matokeo yatabandikwa vituoni hapo hivyo sijui wanaosema kura zitaibiwa zitaibiwaje", alisema Jaji Lubuva na kuongeza " baada ya matokeo kubandikwa katika kila kituo yatapoelekwa katika kata husika kujumlishwa na hapo pia yatabandikwa,
"Mshindi wa udiwani atatangazwa hapo na Yule wa ubunge na urais yatapelekwa jimboni ambako yatajumlishwa na mshindi wa ubunge kutangazwa na kukabidhiwa cheti huku uris yakipelekwa makao makuu ya tume.
Alisema njia hiyo itasaidia matokeo kufika haraka kama inavyotakiwa na baada ya tume ya uchaguzi kupokea matokeo hayo yatatangazwa moja kwa moja kupitia luninga na redioni.
Kutokana na hali hiyo alivishauri vyama vya siasa viache kauli za kuwataka wafuasi waowasiondoke kwenye vituo vya kupiga kura kwa vile hakuna kura zitakazoibiwa.
Kauli ya Lubuva ni mwiba kwa Chadema na Ukawa kwa sababu tayari walishawamoinisha wafuasi wao wataibiwa kura hivyo wafanye fujo, wakati wakijua wazi kuwa mgombea wao atashindwa kihalali ktika uchaguzi huo.
Habari za zilizopatiakana kutoka ndani ya chadema zinaeleza kuwa mwenendo wa mgombea wao, Lowassa katika kampeni zmeanza kuwatia wasiwasi na kwamba sasa wameanza kushawishi wafuasi wao wafanye fujo ili kuvuruga uchaguzi.
Habari hizo zinaeleza kuwa tayari chama hicho kimetoa mafunzo mafunzo ya kwa vijana 3,000 nchini ambao watasambazwa katika vituo vya kupig kura ili wanzishe fujo baada ya matokeo kusambazwa.
Mtoa habari wetu aliye karibu na chama hicho anasema kuwa lengo kuwa la kufanya hizo ni kutaka kuiweka serikali ya rais Kikwete katika matatizo ya mahakama kimataifa ya uhalifu.
Wanasema urais wanajua hawatapata, lakini mgombea wao Lowassa na wafuasi wake hususani waliotoka ccm hivi karibuni wanataka kuona rais Kikwete naye anaishi katika matatizo mazito ya kupelekwa ICC.
Chanzo: Dira