Mwana wa Mungu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2008
- 1,003
- 83
MALAWI Wameshashirikisha wanasheria wao sana na bila shaka wanayo makundi ya wanasheria wanaoshughulikia suala hili la ziwa nyasa. simaanishi wanasheria wa nje, la, wanashirikisha maprof mbalimbali kutoa sababu za kisheria, sio siasa za maneno ni kwanini wao ndo wanamiliki ziwa na siyo Tanzania. SWALI: Tanzania imejiandaa vipi na kukabiliana na suala la malawi? pale kwa Attorney General, ameandaa wanasheria wake wepi au amewapa kazi wepi ambao kazi yao ni kuandika maopinion ya kufa mtu na kufanya research na kuandaa sababu ambazo Tanzania inaweza kubase juu ya ziwa nyasa?au tumelala tu wakati malawi miaka yote wako macho na ziwa lao?
ajabu ni kwamba, Tanzania mara nyingi tumelala kuhusu ziwa hili ndio maana malawi hadi leo hawaamini kama ni letu pia. wao walikuwa wanapiga kampeni ya chini kwa chini, wakifundisha watoto wao, na kupenyeza kwenye ramani za dunia, google na kila sehemu wakionyesha mpaka, na sisi tanzania tulichukulia kawaida tu wala hatukurespond chochote, sasa tayari wameshauambia umma wa dunia kuwa ziwa ni lao na dunia inaamini hivyo, kilichobaki ni kwetu sasa kuleta hoja za kisheria kuthibitisha kuwa tuna haki kwenye ziwa hili...tumekumbuka shule wakati kumekucha na mbu wameng'ata hadi wameshiba. lakini bado tunayo nafasi, zaidi ya kuwa tunazo sababu ya kuwa labda :
ajabu ni kwamba, Tanzania mara nyingi tumelala kuhusu ziwa hili ndio maana malawi hadi leo hawaamini kama ni letu pia. wao walikuwa wanapiga kampeni ya chini kwa chini, wakifundisha watoto wao, na kupenyeza kwenye ramani za dunia, google na kila sehemu wakionyesha mpaka, na sisi tanzania tulichukulia kawaida tu wala hatukurespond chochote, sasa tayari wameshauambia umma wa dunia kuwa ziwa ni lao na dunia inaamini hivyo, kilichobaki ni kwetu sasa kuleta hoja za kisheria kuthibitisha kuwa tuna haki kwenye ziwa hili...tumekumbuka shule wakati kumekucha na mbu wameng'ata hadi wameshiba. lakini bado tunayo nafasi, zaidi ya kuwa tunazo sababu ya kuwa labda :
- suala hili halijawahi kutatuliwa, bado liko kwenye mgogoro tangu uhuru, hivyo tulikuwa tunaishi na mgogoro, kama mgogoro ulikuwa haujatatuliwa tangu uhuru, malawi leo hawawezi kusema sisi hatuna kitu kwasababu mgogoro haujawahi kutatuliwa.
- watu wa tz wamezaliwa mle na tz imekuwa ikiendesha shughuli zake mle, ndo maana tunazo hadi bandari na tumekuwa tukisafirisha vitu kwa meli zetu mle...kama tumejenga bandari za mbambabay, tumesafirisha bidhaa miaka yote hii, tumevua samaki, inakuwaje leo malawi waseme sio letu, mtu anaweza kujenga bandari, kuvua na kufanya navigation kwenye ziwa ambalo si lake?
- mikataba ya ukoloni ilikuwa ya ulaghai, watz hatuikubali kwasababu ilikuwa ya kilaghai.
- Serikali ya Tz iunde jopo maalumu pale kwa Attorney General kushughulikia masuala ya kimataifa tu, na wapewe kazi ya kufanya research na kuandaa points of law kutetea tz katika jambo hili.
- tutumie wasomi wetu vyuoni,..pale udsm kuna wanashera kama kina prof. Peter Maina etc, watumiwe vilivyo katika suala hili.
- kiujumla, tusijelala tena, kwasababu wamalawi hawalali hata siku moja katika jambo hili, tuwe macho kijeshi na kisheria kutetea ziwa hili. Asanteni, Mungu ibariki Tanzania. nawakilisha.